Ngongo
JF-Expert Member
- Sep 20, 2008
- 18,931
- 31,175
Mamia ya wakazi wa vitongoji vya Oloirien na Kijenge Mjini Arusha jana walijitokeza kutoa ushahidi mbele ya Kamati iliyoundwa na Mkuu wa Mkoa wa Arusha kuchunguza mauaji ya vijana wawili yaliyofanywa na polisi hivi karibuni.
Wananchi hao wakiwemo wafanyabiashara, walinzi wa taasisi zilizopo karibu na eneo hilo walianza kumiminika katika viwanja vya Kanisa Katoliki ilikojichimbia Kamati hiyo kuanzia saa mbili asubuhi.
Katika viwanja hivyo vilivyopo karibu na kituo cha mafuta cha Mount Meru ambacho kinahusishwa na mauaji hayo baada ya mhudumu wake kudaiwa kupigia polisi simu akidai kuwa marehemu waliouawa ni majambazi, walionekana viongozi wa kisiasa na watu maarufu jijini hapa wakijaribu galia mambo yanavyojiri.
Wakizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kutoa ushahidi, baadhi ya mashahidi muhimu wa sakata hilo (majina tunayahifadhi) walisema kuwa waliulizwa maswali kwa kina kuhusu tukio hilo ambapo walidai kuwa walieleza kwa ufasaha jinsi walivyoshuhdia mauaji hayo yanayodaiwa kuwa ya kinyama.
``Mimi ndio niliamua ugomvi na kisha nikaondoka muda mfupi niliporudi nikakuta mauaji, nilishangaa sana kwani ugomvi ulikuwa wa chenji, niliwaambia kila kitu shauri lao, mimi nimenawa mikono yangu,``alisema shahidi huyo.
Shahidi mwingine alidai kuwa mara baada ya vijana hao kuuawa aliiitwa na askari mmoja na kumtaka aandike maelezo ya kuwa biashara yake iliyokuwa karibu na eneo yaliofanyika mauaji ilitaka kuvamiwa na vijana hao, lakini alikataa.
``Mimi nilishangaa, nikasema hadharani sitaki, wakamwita mlinzi wangu sijui kilichoendelea, huo ndio ushahidi niliowapa Kamati,`` alisema shahidi huyo.
Katika hatua nyingine, miili ya vijana hao Shedrack Motika na Ewald Mtui imefanyiwa uchunguzi wa kitaalam na madaktari maalum kutoka Hospitali ya KCMC mkoani Kilimanjaro na makao makuu ya polisi jijini Dar es Salaam.
Wakati wa zoezi hilo likifanyika, ndugu wa marehemu walikuwa wametanda katika eneo la Hospitali ya Mkoa Arusha kufuatilia hali ya mambo.
Hata hivyo, mpaka sasa hakuna taarifa zozote zilizotolewa na kwamba taarifa kamili juu ya sakata zima litatolewa mara baada ya Kamati kumaliza kazi zake wiki ijayo.
Kamati hiyo yenye watu saba inayoongozwa na Mwanasheria wa Serikali Kanda ya Kaskazini, itaendelea tena kupokea maoni na ushahidi wa wananchi kuhusu tukio hilo. Pia itazuru eneo la mauaji yalikofanyika.
Mauaji hayo yanayodaiwa kuwa ya kinyama, yalifanywa na polisi Machi mosi mwaka huu baada ya mhudumu wa kituo cha mafuta cha Mount Meru kuzozana na marehemu hao.
Mhudumu huyo alidaiwa kumwarifu tajiri yake ambaye naye aliwapigia polisi simu ambao baadaye waliwaua vijana hao, Ewald Mtui na Shedrack Motika.
Tukio hili linaelezwa kushabihiana na jingine lililotoea katika Jiji la Dar es Slaam mwazoni mwa mwaka 2006 ambalo polisi waliwaua wafanyabishara watatu na dereva teksi mmoja.
Polisi walidai watu hao walikuwa majambazi, lakini baada ya Rais Jakaya Kikwete kuunda kwa Tume ya uchunguzi iliyoongozwa, Jaji Kipenka Musa, iligundua kwamba waliouawa hawakuwa majambazi.
