DOKEZO Wanafunzi Wilaya ya Mbozi (Songwe) wanalimishwa kwenye mashamba binafsi ya Walimu

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
A

Anonymous

Guest
Kuna jambo ambalo nimekutana nalo nikiwa likizo huku Mkoa wa Songwe, Wilaya ya Mbozi, kuna baadhi ya Shule za Msingi, Walimu wanamiliki mashamba na kuwafanyisha kazi Wanafunzi.

Nimezungumza na baadhi ya Watoto wanasema ikifika Januari msimu wa kilimo shule wanatega na kwenda siku ambazo hakuna ratiba ya kuwapeleka shamba.

Kama ni mafunzo ya vitendo basi ingekuwa inafanyika shuleni au kwenye mashamba ya Shule lakini kibaya zaidi ni kuwa wanalazimika kwenda kulifuata shamba la Mwalimu au Walimu umbali wa Kilometa 2 ikiemo kuvuka mito.

Ujumbe huu uwafikie Wizara ya Elimu wajue hiki kinachoendelea kuhusu watumishi wao.
 
Tulilima Sana ,tulibeba Sana kuni za mradi ,tulibeba matofali,mazao mashambani ,mbolea ,maji nk Wala hatukuona hela na wala hatukulalamika kwa sababu tuliwaheshimu na kuwapenda walimu wetu,tulijua kabisa wanatumia muda wao mwingi Sana kutupambania bila sisi kuwalipia,tuliwasaidia na wao walitusaidia.kubwa zaidi tulitoka na ujuzi ambao mpaka leo tunautumia kwny maisha yetu.
 
Nimeshuhudia shule nyingi tu hasa zile za kando na mjini na vijijini wakilima mashamba ya walimu.
 
Mzee baba hilo hata hulifanyeje haliwezi kuzuilika kwasababu mwalimu hayo ndio marupurupu yake na inavyoonekana wewe una roho mbaya tu kwa walimu.
Au kwa kuwa ulienda kijijini umetaka kuonekana wewe ndio mjanja na labda umewaahidi wazazi utawapazia sauti. Walimu wanaishi maisha magumu mno kama watoto wanasaidia muda wa ziada na haiathiri ratiba ya masomo shida iko wapi?
Kipindi nasoma enzi hizo sio tu kulimishwa mashamba ya walimu lakini pia tulikuwa tunajitolea siku za wikiend kwenda kusaidia walimu wetu kulima.
Walimu wa zamani ndio waliufaidi ualimu japo mshahara ulikuwa mdogo em fikiria wakati wa mavuno tutawapelekea mahindi ya kuchoma,mapapai matunda yote bado mayai lakini kubwa zaidi ni pale ambapo mwalimu atakuja kwenu lazima ukahadithie shuleni.
Ila wazazi wa sasa hivi ukiweko na wewe mmejaa roho mbaya na chuki dhidi ya walimu.
 
Kuna jambo ambalo nimekutana nalo nikiwa likizo huku Mkoa wa Songwe, Wilaya ya Mbozi, kuna baadhi ya Shule za Msingi, Walimu wanamiliki mashamba na kuwafanyisha kazi Wanafunzi.

Nimezungumza na baadhi ya Watoto wanasema ikifika Januari msimu wa kilimo shule wanatega na kwenda siku ambazo hakuna ratiba ya kuwapeleka shamba.

Kama ni mafunzo ya vitendo basi ingekuwa inafanyika shuleni au kwenye mashamba ya Shule lakini kibaya zaidi ni kuwa wanalazimika kwenda kulifuata shamba la Mwalimu au Walimu umbali wa Kilometa 2 ikiemo kuvuka mito.

Ujumbe huu uwafikie Wizara ya Elimu wajue hiki kinachoendelea kuhusu watumishi wao.
Wewe utakuwa wa mwaka Afumbili
 
Ngoja vijana wapate experience huko , wasikae lege lege.
Kwa watoto wa Kijijini hiyo siyo kazi kubwa kama unavyoiona mtoto wa mjini ni sehemu tu ya shughuli zao !

Mleta uzi hujasema wanalimishwa muda gani ? Pia huenda ni mafunzo kwa vitendo kweli maana sio kila kitu kiko shuleni huenda mwalimu ndo ana bustani ya shamba darasa nyumbani kwake (ya mfano) , huenda mwalimu ndo anazo zana za kufanyia kilimo mfano pampu za kumwagilia, za kupulizia dawa na madawa mbali mbali huenda shule haina mashamba au kama yapo basi hayajafanyiwa chochote kutokana na shule zetu kuwa na hali mbaya mafungu hayafiki huku chini.

Hiyo shule hakuna kamati ya shule na umoja wa wazazi ?
 
Walimu wanalipwa mshahara wawalipe vibarua wawafanyie kazi. Ingekuwa hayo mashamba ni miradi ya shule hapo sawa.
Kuwalimisha wanafunzi huo muda uko wapi kwenye kalenda ya wizara?

Hao wanafunzi sio kwamba wanajifunza kazi maana mazingira yao ni ya vijijini,hii ina tafsiri kuwa tayari kazi za shamba wanazielewa huko makwao. Walimu hapa wanajinufaisha bila sababu ya msingi.

Vipi wanafunzi wakichafuka na kuchafua mavazi yao Nan anawajibika kununua sabuni za kufulia kila siku?
Kwahiyo wasipoenda kulima huko wewe utakuwa umepata Nini? Acha roho mbaya ya wivu wa kike wewe
 
Wewe mtoto wa Afumbili acha kelele
Walimu wanalipwa mshahara wawalipe vibarua wawafanyie kazi. Ingekuwa hayo mashamba ni miradi ya shule hapo sawa.
Kuwalimisha wanafunzi huo muda uko wapi kwenye kalenda ya wizara?

Hao wanafunzi sio kwamba wanajifunza kazi maana mazingira yao ni ya vijijini,hii ina tafsiri kuwa tayari kazi za shamba wanazielewa huko makwao. Walimu hapa wanajinufaisha bila sababu ya msingi.

Vipi wanafunzi wakichafuka na kuchafua mavazi yao Nan anawajibika kununua sabuni za kufulia kila siku?
 
Peleka ujinga wako huko mzee. Tena wanapaswa kulima haswaaaa ili wajifunze stadi za maisha kwani 90% ya maisha ya mwanafunzi yapo mkononi mwa walimu. Hao ni kama wazazi wake baba na mama.
 
Inasikitisha sana mtoto kaenda kusoma mwalimu anamkatia mraba alime paka achoke daa Hawa walimu wanazingua sana
 
Back
Top Bottom