Wanaokwenda jela si wote wana hatia, hata wewe kesho unaweza kuwa mfungwa

NetMaster

JF-Expert Member
Sep 12, 2022
1,454
4,853
Hakuna anaejua siku yake ya kesho itakuwa vipi, lolote laweza kutokea uwe muhalifu ama sio mhalifu waweza kujikuta umeingia rasmi 18 za kwenda gerezani.

Wiki iliyopita nilienda mtembelea rafiki gerezani, yupo kwa takribani mwezi sasa kosa likiwa kununua simu kwenye magroup haya ya whatsapp, iliyoibiwa, simu aliyonunua kumbe ilikuwa ya wizi, kapewa kesi ya unyang'anyi kwa kutumia silaha, nilivyomkuta machozi yalinilenga. Ni mwezi kakaa lakini hali niliyomkuta nayo inasikitisha.

Mlo mmoja kwa siku tena ugal mkubwa ila mboga sasa unakuta majan yakunde yalokomaa maharage manne mchuzi pipa

Kuoga kwa folen

Kujisaidia kwa folen tena waziwazi kabsa wenzio wanakuona

Kulala sa kumi jioni,

Godoro kuu kuu zimeoza kwa jasho

Chumba kimoja wafungwa 50 mpk 60

Hakuna simu wala mawasliano ya aina yoyote

Kazi ni amri ni lazima kufanya

Ukiugua dawa za shida yan

Kwa upande wa mahabusu wanapoingizwa pale kwa mara ya kwanza huamini kuwa watatoka soon ila siku huwa wiki, wiki huwa mwezi, mwezi huwa miaka, wapo mahabusu kibao tangu 2020 kesi hazijasikilizwa

Epuka sana mambo ya madawa ya kulevya , wizi (ikiwemo kununua vya wizi), ujangili, kutembea na wanafunzi wa shule kike, n.k, hizi kesi ndio zina sotesha sana watu gerezani

Kama unadhani jela ni shule mpeleke mwanao, sio kuzuri hata kidogo
 
Hakuna anaejua siku yake ya kesho itakuwa vipi, lolote laweza kutokea uwe muhalifu ama sio mhalifu waweza kujikuta umeingia rasmi 18 za kwenda gerezani.

Wiki iliyopita nilienda mtembelea rafiki gerezani, yupo kwa takribani mwezi sasa kosa likiwa kununua simu iliyoibiwa kwenye magroup, kesi yake ni wizi na unyang'anyi kwa kutumia silaha, kapigwa mvua ya kutosha, nilivyomkuta machozi yalinilenga. Ni mwezi kakaa lakini hali niliyomkuta nayo inasikitisha.

Mlo mmoja kwa siku tena ugal mkubwa ila mboga sasa unakuta majan yakunde yalokomaa maharage manne mchuzi pipa

Kuoga kwa folen

Kujisaidia kwa folen tena waziwazi kabsa wenzio wanakuona

Kulala sa kumi jioni,

Godoro kuu kuu zimeoza kwa jasho

Chumba kimoja wafungwa 50 mpk 60

Hakuna simu wala mawasliano ya aina yoyote

Kazi ni amri ni lazima kufanya

Ukiugua dawa za shida yan

Kwa upande wa mahabusu wanapoingizwa pale kwa mara ya kwanza huamini kuwa watatoka soon ila siku huwa wiki, wiki huwa mwezi, mwezi huwa miaka, wapo mahabusu kibao tangu 2020 kesi hazijasikilizwa

Mtaani mtu anakuambia hakuna issue za pesa, anaona uvivu wa kulima hata bustani. Lakini akifika kule atalima Hadi maji ayaite bhaji

Kama unadhani jela ni shule mpeleke mwanao, sio kuzuri hata kidogo
Maisha ya duniani ni fumbo zito sana
 
Hivi mtu uzingatie mambo gani! Ili kuepukana na makosa yanayoweza kukupeleka jera?
Ni kumuomba mungu akuepushe maana jela kuingia ni kugusa Mim Kaka yangu alinusurika HV kuingia jela tena Kwa kesi ya kusingiziwa
 
Chakula wanacholima(ga) kinakwenda(ga) wapi? Au hakitoshi?

Na Sheria unataka wafungwa wale kwa tabu au ni uchumi wetu mdogo?
Wanasema(ga) ukienda(ga) jela unatakiwa ujutie
 
Nilijikuta kwenye 18 za polisi sababu nimeongea na simu karibu na kituo cha polisi wakaniweka lock up..kimasihala aisee. Nilitoka ndani ya dk 5
 
Jela ni shule ndio maana wapelekwao kule huja uraiyani wakiwa na maadili mema
Nani kakudanganya mkuu, kwamba wakitoka kule wanakuwa na maadili mema...?

Wengi wanatoka huko wakiwa hawapo sawa kiakili. Nadhani umesoma maelezo ya OP hapo juu. Maisha ya kule yanakuvuruga kuanzia nje mpaka ndani.
 
Hakuna anaejua siku yake ya kesho itakuwa vipi, lolote laweza kutokea uwe muhalifu ama sio mhalifu waweza kujikuta umeingia rasmi 18 za kwenda gerezani....
Wafungwa ni binadamu, nchi yetu inawakosea haki yao ya kimaisha. Katiba mpya inayojisimamia ni muhimu kuliko maelezo, kila MTz atafaidika nayo.
 
Back
Top Bottom