Zimmermann
JF-Expert Member
- Sep 28, 2010
- 2,802
- 1,242
Mwandishi wa Polisi, Zanzibar
JESHI Polisi visiwani Zanzibar, limewaagiza wamiliki na wafanyabiashara wa baa visiwani humo, kuchukua tahadhari kwa kuweka walinzi imara katika maeneo yanayozunguuka nyumba za biashara hiyo, ili kuepuka matukio ya uchomaji wa baa zao.
Rai hiyo ilitolewa jana na Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja, Aziz Juma Mohammed, alipokuwa akizungumza katika hafla ya kutunuku vyeti vya sifa na zawadi kwa askari polisi waliozima matukio ya kihalifu na kukamata silaha. Kamanda Aziz alisema matukio ya watu kuchoma moto baa, yanaweza kuzuilika kama kila mfanyabiashara wa baa ataweka walinzi imara wanaoweza kukabiliana na watu wanaojichukulia sheria mkokononi.
Hata hivyo Kamanda Aziz alisema polisi kwa upandewao wataendelea na juhudi za kufanya doria za mara kwa mara katika maeneo mbalimbali na kutafuta taarifa za kiintelijensia ili kuwabaini na kuwakamata wale wote wanaojihusisha na vitendo hivyo.
Alikiri kuwa ingawa kuna matukio ya moto yanayotokana na ajali za kawaida, lakini baadhi ya matukio yanafanywa kwa makusudi na watu wachache ama kwa sababu za imani zao za kidini au visa.Kamanda huyo alisema polisi wataendelea kuwachukulia hatua wale wote watakaobainika kuwa wamekuwa wakishiriki katika vitendo hivyo.Alisema hiyo inatokana na ukweli kwamba wote ni wahalifu wanaopaswa kufikishwa mahakamani.
Source: Mwananchi
JESHI Polisi visiwani Zanzibar, limewaagiza wamiliki na wafanyabiashara wa baa visiwani humo, kuchukua tahadhari kwa kuweka walinzi imara katika maeneo yanayozunguuka nyumba za biashara hiyo, ili kuepuka matukio ya uchomaji wa baa zao.
Rai hiyo ilitolewa jana na Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja, Aziz Juma Mohammed, alipokuwa akizungumza katika hafla ya kutunuku vyeti vya sifa na zawadi kwa askari polisi waliozima matukio ya kihalifu na kukamata silaha. Kamanda Aziz alisema matukio ya watu kuchoma moto baa, yanaweza kuzuilika kama kila mfanyabiashara wa baa ataweka walinzi imara wanaoweza kukabiliana na watu wanaojichukulia sheria mkokononi.
Hata hivyo Kamanda Aziz alisema polisi kwa upandewao wataendelea na juhudi za kufanya doria za mara kwa mara katika maeneo mbalimbali na kutafuta taarifa za kiintelijensia ili kuwabaini na kuwakamata wale wote wanaojihusisha na vitendo hivyo.
Alikiri kuwa ingawa kuna matukio ya moto yanayotokana na ajali za kawaida, lakini baadhi ya matukio yanafanywa kwa makusudi na watu wachache ama kwa sababu za imani zao za kidini au visa.Kamanda huyo alisema polisi wataendelea kuwachukulia hatua wale wote watakaobainika kuwa wamekuwa wakishiriki katika vitendo hivyo.Alisema hiyo inatokana na ukweli kwamba wote ni wahalifu wanaopaswa kufikishwa mahakamani.
Source: Mwananchi