Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,788
- 218,420
Kuna maneno maneno yanazunguka humu JF na kwingineko kutoka kwa Mamluki wanaotumikishwa, kwamba Wagombea Ubunge wa CHADEMA wamejimilikisha majimbo, na kwamba eti wale wagombea wa CHADEMA wa miaka ile iliyopita, ama wale waliokuwa Wabunge basi sasa wasigombee tena ubunge, wawapishe watu wengine.
Hoja hii ya kijinga imeletwa hasa baada ya Mbunge wa zamani wa Mbeya Mjini kutangaza hadharani kwamba atapambana na Tulia Ackson popote atakapokimbilia na atamshinda.
Ufafanuzi wa Jambo hili ni huu hapa; CHADEMA kama chama cha siasa kinao utaratibu wa kisheria wa kupata wagombea wake kwa kupitia kura za maoni, anayeshinda ndiye anayegombea, unless otherwise.
Hii maana yake ni kwamba wanachama wa CHADEMA ndio wanaochagua mtu wa kugombea kwenye jimbo husika, baada ya kuridhika naye na kuwa na uhakika kwamba anakubalika hata kwa wananchi wengine wa jimbo husika.
Kwa mfano, kwenye Jimbo la Kyela kwa mwaka 2020, aliyeshinda kura za maoni aliitwa Alinanuswe Mwalwange, na huyu ndiye aliyekuwa Mgombea wa CHADEMA kwenye jimbo hilo.
Chama cha siasa kilicho makini kinaangalia Mgombea anayeweza kukivusha na kupata ushindi bila kujali amegombea mara ngapi, as long as ana afya njema ya mwili na akili, hoja kwamba huyu amegombea mara nyingi ni hoja ya kijinga.
Ndio maana baada ya Lowassa, Kikwete na Makamba kuwa Wabunge na kustaafu Majimbo yao wakawarithisha watoto wao, ndio maana Abood na Lubeleje walikuwa wagombea wa CCM kwenye majimbo yao kwa miaka nenda rudi.
CHADEMA itaendelea kusimika wagombea wanaokubalika kwenye kila Jimbo bila kujali makelele ya Mamluki.
Mungu ibariki CHADEMA.
Hoja hii ya kijinga imeletwa hasa baada ya Mbunge wa zamani wa Mbeya Mjini kutangaza hadharani kwamba atapambana na Tulia Ackson popote atakapokimbilia na atamshinda.
Ufafanuzi wa Jambo hili ni huu hapa; CHADEMA kama chama cha siasa kinao utaratibu wa kisheria wa kupata wagombea wake kwa kupitia kura za maoni, anayeshinda ndiye anayegombea, unless otherwise.
Hii maana yake ni kwamba wanachama wa CHADEMA ndio wanaochagua mtu wa kugombea kwenye jimbo husika, baada ya kuridhika naye na kuwa na uhakika kwamba anakubalika hata kwa wananchi wengine wa jimbo husika.
Kwa mfano, kwenye Jimbo la Kyela kwa mwaka 2020, aliyeshinda kura za maoni aliitwa Alinanuswe Mwalwange, na huyu ndiye aliyekuwa Mgombea wa CHADEMA kwenye jimbo hilo.
Chama cha siasa kilicho makini kinaangalia Mgombea anayeweza kukivusha na kupata ushindi bila kujali amegombea mara ngapi, as long as ana afya njema ya mwili na akili, hoja kwamba huyu amegombea mara nyingi ni hoja ya kijinga.
Ndio maana baada ya Lowassa, Kikwete na Makamba kuwa Wabunge na kustaafu Majimbo yao wakawarithisha watoto wao, ndio maana Abood na Lubeleje walikuwa wagombea wa CCM kwenye majimbo yao kwa miaka nenda rudi.
CHADEMA itaendelea kusimika wagombea wanaokubalika kwenye kila Jimbo bila kujali makelele ya Mamluki.
Mungu ibariki CHADEMA.