Wanasheria msikubali TLS ikanajisiwa

Iwapo wanajeshi wanapewa ukuu Wa Wilaya na Mikoa, iwapo mwanajeshi anaongiza idara nyeti ya CCM.

Iwapo naibu mwanasheria mkuu Wa serikali anateuliwa kuwa mbunge kwa tiketi ya CCM

Iwapo naibu mwanasheria mkuu toka mhimili uliojichimbua chini zaidi ya yote anakwenda kuongoza mhimili Wa bunge la wananchi

Iwapo hapo ndipo tumefikishwa naona acha tuendelee tu.

Tunasubiria na uchaguzi Wa chama cha wafanyakazi, chama cha walimu napo tuweke majembe ndo nchi itasimama vizuri
 
Stolla,Frank na.wasongo hawa wote ni Makada wa CCM tena mmoja aligombea mpaka nafasi ya urais.

Pole.Lissu ni Mtanzania anayohaki sawa na kada wa CCM
Suala sio UKADA, au kuwahi kugombea nafasi Fulani..., hoja ni kuwa na nafasi ya UONGOZI ndani ya chama.
Nani kati ya hao uliowataja yuko kwenye safu ya viongozi wa KITAIFA kama Lissu alivo CDM...!??
 
Memba wa TLS naona mwaka huu wanaona kweli siasa inewaingilia, lazima inawachosha wengi wao.

Wamenishangaza why wengine wasio kwenye vyama huku na kule kea media kila leo, hawajawania cheo hicho naamini na haya yote mtu angepita bila tabu kwa sasa.
WE MAMA TLS ILIKUWEPO KABLA HATA TANU HAIJANZISHWA....EBOOO

OVA
 
Zitto akiwa mwenyekiti wa PAC alikopeshwa pesa na NSSF shirika analopaswa kukagua mahesabu take tume ya maadili imekaa kimya wanasiasa wetu hawaaminiki wako kwa ajili ya kuwaibia wananchi
 
Suala sio UKADA, au kuwahi kugombea nafasi Fulani..., hoja ni kuwa na nafasi ya UONGOZI ndani ya chama.
Nani kati ya hao uliowataja yuko kwenye safu ya viongozi wa KITAIFA kama Lissu alivo CDM...!??

Kwenye Katiba yao imeelezwa kwamba ukiwa kwenye nafasi fulani hugombei uongozi TLS??Kama hapana basi funga tu mdomo.Mawakili wana AKILI ndiyo sababu wameamua walichoamua.

Tubaki watanzania mazuzu kuchagua Ma....z...........zu
 
Nianze kwa Salaam,

Nimeguswa na majibizano yanayoendelea kuhusu haki ya Tundu Lissu kugombea Urais wa TLS. Aidha nimechangia mijadalaa mingi inayohusu TLS na TL.

Kwa hili, hoja yangu natumia mfano wa ZITTO Kabwe
Zitto alikuwa M/kiti wa PAC, kamati ya BUNGE ya mashirika ya Umma(na asasi zote zinazopokea fedha kutoka Serikalini). Ndani ya kamati waliona fedha za SERIKALI zinazotolewa kwa vyama vya Siasa kama Ruzuku hazitumiki ilivokusudiwa. Alisimamma Bungeni na kuomba Mkaguzi Mkuu(CAG) kukagua hesabu za Vyama vyote vya Siasa, tena aanzie Chama chake-CDM.

Mapokeo ya Tamko hilo yalikuwa tofauti, kila mtu kivyake, wengine waliona kitendo kile kama uzalendo, wengine ujasiri,wengine unafiki na wengine usaliti.

CDM walimuona MSALITI, kupitia Vikao rasmi Chamani waliamua kumhoji, kumsulubu na wakanitumia hiyo Kama ni hoja mojawapo kumfukuza Chamani, wakatamka wazi kwamba alipaswa awatonye ili waweke Mambo sawa ndipo atoe hoja ile na hatimae CHADEMA ingeonekana SAFI.

Ambacho hatujui kwa hakika ni dhamira ya ZITTO nyuma ya hoja yake
1. Alikuwa mzalendo wa kweli?
3. Alikuwa Mnafiki?
4. Alikuwa MSALITI akitumia nafasi ile kumshughulikia MBOWE?

Hii ndio dhana Halisi ya Mgongano wa maslahi yaani COMFLICT OF INTEREST. ZITTO Asimame na PAC au CHADEMA?

Kwa wenzetu, conflict of interest inatosha kumfukuzisha Mtu kazi au kumnyima kazi.

Yaliyomtokea ZITTO lazima yatatokea kwa Lissu ambapo atalazimika achague kati ya TLS na CHADEMA.

