WANANCHI na WALANCHI

Exaud J. Makyao

JF-Expert Member
Nov 30, 2008
1,518
22
1. Urithi wetu umegeuziwa kwa wageni,
na ajira bora kwa wageni pia.
2. Katika nchi yetu wenyewe,
tumekuwa kama yatima wasio na baba,
mama zetu wamekuwa kama wajane.
3. Tumebaki kuitwa WANANCHI,
Lakini wapo WALANCHI.
4. Ni lazima kununua maji tunayohitaji,
Raslimali zetu zapatikana kwa kuzinunua.
5. Haki zetu, sasa zapatikana sokoni,
Wenye nacho ndiyo wamiliki wa haki zetu.
6. Wenye nacho hawashindwi kesi,
Katika zetu mahakama.
7. Wale ambao wanafuatilia maisha yetu,
wapo kwenye njia zetu,
Tumechoka na hakuna pumziko.
8. Tumejitolea kuwatumikia wageni,
ili tupate chakula chetu cha siku kwa siku.
9. Je, ni Baba zetu walitenda mabaya,
na sisi tunachukua adhabu yao?.
Au twateseka kwa makosa yetu wenyewe?
10. Wageni wanatutawala, vitega uchumi wajitwalia,
nani ajitolee kutuweka huru kutoka katika mateso?
 
1. Urithi wetu umegeuziwa kwa wageni,
na ajira bora kwa wageni pia.
2. Katika nchi yetu wenyewe,
tumekuwa kama yatima wasio na baba,
mama zetu wamekuwa kama wajane.
3. Tumebaki kuitwa WANANCHI,
Lakini wapo WALANCHI.
4. Ni lazima kununua maji tunayohitaji,
Raslimali zetu zapatikana kwa kuzinunua.
5. Haki zetu, sasa zapatikana sokoni,
Wenye nacho ndiyo wamiliki wa haki zetu.
6. Wenye nacho hawashindwi kesi,
Katika zetu mahakama.
7. Wale ambao wanafuatilia maisha yetu,
wapo kwenye njia zetu,
Tumechoka na hakuna pumziko.
8. Tumejitolea kuwatumikia wageni,
ili tupate chakula chetu cha siku kwa siku.
9. Je, ni Baba zetu walitenda mabaya,
na sisi tunachukua adhabu yao?.
Au twateseka kwa makosa yetu wenyewe?
10. Wageni wanatutawala, vitega uchumi wajitwalia,
nani ajitolee kutuweka huru kutoka katika mateso?

Exaud,
Haya ni mawazo ya Kifalsafa hasa.
Naamini wachambuzi wa mabo wataitafutia Desa muafaka.
Kwa mawazo yangu,
Hiyo hali ya kupoteza uhuru inazikumba nchi nyingi za Afrika.
Hakika tunahitaji dawa.
 
Exaud,
Haya ni mawazo ya Kifalsafa hasa.
Naamini wachambuzi wa mabo wataitafutia Desa muafaka.
Kwa mawazo yangu,
Hiyo hali ya kupoteza uhuru inazikumba nchi nyingi za Afrika.
Hakika tunahitaji dawa.

Leta dawa bibie.
 
Exaud,
Haya ni mawazo ya Kifalsafa hasa.
Naamini wachambuzi wa mambo wataitafutia Desa muafaka.
Kwa mawazo yangu,
Hiyo hali ya kupoteza uhuru inazikumba nchi nyingi za Afrika.
Hakika tunahitaji dawa.

Utaifa wetu, lazima udhihirike katika vitendo na hisia zetu kuliko maneno matupu.
 
Mkuu, tujiandikishe kupiga kura, na tupige kweli. Haya, na tukutane kwenye sanduku la kura!

KYACHAKICHE,
Kuna majina mengine hutoweka kiaina kwenye daftari la wapiga kura siku ya kupiga kura mkuu.Waweza kujiandikisha na usipige kura.
Umelisahau hilo?
 
KYACHAKICHE,
Kuna majina mengine hutoweka kiaina kwenye daftari la wapiga kura siku ya kupiga kura mkuu.Waweza kujiandikisha na usipige kura.
Umelisahau hilo?
Ni kweli mkuu, hapo nako ni pakufanyia kazi. Nakumbuka mwaka 2000 bwana Mapesa alidai katika kituo chake chakupigia kura alipata alipata kura 1 tu ( ya kwake) huku familia yake yote akiwemo mke wake wakidaiwa kupigia kura kituo hicho hicho, haijulikani kama na wao walimnyima kura.
 
Ni kweli mkuu, hapo nako ni pakufanyia kazi. Nakumbuka mwaka 2000 bwana Mapesa alidai katika kituo chake chakupigia kura alipata alipata kura 1 tu ( ya kwake) huku familia yake yote akiwemo mke wake wakidaiwa kupigia kura kituo hicho hicho, haijulikani kama na wao walimnyima kura.

Ni kama kichekesho.
Maajabu ya mussa haya.
 
Wakuu heshima mbele
Moja ya swali rahisi kuuliza ni "ufanyike mpango gani kulinusuru taifa?" HIli swali kwa kawaida linawapa nafasi kubwa sana mafisadi kujipanga na kuendelea kufanya ufisadi kisheria.
MAFISADI wanawapa majibu marahisi sana wazalendo ili wasijishughulishe hata kidogo kuweka madarakani serikali inayowajibika na yenye kuthubutu kuwazibia mianya ya unyonyaji mafisadi.

Lakini swali likiwa "NIFANYE NINI MIMI MWENYEWE KUOKOA NCHI YANGU NA WATU WAKE?" Hapa kunakuwa na mtenganisho wa mashujaa wachache sana waliojitoa muhanga kuhakikisha kuwa serikali makini inaingia madarakani.

SHIME watanzania kila mmoja wetu ajipe wajibu wa kuhakikisha kuwa anaonyesha msimamo wake kila siku dhidi ya mafisadi na chama chao na pia anajipa wajibu na kuingia gharama yoyote kuhakikisha kuwa mission ya kuondoa serikali mbovu madarakani inafanikiwa.

HUO NDIYO MWANZO WA MWISHO WA KULALAMIKIA LAANA YETU.
 
,,,,,,,,,,,,,,,,,,,

Moja ya swali rahisi kuuliza ni "ufanyike mpango gani kulinusuru taifa?"

Lakini swali likiwa "NIFANYE NINI MIMI MWENYEWE KUOKOA NCHI YANGU NA WATU WAKE?"

HUO NDIYO MWANZO WA MWISHO WA KULALAMIKIA LAANA YETU.

KAMENDE,
Tuko pamoja.
Tunahitaji watu walioko tayari kuwa sehemu ya mabadiliko tunayo yataka.
 
Back
Top Bottom