Wanafunzi wa shule za upili wa Taasisi ya Confucious UDSM Tanzania watembelea kijiji cha kale cha Siping na jumba la maonyesho la mji wa Jinhua

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,010
1,034

Tarehe 22, Juni, wanafunzi wa shule za upili wa Taasisi ya Confucious katika chuo kikuu cha Dar es Salaam Tanzania (UDSM) wametembelea kijiji cha kale cha Siping na jumba la maonyesho la mji wa Jinhua.

Kijiji cha Siping kilichoko katika mlima Jiufeng mjini Jinhua, kilijengwa mwanzoni mwa enzi ya Ming, ambacho ukubwa wake ni mita za mraba 6,000. Ukuta wa majengo kijijini umechongwa picha mbalimbali za ndege, wanyama, maua na kadhalika, ambao una thamani kubwa ya kihistoria na kiutamaduni. Kijiji hicho kimewekwa kwenye orodha ya vijiji maarufu vyenye historia na utamaduni vya China mwaka 2010.

Wanafunzi hao walitembea katika kijiji hicho, kujionea mandhari nzuri ya kijiji na kuzungumza na wanakijiji.

1687936165441.png


Wanafunzi na walimu wanapiga picha kwa pamoja nje ya lango la kijiji cha Siping

1687936184710.png


Wanafunzi wanatazama samaki wa rangi aina ya “Koi Fish”.

1687936201652.png
1687936218036.png


Wanafunzi wanatembea kwenye vichochoro kijijini Siping

1687936227387.png
1687936236113.png


Wanafunzi wanapiga picha pamoja na wanakijiji

1687936252349.png
1687936258571.png


Wanafunzi wanatazama vinyago vya kichina

1687936275293.png

Wanafunzi wanajifunza chesi ya Go

1687936293286.png


Wanafunzi wanajaribu mchezo wa Touhu

1687936311255.png


Wanafunzi wanatazama kisima

1687936329284.png


1687936339193.png


Wanafunzi wakikaa ndani ya shule ya Chongde​

Siku hiyo mchana, wanafunzi hao walikwenda jumba la maonyesho la mji wa Jinhua. Jumba hilo linaonyesha historia ya maendeleo ya mji wa Jinhua na mpango wa maendeleo ya mji huo kwa kutumia teknolojia ya VR, modeli ya kidijitali, 3D na teknolojia nyingine za kisasa. Wanafunzi hao walishangaa kuona kasi ya maendeleo ya mji wa Jinhua.
 
Back
Top Bottom