Hute
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,537
- 6,458
nilipanda gari moja toka dsm kwenda khm, nilikaa na jamaa mmoja ambaye ni diwani wa chadema, mle ndani ya basi kulikuwa na majibizano mengi ya kisiasa na kuwa mwaka 2015 cdm lazima iende magogoni. cha ajabu, waliibua issue moja juu ya umiliki wa hotel ya mongo, iliyopo kahama mjini, wanasema jamaa aliinunue ile hotel. pamoja na kwamba inaweza kuwa na jina la mtu mwingine, ile hotel watu kule kahama hata ukiuliza raia wa kawaida atakwambia ni ya maige...nilijiuliza kapata wapi pesa kununua au kujenga nyumba ya kuishi ya bilioni, alafu akanunua na hotel gorofa nne kama ile....hapo hapo wanasema alibadilisha afisa misitu kwenye gave reserve gani sijui huko shinyanga akaweka wake wakawa wanapitisha mbao kama njugu na yeye kuzifanyia biashara...kuna tuhuma nyingi sana kule jamani kwa wale waliofika, nendeni leo kahama mkajionee au kaulizeni mtu yeyote mtaani hata mwendesha baiskel tu. halafu hayuko fresh kabisa na lembeli, nasikia hawaivi kwasababu lembeli mbunge alimanika mshikaji....