Nikiwa kama mpenzi wa burudani , hasa muziki wa dansi nimejisikia vibaya baaada ya kumuona huyu mzee leo chanel Ten, akiomba msaada wa watanzania kumchangia chochote kwa tamasha ambalo litafanyika dar es salaam.Amediriki kusema katika miaka yote ya kimuziki hajafanikiwa kumiliki hata baiskeli,. Kwa hali hii naamini kabisa ndo maana wengi wa wasanii hujiingiza katika biashara haramu ili waendane na majina yao.