Wanafunzi MAKUMIRA waambiwe ukweli

walifunga barabara ili wananchi waelewe na wafahamu kilio chao, na hakuna hata abiria mmoja aliyekasirika na kitendo hicho cha wanafunzi, mimi nawaunga mkono kabisa kabisa, maana bila mgomo hakuna haki nchi hii..


Manyanza,

Unaposema hakuna abiria aliyekasirika unakuwa unakosea heshima uvumilivu na uungw'ana wa watumiaj wa barabara. mimi mwenyewe nilikuwa miongoni mwa watu waliojitahidi kuwazuia vijana watano walioshuka kwenye toyota pickup moja wakitaka kuwa confront wanafunzi hao kabla polisi hawajafika. Watumiaji wa barabara walikasirishwa sana na tumenusirika kuwa na vurugu pale.
Utashi wako wa kisiasa isiwe sababu ya kutetea maovu yote yanayofanywa na unaowashabikia.
Na kufunga barabara ili mtu mwenye safari yake aelewe kilio chao, wao wanajua hao wasafiri wana kilio gani? Je kama kuna mjamzito anawaishwa hospitali? na yeye asikilize kwanza kilio cha mikopo ya wanafunzi kabla ya kujifungua?
Manyanza, kuwa makini na maoni unayotoa. Mtawapoteza vijana hawa. Tuungane kuwaambia kuwa waekosea, ili siku nyingine wawe makini zaidi.
 
Kama kawaida ya viongozi wa CHADEMA Mh. Freeman Mbowe alitoa hotuba ya kuwachochea wanafunzi kufanya vurugu ili nchi isitawalike. Hii ndio agenda mpya ya CHADEMA.
Vinara wa ufunguzi wa tawi hilo la CHADEMA ndio walikuwa vinara wa kuongoza mgomo huo wa wanafunzi.
Hata hivyo, narudia tena kuwa swala la u-CHADEMA siyo la msingi. Wangeshawishiwa kama walivyoshawishiwa na Mbowe na Lema halafu wakagoma bila kuingilia uhuru wa wasiohusika na mgogoro huo, kama wenzao wa Iringa, sote tungewaunga mkono.

Naomba utuletee hiyo hotuba ya uchochezi aliyoitoa ili nayo tuijadili, maana isije ikawa unaongea vitu ambavyo havina ushahidi wa aina yoyote ile.
 
ZeMarcopolo
Najua CDM inawanyima usingizi kwani hata UDOM mlisema CDM imeshinikiza.
ulitaka waandamane kwenda wapi bodi ya mikopo (sijui kama wana ofisi hapa Arusha), je unauhakika gani kama wasingeambiwa wanataka kuteka sehemu husika....
tangu 11/2010 wako chuo hawajapewa mikopo yao lakini limekuja swala la DOWANS haraka haraka wanataka kulipwa, wakati wao wanachindia maembe na mikate hapo kuna mtu ataonyesha ustaarabu wake au CCM mnataka ustaarabu upi watanzania wauonyeshe?
hebu onyesheni ustaarabu wa kuwajibika kwanza harafu ndiyo mhoji na ustaarabu wa mnao watawala ingawa ni kwa mabavu...


Ndio maana Jenerali Ulimwengu alisema (and I support) kuwa ni LAZIMA tuwe na National ethos kabla hatujaanza kuandika katiba mpya. Maana yake ni kwamba kama taifa tuweze kuona jambo na kusema hili si sahihi na tukasimama kulipinga. Nakubaliana na wewe kuwa watawala wanawajibika kuwapa wananchi haki zao, ikiwa ni pamoja na wanafunzi hawa kupata mkopo kwa wakati. Hata hivyo, unadhihirisha kuwa hatuna National ethos iwapo unaweza kuja kwenye public discussion na kujustify mdai haki kuingilia haki ya mwingine! tena bila kuona aibu!!! shame on you!
 
Naomba utuletee hiyo hotuba ya uchochezi aliyoitoa ili nayo tuijadili, maana isije ikawa unaongea vitu ambavyo havina ushahidi wa aina yoyote ile.

Msindima,
ushahidi gani unahitaji ili kujua kuwa wanafunzi waliziba barabara? Jambo limekwamisha shughuli za wengi na wakazi wote wa Arusha wanajua. Kuhusu hotuba ya Mbowe ninayo in audio form. Nikirudi ofisini nitaiweka hapa muisikilize.
 
Msindima,
ushahidi gani unahitaji ili kujua kuwa wanafunzi waliziba barabara? Jambo limekwamisha shughuli za wengi na wakazi wote wa Arusha wanajua. Kuhusu hotuba ya Mbowe ninayo in audio form. Nikirudi ofisini nitaiweka hapa muisikilize.

Duh! afadhali katiba ibadilishwe, maana hii ya sasa kama ataingia wa type hizi za akina FM, itakua balaa!!!
 
Ndio maana Jenerali Ulimwengu alisema (and I support) kuwa ni LAZIMA tuwe na National ethos kabla hatujaanza kuandika katiba mpya. Maana yake ni kwamba kama taifa tuweze kuona jambo na kusema hili si sahihi na tukasimama kulipinga. Nakubaliana na wewe kuwa watawala wanawajibika kuwapa wananchi haki zao, ikiwa ni pamoja na wanafunzi hawa kupata mkopo kwa wakati. Hata hivyo, unadhihirisha kuwa hatuna National ethos iwapo unaweza kuja kwenye public discussion na kujustify mdai haki kuingilia haki ya mwingine! tena bila kuona aibu!!! shame on you!

