MAOFISA wa usalama wa taifa na polisi wanawahoji wanafunzi wanane wanaosoma shule moja ya sekondari kuhusu jaribio la kuulipua ubalozi wa Marekani nchini Tanzania.
Wanafunzi hao wa shule ya Biafra wilayani Kinondoni, Dar es Salaam, walikamatwa jana saa tisa alasiri.
Mtuhumiwa mkuu wa mpango huo wa kuulipua ubalozi wa Marekani, Nassib Zukheri alikamatwa Jumapili saa tatu usiku wakati akifungua koki ya tanki la mafuta katika ubalozi huo.
Nassib ni mwanafunzi wa kidato cha pili katika shule ya Biafra, yupo polisi anahojiwa.
Inadaiwa kuwa mtoto huyo anayekadiriwa kuwa na umri wa kati ya miaka 15 hadi 17 aliingia katika ubalozi huo kwa kupitia geti namba tatu.
Mkuu wa polisi kandaa maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova, amesema, jeshi hilo linatilia shaka ulinzi katika ubalozi wa Marekani nchini na kwamba upelelezi unaendelea kwa kushirikiana na maofisa wa usalama katika ubalozi huo.
Kwa mujibu wa Kova, ulinzi umeimarishwa katika balozi zote nchini.
Chanzo: Gazeti la Habari Leo
Wanafunzi hao wa shule ya Biafra wilayani Kinondoni, Dar es Salaam, walikamatwa jana saa tisa alasiri.
Mtuhumiwa mkuu wa mpango huo wa kuulipua ubalozi wa Marekani, Nassib Zukheri alikamatwa Jumapili saa tatu usiku wakati akifungua koki ya tanki la mafuta katika ubalozi huo.
Nassib ni mwanafunzi wa kidato cha pili katika shule ya Biafra, yupo polisi anahojiwa.
Inadaiwa kuwa mtoto huyo anayekadiriwa kuwa na umri wa kati ya miaka 15 hadi 17 aliingia katika ubalozi huo kwa kupitia geti namba tatu.
Mkuu wa polisi kandaa maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova, amesema, jeshi hilo linatilia shaka ulinzi katika ubalozi wa Marekani nchini na kwamba upelelezi unaendelea kwa kushirikiana na maofisa wa usalama katika ubalozi huo.
Kwa mujibu wa Kova, ulinzi umeimarishwa katika balozi zote nchini.
Chanzo: Gazeti la Habari Leo