YHK geneous
Senior Member
- Jun 24, 2017
- 188
- 120
Uzi huu ni maalum kwa ajili wa waandishi na wapenzi wa kusoma mashari kuja hapa kujadiliana na kufundishana vitu mbalimbali kuhusu ushairi.
Karibuni jamani tushirikishane na tutunge mashairi mbalimbali bila kusahau swala la kupeana fursa mbalimbali za kiuandishi wa mashairi au nyimbo sehemu mbalimbali.
Karibuni tujifunze pamoja...
Natanguliza utunzi wangu hapa chini
NAREJEA KIAMBONI
Wakati umeshafika, Nirejee kiamboni.
Nimemaliza pirika, Nahitaji ahueni.
Majira yashakatika, ninafuraha moyoni.
Chengoni ni kiamboni, nami nimepakumbuka.
Gange zilinigubika, zikanitoa nyumbani.
Majukumu nikashika, Nikaondoka nchini.
Sasa leo imefika, Narudi mastakimuni.
Chengoni ni kiamboni, Nami nimepakumbuka.
Mtima umeridhika, bashasha tele moyoni.
Aila kuikumbuka, lakini hauioni.
Hilo nilishalichoka, ni huzuni fuadini.
Chengoni ni kiamboni, Nami nimepakumbuka.
Wengi niliwakumbuka, Wazazi ndugu jirani.
Na watoto kadhalika, marafiki kwa utani.
Ni vingi vya kukumbuka, usipokuwa nyumbani.
Chengoni ni kiamboni, Nami nimepakumbuka.
Naona nimeshafika, Acha niingie ndani.
Kwa safari nimechoka, naomba nikae chini.
Sasa nukta ninaweka, Nawaaga kwaherini.
Chengoni ni kiamboni, aghalabu kupachoka.
Karibuni jamani tushirikishane na tutunge mashairi mbalimbali bila kusahau swala la kupeana fursa mbalimbali za kiuandishi wa mashairi au nyimbo sehemu mbalimbali.
Karibuni tujifunze pamoja...
Natanguliza utunzi wangu hapa chini
NAREJEA KIAMBONI
Wakati umeshafika, Nirejee kiamboni.
Nimemaliza pirika, Nahitaji ahueni.
Majira yashakatika, ninafuraha moyoni.
Chengoni ni kiamboni, nami nimepakumbuka.
Gange zilinigubika, zikanitoa nyumbani.
Majukumu nikashika, Nikaondoka nchini.
Sasa leo imefika, Narudi mastakimuni.
Chengoni ni kiamboni, Nami nimepakumbuka.
Mtima umeridhika, bashasha tele moyoni.
Aila kuikumbuka, lakini hauioni.
Hilo nilishalichoka, ni huzuni fuadini.
Chengoni ni kiamboni, Nami nimepakumbuka.
Wengi niliwakumbuka, Wazazi ndugu jirani.
Na watoto kadhalika, marafiki kwa utani.
Ni vingi vya kukumbuka, usipokuwa nyumbani.
Chengoni ni kiamboni, Nami nimepakumbuka.
Naona nimeshafika, Acha niingie ndani.
Kwa safari nimechoka, naomba nikae chini.
Sasa nukta ninaweka, Nawaaga kwaherini.
Chengoni ni kiamboni, aghalabu kupachoka.