mlimbwa1977
Member
- Feb 7, 2011
- 24
- 0
Imebainika kuwa wanafunzi wengi katka vyuo vyetu nchini wanajihusisha na ghiliba/ujanjaujanja wakati wa mitihani mbalimbali au kazi wanazopewa na walimu wao,wapo wasiojihusisha kabisa na kazi zinazotolewa(assignments) lakini mwisho wa siku mtu anafaulu kwa kupata alama a,ndani ya vyumba vya mitihani ni aibu watu wanatengeneza kitu kinaitwa 'network' ili wapeane majibu kwa kila swali lililopo kwenye mtihani (hawana muda wa kuchemsha akili zao,mambo kwa shortcut).
Hiyo ni mipango mkakati inayomwezesha mtu kupata/kufikia malengo aliyoyakusudia(starategic objectives) lakini je hii ni njia sahihi itakayoliwezesha taifa letu kupata/kuwa na wataalamu weledi/waliobobea kuweza kulivusha taifa hili katika matatizo lukuki yanayoelekea kutushinda?
wapenda maendeleo,nini kifanyike kutokomeza hali hii kwa ustawi wa taifa letu?
Hiyo ni mipango mkakati inayomwezesha mtu kupata/kufikia malengo aliyoyakusudia(starategic objectives) lakini je hii ni njia sahihi itakayoliwezesha taifa letu kupata/kuwa na wataalamu weledi/waliobobea kuweza kulivusha taifa hili katika matatizo lukuki yanayoelekea kutushinda?
wapenda maendeleo,nini kifanyike kutokomeza hali hii kwa ustawi wa taifa letu?