Mkuu ZeMarcopolo kwa kiasi kikubwa umeelezea kero yako kwa hoja nzuri kabisa. Ni kweli kuwa si vyema kwa vijana wale kupeleka kashkash lao barabarani. Isipokuwa kubali pia kwamba umeingiza jazba ya kisiasa kidogo kwa kuhusisha (angalau kwa kudokeza tu) mgomo huo na CDM. Aidha, Nakubaliana nawe kuhusu umuhimu wa ustaarabu na National ethos katika kutengeneza mustakabali wa taifa (suala la katiba). Lakini uelewe pia kwamba ustaarabu una misingi yake. Ukimtibua mtu muungwana kwa kiasi kikubwa ujue hakuna gerentii kama utapata jibu la kistaarabu.

Makaburu wa Afrika ya Kusini baada ya kupuuzia madai ya usawa yaliyokuwa yakitolewa kwa amani na waasisi wa ANC (wakiongozwa na Chief Albert Luthuli), walionywa kuwa "msipokubali kuzungumza na mtu wa amani basi mjiandae kujadiliana na mtu mwenye upanga". Walipuuza busara hiyo; na hiyo ilikuwa kabla ya akina Mandela na Umkhonto we Sizwe. Pamoja na kwamba siungi mkono vurugu, sishangai watu wakivuka mipaka ya ustaarabu baada ya haki zao kukosa majibu ya uhakika.

Majuzi niliwasikia wanafunzi wa chuo kimoja (sijui UDOM?) wakishangaa: mbona kila tunapogoma ndipo mikopo inapatikana? Hili ni somo jingine kwa watawala: mkiwaburuza sana wananchi msitegemee majibu ya ustaarabu. Kama kweli CDM wanahusika basi ujue wao sio kichocheo; wanatumia fursa tu kama mwanasiasa yeyote makini anayejua mikakati ya ushindani wa kisiasa!
 
Drifter,

Umeeleza vizuri sana hapo juu na nimebidi nikupe THANKS.

ZeMarcopolo alikuwa na habari nzuri sana na jambo zuri tu kujadili ila kaharibu kuingiza mambo ya Chadema na Mbowe. Mwisho anaanza kuruka kuwa hayo si muhimu. Kama si muhimu, kwa nini uliyaweka? Ulifikiri unaongea na wajomba zako kijijini ambao hawajaenda shule na watakukubalia kila kitu? Mungu bariki JF bado wamejaa watu wenye akili zao nzuri tu na kumbukumbu safi kabisa.

Migomo si mizuri ila utakuwa unafanya makosa kuwalaumu Wagomaji, Waandamanaji, Wakosoaji nk bila kutafuta mzizi wa fitina umeanzia wapi. Tanzania ya leo, haki yako lazima upiganie. La muhimu ni kuwa UJUMBE WA VIJANA UMEFIKA.
 
Ndugu unafahamu hoja uliyotoa na response yake kutoka kwa watu wanaojua ukweli? mbona mimi nipo hapa makumira na huo mkutano unaosema sikusikia huo ujinga wako?? Mbowe alizungumzia umuhimu wa wanazuoni kuwa na sauti na mchango ktk kutetea wananchi wenzao hasa wa tabaka la chini kabisa???
kuna uhusiano gani kati ya kufunguliwa kwa tawi la cdm makumira na maandamano yaliyofanywa na wanafunzi wa mwaka wa 1 tena wachache kati ya wengi???????
huyo mbowe unayesema ndiye aliyewatuma vyuo vikuu huria kuandamana mpk bodi ya mikopo jana????au nao aliwafungulia tawi la cdm????
kuwa na akili za kufikiria kwa undani tena kama mtu mzima mwenye akili timamu, acha kuwa kama babu makambale nakutuletea ushabiki wa kijinga usio na maslai kwa nchi wala watu wake

jaribu kuwa mchunguzi wa mambo kabla ya kuropoka,nyie ndio walewale wa chama cha wakandamizaji mnaopindisha ukweli hata ktk ukweli
 
Mkuu nakuunga mkono kwamba wasingefunga barabara. Lakini napingana na wewe kwamba wanatumiwa kwa maslahi ya kisiasa. Kwani Chadema ndio waliochelewesha mikopo ya wanafunzi? Na kama unajua kwamba ukichelewesha mikopo ya wanafunzi watagoma kwa nini ucheleweshe? Kwa nini kulipa Dowans haina mjadala na inafanyiwa fast tracking lakini madai ya wanafunzi hayashuhulikiwi?
 
Sio wa kwanza na kitendo cha vinara hao wa CHADEMA kuongoza mgomo si tatizo. Tatizo ni kuziba barabara, jambo ambalo linaingilia uhuru wa wasiohusika na mgogoro huo.
Ni jukumu letu kuwafundisha wanafunzi hawa na wafuasi wote wa CHADEMA kwa ujumla kuwa katika kutaka haki zao ziheshimiwe ni wajibu wao kuheshimu haki za wengine. Hiyo ndio essence ya hii thread.

kima wewe UKITAKA HAKI, TENDA HAKI!!! Full stop! haya kakojoe ukalale!!!
 
Back
Top Bottom