Kwa kuanza napenda kuchukua fursa hii kumshukuru sana mwenyezi Mungu kwa kuniruhusu niendelee kula licha ya uovu mwingi ninaotenda kila siku hapa duniani. Pia kwa wale ambao ndugu, marafiki na jamaa zao walikatishwa na mwenyezi Mungu kuendelea kula, nachukua muda huu kuwapa pole.
Waliotangulia kuona jua kabla yetu walisema "kila lenye mwanzo halikosi mwisho", ndugu na rafiki zangu wana JF, hatimae zile siku 60 ili niapishwe kuwa WAZIRI WA UPUUZI NA MIPANGO YA GHAFLA GHAFLA zinahitimishwa kesho. Napenda kuchukua muda huu kuwakaribisha katika sherehe hizo zitakazofanyika mnamo saa 10:30 jioni. Baadhi ya mambo ambayo wizara yangu itayashugulikia ni haya yafuatayo.
1. Kuhamasisha wananchi kuacha upuuzi wa kuchagua viongozi njaa na wasiokuwa na uwezo wa kupigania maslahi ya wapigakura wao.
2. Kuelimisha wananchi waache upuuzi wa kuiga kila wanachoona katika vioo vyao vinavyofanywa na wazungu, badala yake waige yale mazuri tu.
3. Kuelimisha wananchi waache kusikila maada za kipuuzi kama ile ya udini, maana hakuna mwenye uhakika wa dini yake kama inakubalika mbele za mwenyezi Mungu, maana haya ni mapokeo tu na zaidi kila mtu anaabudu dini aliyopo kutokana na dini hiyo kuwa ya kwanza kuingizwa eneo lake.
Mambo ya upuuzi ni mengi sana, lakini hayo hapo juu ni kwa uchache tu.
WanaJF wote mnakaribishwa sana.
Ndimi WAZIRI MTEULE WA UPUUZI NA MAMBO YA GHAFLA GHAFLA.
Waliotangulia kuona jua kabla yetu walisema "kila lenye mwanzo halikosi mwisho", ndugu na rafiki zangu wana JF, hatimae zile siku 60 ili niapishwe kuwa WAZIRI WA UPUUZI NA MIPANGO YA GHAFLA GHAFLA zinahitimishwa kesho. Napenda kuchukua muda huu kuwakaribisha katika sherehe hizo zitakazofanyika mnamo saa 10:30 jioni. Baadhi ya mambo ambayo wizara yangu itayashugulikia ni haya yafuatayo.
1. Kuhamasisha wananchi kuacha upuuzi wa kuchagua viongozi njaa na wasiokuwa na uwezo wa kupigania maslahi ya wapigakura wao.
2. Kuelimisha wananchi waache upuuzi wa kuiga kila wanachoona katika vioo vyao vinavyofanywa na wazungu, badala yake waige yale mazuri tu.
3. Kuelimisha wananchi waache kusikila maada za kipuuzi kama ile ya udini, maana hakuna mwenye uhakika wa dini yake kama inakubalika mbele za mwenyezi Mungu, maana haya ni mapokeo tu na zaidi kila mtu anaabudu dini aliyopo kutokana na dini hiyo kuwa ya kwanza kuingizwa eneo lake.
Mambo ya upuuzi ni mengi sana, lakini hayo hapo juu ni kwa uchache tu.
WanaJF wote mnakaribishwa sana.
Ndimi WAZIRI MTEULE WA UPUUZI NA MAMBO YA GHAFLA GHAFLA.