Ikatokea wamepishana na MBOWE Basi tutegemee TLS kutumika kumuadhibu MBOWE kama Zitto alivoitumia PAC. Kinyume chake kama watabaki jinsi walivyo leo basi tutegemee TLS kubeba Agenda za CDM tena kwa maelekezo mahususi.

TUNDU LISSU
Nionavyo Mimi TL binafsi, anatafuta jukwaa la kusemea na kusikika ili kufurahisha na kujikusanyia mashabiki na kujijengea umaarufu kisiasa na kibiashara (Uwakili).

Anatafuta jukwaa jipya baada ya kulinajisi lile la awali - POLITICAL PLATFORM.
TL ni Mbunge, ni Mwanasheria Mkuu wa CDM, Kiongozi mwandamizi CDM n.k, chochote asemacho, atendacho ni Habari, vyeo hivi vimempa jukwaa adhimu la kusemea. Je amelitumiaje jukwaa hili?

Amekuwa mchambuzi, mkosoaji/mshauri wa SERIKALI na hususan Raisi. Tatizo lake kubwa ni APPROACH, bila upotoshaji, kejeli, dharau, kashfa na Matusi, basi TL hajafanya Siasa.

Kisaikolojia, huwezi kumtusi, kumkashifu, kumdharau au kumkejeli Mtu halafu utegemee afuate ushauri wako. Naamini kuna tofauti ndogo sana kati ya JPM na TL katika kuchagua maneno jukwaani.

Kupitia TL nafasi na hadhi ya UPINZANI ktk SERIKALI ya JPM imepotea kabisa hawasikilizwi wala kushirikishwa. Bado nakumbuka jinsi JPM alivokata tamaa na UPINZANI mpaka kufikia kusema "UKIONA MPINZANI ANAKUSIFIA JIULIZE UMEKOSEA WAPI" matokeo yake sote tunayajua
Leo hii hata Diamond Platnumz anasikilizwa kuliko TL, ndio kwa sababu yeye kaonyesha Busara zaidi ya TL.

Je, mapungufu haya sasa ndio tunataka yahamie TLS, ili nao wabezwe,wasisikilizwe.

OLENI SANA TLS
Pamoja na umahiri wake kitaaluma lakini TL bado ana matatizo ktk ueledi ndio kusema sijaona mchango wake pale CHADEMA kwa matatizo ya Msingi kama Katiba ya Chama, au kumshauri MBOWE ktk mambo yanayoathiri taswira ya Chama kama Ukabila,Ukanda, Udini, Ufisadi Chamani, Matumizi mabaya ya Ruzuku, achilia mbali matatizo binafsi ya M\Kiti, kama ukwepaji kodi, utakatishaji fedha, ulipaji wa madeni, ufuska, udikteta na upendeleo. Yote hayo yote yamemshinda sasa anataka atengeneze TLS.

Anyway, sishangai tena. maana ni ajabu kubwa wanasheria kushindwa kuweka sheria dhidi ya Conflict of Interest, kushindwa kuweka kanuni na sifa za Mgombea, kanuni zitakazo wafanya TLS kuwa asasi huru dhidi ya external interference toka SERIKALI au POLITICAL PARTIES.

Sishangai kusikia Lissu kateuliwa na hawa Learned Brothers kuwa Rais wao. Ndio, bado nakumbuka barua toka kwa Kaka zao, Wanasheria wa Afrika Mashariki waliomwandikia Mwakyembe wanasema wazi juu ya haja ya kuwa chombo huru kisichoingiliwa. Lakini wanarudi kupinga dhana hii kwa kisingizio rahisi ati siku hizi haiwezekani kupata Mwanasheria ambaye hana mapenzi na Chama Fulani.

Duuuh, hii nayo kali eti wao wanashindwa kutofautisha ushabiki wa Chama na kuwa kiongozi wa Chama.

Kama ni sawa kwa Mwanasheria Mkuu CHADEMA kugombea Basi uchaguzi Mkuu ujao Mwanasheria Mkuu wa CCM naye agombee, bila shaka sio vibaya hata Mwanasheria Mkuu wa SERIKALI ((AG),, baadae Jaji Mkuu Mpaka DPP maana na wenyewe ni Learned Brothers pia..!!!

Naam, sio ajabu INCHI yangu inaongoza kwa kuwa na mikataba mibovu, inayotafuna Maliasili zetu iliyoandaliwa au kukubaliwa na hawa ndugu zetu.

Sasa nimeelewa kwa nini Lissu ni jembe, maana anatambua kwamba wenzie ni mbumbumbu ambao hawawezi kuona ubaya wa yeye kugombea.

Hongera Lissu kwa New Platform nalo kojolea ukiweza acha kinyesi linuke hasa then tafuta another platform keep it up.
 
Back
Top Bottom