Nicholaus Kilunga
JF-Expert Member
- Feb 15, 2014
- 1,188
- 567
Wanafunzi wa chuo kikuu cha mtakatifu Augustino tawi kuu la Mwanza wameipa ruhusa CHADEMA ya kuongoza nchi,akizungumza na mwandishi wa habari hii mmoja wa wanafunzi chuoni hapo,Valeliani Baleke ,amesema kwa muda mrefu sana CDM kimeonekana kuwa chama sahihi kwa watanzania,chama ambacho kimejipambanua kama chama kinachotetea na kusimamia maslahi ya wanyonge,akitolea mifano ya namna CDM ilivyoibana serikali kwenye issue za EPA,Buzwagi,Meremeta,Escrow na katiba mpya,"huko kote CDM ilisimama kidete kwa ajiri ya maslahi ya wananchi".
Nae bwana Damas Kimenyi ambaye pia anasomea masuala ya sheria pia akiwa ni katibu wa CDM wilaya ya Ilemela,alisema wao kama wasomi wanaiunga mkono CDM sio kwa sababu ya maslahi,bali ni kwa sababu ndicho chama kinachoweza kuitoa nchi korongoni ilipopelekwa na serikali ya CCM,wanafunzi wengi wa chuo hicho walioongea na mwandishi wa habari hii walionekana kukikubali zaidi chama hicho cha upinzani nchini,huku wengi wakionekana kumtaka katibu mkuu wa chama hicho Dr Willbroad Slaa agombee urais kwa tiketi ya chama hicho baadae aungwe mkono na vyama vinayounda UKAWA,wakisema ndani ya CCM hakuwezi kupatikana kiongozi bora kutokana na chama hicho kukithiri kwa ufisadi na kushondwa kusimamia masuala ya msingi ya nchi hii.
Wanafunzi hao walitoa maoni hayo baada ya mwandishi kuwataka wazungumzie ujio wa viongozi wa kutaifa wa chama hicho chuoni hapo,ambapo leo naibu katibu mkuu Zanzibar Salum Mwalim atatikisa katika viwanja vya shule ya msingi Nyamalango,naibu katibu huyo ataambatana na mwenyekiti wa BAVICHA taifa Patrobas Katambi,mwenyekiti wa BAWACHA taifa Halima Mdee,wabunge Wenje wa Nyamagana,Kiwia wa Ilemela,Machemli na Profesa Jay mwanamziki na mtia nia wa ubunge Mikumi kuanzia majira ya saa 9 mchana katika sherehe ya kuwaaga wahitimu wa chuo hicho ambao pia walikuwa ni wanaCHADEMA(CHASO SAUT)
Nae bwana Damas Kimenyi ambaye pia anasomea masuala ya sheria pia akiwa ni katibu wa CDM wilaya ya Ilemela,alisema wao kama wasomi wanaiunga mkono CDM sio kwa sababu ya maslahi,bali ni kwa sababu ndicho chama kinachoweza kuitoa nchi korongoni ilipopelekwa na serikali ya CCM,wanafunzi wengi wa chuo hicho walioongea na mwandishi wa habari hii walionekana kukikubali zaidi chama hicho cha upinzani nchini,huku wengi wakionekana kumtaka katibu mkuu wa chama hicho Dr Willbroad Slaa agombee urais kwa tiketi ya chama hicho baadae aungwe mkono na vyama vinayounda UKAWA,wakisema ndani ya CCM hakuwezi kupatikana kiongozi bora kutokana na chama hicho kukithiri kwa ufisadi na kushondwa kusimamia masuala ya msingi ya nchi hii.
Wanafunzi hao walitoa maoni hayo baada ya mwandishi kuwataka wazungumzie ujio wa viongozi wa kutaifa wa chama hicho chuoni hapo,ambapo leo naibu katibu mkuu Zanzibar Salum Mwalim atatikisa katika viwanja vya shule ya msingi Nyamalango,naibu katibu huyo ataambatana na mwenyekiti wa BAVICHA taifa Patrobas Katambi,mwenyekiti wa BAWACHA taifa Halima Mdee,wabunge Wenje wa Nyamagana,Kiwia wa Ilemela,Machemli na Profesa Jay mwanamziki na mtia nia wa ubunge Mikumi kuanzia majira ya saa 9 mchana katika sherehe ya kuwaaga wahitimu wa chuo hicho ambao pia walikuwa ni wanaCHADEMA(CHASO SAUT)