Kutokana na ripoti ya Jaji Musa mashitaka ya mauaji yalifunguliwa dhidi ya polisi 13, kati yao akiwamo aliyekuwa Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dar es Salaam, Abdallah Zombe, pia akishikilia wadhifa wa Mkuu wa Upelelezi wa Polisi mkoa wa Dar es Salaam.
SOURCE: Nipashe
Wananchi hao wakiwemo wafanyabiashara, walinzi wa taasisi zilizopo karibu na eneo hilo walianza kumiminika katika viwanja vya Kanisa Katoliki ilikojichimbia Kamati hiyo kuanzia saa mbili asubuhi.
Katika viwanja hivyo vilivyopo karibu na kituo cha mafuta cha Mount Meru ambacho kinahusishwa na mauaji hayo baada ya mhudumu wake kudaiwa kupigia polisi simu akidai kuwa marehemu waliouawa ni majambazi, walionekana viongozi wa kisiasa na watu maarufu jijini hapa wakijaribu galia mambo yanavyojiri.
Wakizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kutoa ushahidi, baadhi ya mashahidi muhimu wa sakata hilo (majina tunayahifadhi) walisema kuwa waliulizwa maswali kwa kina kuhusu tukio hilo ambapo walidai kuwa walieleza kwa ufasaha jinsi walivyoshuhdia mauaji hayo yanayodaiwa kuwa ya kinyama.
``Mimi ndio niliamua ugomvi na kisha nikaondoka muda mfupi niliporudi nikakuta mauaji, nilishangaa sana kwani ugomvi ulikuwa wa chenji, niliwaambia kila kitu shauri lao, mimi nimenawa mikono yangu,``alisema shahidi huyo.
Shahidi mwingine alidai kuwa mara baada ya vijana hao kuuawa aliiitwa na askari mmoja na kumtaka aandike maelezo ya kuwa biashara yake iliyokuwa karibu na eneo yaliofanyika mauaji ilitaka kuvamiwa na vijana hao, lakini alikataa.
``Mimi nilishangaa, nikasema hadharani sitaki, wakamwita mlinzi wangu sijui kilichoendelea, huo ndio ushahidi niliowapa Kamati,`` alisema shahidi huyo.
Katika hatua nyingine, miili ya vijana hao Shedrack Motika na Ewald Mtui imefanyiwa uchunguzi wa kitaalam na madaktari maalum kutoka Hospitali ya KCMC mkoani Kilimanjaro na makao makuu ya polisi jijini Dar es Salaam.
Wakati wa zoezi hilo likifanyika, ndugu wa marehemu walikuwa wametanda katika eneo la Hospitali ya Mkoa Arusha kufuatilia hali ya mambo.
Hata hivyo, mpaka sasa hakuna taarifa zozote zilizotolewa na kwamba taarifa kamili juu ya sakata zima litatolewa mara baada ya Kamati kumaliza kazi zake wiki ijayo.
Kamati hiyo yenye watu saba inayoongozwa na Mwanasheria wa Serikali Kanda ya Kaskazini, itaendelea tena kupokea maoni na ushahidi wa wananchi kuhusu tukio hilo. Pia itazuru eneo la mauaji yalikofanyika.
Mauaji hayo yanayodaiwa kuwa ya kinyama, yalifanywa na polisi Machi mosi mwaka huu baada ya mhudumu wa kituo cha mafuta cha Mount Meru kuzozana na marehemu hao.
Mhudumu huyo alidaiwa kumwarifu tajiri yake ambaye naye aliwapigia polisi simu ambao baadaye waliwaua vijana hao, Ewald Mtui na Shedrack Motika.
Tukio hili linaelezwa kushabihiana na jingine lililotoea katika Jiji la Dar es Slaam mwazoni mwa mwaka 2006 ambalo polisi waliwaua wafanyabishara watatu na dereva teksi mmoja.
Polisi walidai watu hao walikuwa majambazi, lakini baada ya Rais Jakaya Kikwete kuunda kwa Tume ya uchunguzi iliyoongozwa, Jaji Kipenka Musa, iligundua kwamba waliouawa hawakuwa majambazi.
Kutokana na ripoti ya Jaji Musa mashitaka ya mauaji yalifunguliwa dhidi ya polisi 13, kati yao akiwamo aliyekuwa Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dar es Salaam, Abdallah Zombe, pia akishikilia wadhifa wa Mkuu wa Upelelezi wa Polisi mkoa wa Dar es Salaam.
SOURCE: Nipashe