Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,890
- 6,896
Vyombo vya habari ni jicho la jamii niliandika katika moja ya blog mojawapo mashuhuri napa nchini siku chache zilizopita. Leo walionikandia kuhusu ushauri wangu kwa vyombo vya habari wanashuhudia Wanahabari wa Ikulu yetu tukufu na mahali pa heshima wanapotoa habari yenye maneno ya misemo ya vibaka mitaani kwa lugha za matusi, dharau na uchochezi ikiwa ni taarifa rasmi ya Ikulu, ni aibu tupu kwa nchi yetu. Pamoja na kusomea na kupata ujuzi wa mawasiliano ya habari na kubobea katika kusomea elimu ya rhytorics unashangaa mtu kama huyo leo anatoa hadharani lugha iliyo chini ya kiwango hata mtu asiye na taaluma ya uandishi anabaki kushangaa usanii wa vyombo vya habari vya Ikulu yetu.
Nilisema vyombo vya habari Tanzania tunahitaji kupiga hatua moja mbele zaidi kwa kutumia taaluma yetu, leo alichoongea mwakilishi wa Rweyemamu na wakati Rweyemanu ametilia sahihi nakala hiyo kama mkuu wa mawasiliano Ikulu kujibu kauli ya Dr. Slaa kuhusiana na Richmond na Dowens ni nje ya kiwango kabisa kwa watu wanaojua na wenye taaluma ya uanahabari (lack all depth). Na huwezi amini kama huyu amewahi kuwa mhariri wa gazeti nchini.
Wengi wa watumishi wa serikali hufanya kazi na wajibu zao zaidi kwa dalili ya kulinda maslahi binafsi kwa wakubwa wao hali inayojenga udhaifu wa kutokuwa na hali ya kujenga hoja za kujiamini ila kuwapamba wakubwa kwa mazuri tu ingawa ndani ya mioyo yao wanajua madhaifu yao.
Kauli alizosema Mheshimiwa Rais Kikwete za kiungwana na kiustaarabu na kuheshimiana katika salamu za mwaka mpya ziko wapo wakati wanahabari wa Ikulu yake kabla hatujameza mate wameanza na kashfa za lugha chafu chafu za dharau, matusi, kejeli na uchochezi?
Jungu kuu halikosi ukoko
Nilisema vyombo vya habari Tanzania tunahitaji kupiga hatua moja mbele zaidi kwa kutumia taaluma yetu, leo alichoongea mwakilishi wa Rweyemamu na wakati Rweyemanu ametilia sahihi nakala hiyo kama mkuu wa mawasiliano Ikulu kujibu kauli ya Dr. Slaa kuhusiana na Richmond na Dowens ni nje ya kiwango kabisa kwa watu wanaojua na wenye taaluma ya uanahabari (lack all depth). Na huwezi amini kama huyu amewahi kuwa mhariri wa gazeti nchini.
Wengi wa watumishi wa serikali hufanya kazi na wajibu zao zaidi kwa dalili ya kulinda maslahi binafsi kwa wakubwa wao hali inayojenga udhaifu wa kutokuwa na hali ya kujenga hoja za kujiamini ila kuwapamba wakubwa kwa mazuri tu ingawa ndani ya mioyo yao wanajua madhaifu yao.
Kauli alizosema Mheshimiwa Rais Kikwete za kiungwana na kiustaarabu na kuheshimiana katika salamu za mwaka mpya ziko wapo wakati wanahabari wa Ikulu yake kabla hatujameza mate wameanza na kashfa za lugha chafu chafu za dharau, matusi, kejeli na uchochezi?
Jungu kuu halikosi ukoko