Waliokuwa wafanyakazi New Habari waitaka Serikali imshinikize Rostam Aziz awalipe madai yao. Kuandamana nyumbani kwa Rostam na Bashe

Fred Katulanda

JF-Expert Member
Apr 1, 2011
374
509
Wafanyakazi zaidi ya 200 waliokuwa wameajiriwa kwenye kampuni ya new habari(2006) limited inayomiliki magazeti ya Mtanzania na mengine wameiomba Serikali imshinikize mfanyabiashara maarufu, Rostam Aziz kuwalipa fedha zao ambazo ni mafao yao.

Msemaji wa wafanyakazi hao, Arodia Peter amesema wanaomba taarifa zao zimfikie Rais Samia baada ya mwajiri wao ya New Habari inayomilikiwa na Rostam Aziz chini ya afisa mtendaji mkuu, Hussein Bashe ambae sasa ni waziri wa kilimo kwa kushindwa kuwapelekea mafao yao kwenye mifuko ya hifadhi ya kijamii.

Msemaji amedai Rostam Aziz kupitia kwa mtendaji mkuu, Hussein Bashe waliwaondoa kazini Mei 31, 2019 bila kuwalipa stahiki za mafao kupitia mifuko ya hifadhi ya jamii ya NSSF na iliyokuwa PPF kwa mujibu wa sheria.

Pia wamedai mwajiri wao aliwaondoa kazini kwa lazima wafanyakazi wake bila kutangaza kwa umma pia sababu za kufanya hivyo kwa mujibu wa sheria.

Lakini pamoja na hatua ya kuwaondoa hawajawalipa mafao kama ambavyo walikuwa wamewaahidi.

Rostam.jpg


=====

UPDATES: 05 Februari 2022

======

Baada ya Masaa 24 Toka Wanaodai Mafao kuongea na Wanahabari, Hatimaye Wafanyakazi Wamekiri kwamba Rostam Aziz kawalipa Mafao yao.

Wakati akosoma taarifa kwa vyombo vya Habari, Arodia Peter amesema kwamba juzi baada ya kuongea na vyombo vya habari, Rostam Aziz aliwaita kwa kikao cha dharura. Rostam alisema alikuwa hana habari kama anadaiwa, hivyo muda huo huo akafanya Malipo yote waliyokuwa wakidai ikiwemo Mafao kwenye mifuko ya Jamii.

Wafanyakazi wa New Habari ambayo inamiliki Magazeti ya Mtanzania, Rai, Bingwa, Dimba na The African, Walikuwa wanazungushwa kulipwa mafao yao kwa miaka Mitatu baada ya kuachishwa kazi.

Pia, soma:
Rostam Aziz akubali yaishe, atoa hundi za malipo ya waliokuwa wafanyakazi wa New Habari (2006)
 
Na Andrew Chale, Dar es Salaam.

WAFANYAKAZI zaidi ya 200, Waliokuwa wakifanyakazi katika kampuni ya New Habari (2006) Ltd, wametoa siku 14 kwa Mmiliki wa Kampuni hiyo, Mfanyabiashara na Bilionea Rostam Aziz awe amepeleka fedha za mafao katika mifuko ya Hifadhi ya Jamii ikiwemo NSSF na PSSSF kiasi cha zaidi ya Bilioni 3.

Akizungumza mbele ya Waandishi wa Habari mapema leo Februari 3. 2022, Katibu wa waliokuwa wafanyakazi wa New Habari (2006) Ltd, Arodia Peter alisema licha ya kusubiria kwa muda mrefu taratibu za kisheria dhidi ya mfanyabiashara huyo pamoja na Mbunge wa Nzega Mjini ambaye pia ni Waziri wa Kilimo
Hussein Bashe kushindwa kuwasilisha mafao yao kwenye mifuko licha ya kuwakata michango kwa miaka zaidi ya 10.

"Walikuwa wanatukata mishahara yetu kila mwezi pamoja na michango ya mwajiri kwa mujibu wa sheria kwa zaidi ya miaka 10.

Licha ya kuhoji, Mwajili alituhaminisha kuwa anapeleka makato yetu katika mifuko husika...

Lakini tunashangaa Watendaji wa mifuko hiyo kutochukua hatua yoyote kwa mwajiri kwa zaidi ya miaka 10 tofauti na sheria ya mifuko hiyo unayoelekeza." Alisema Arodia.

Na kuongeza kuwa;
"Tunapenda kufikisha taarifa na kilio chetu kwa Rais Samia Suluhu Hassan juu ya madhila yanayotupata na yanayoendelea dhidi ya Rostam Aziz na Afisa Mtendaji Mkuu, Mbunge na Waziri wa kilimo Hussein Bashe kwani wameshindwa kabisa kutupelekea mafao yetu katika mifuko ya Hifadhi ya Jamii." alisema Arodia.

Rostam Aziz na Hussein Bashe walituondoa kazini Mei 31 mwaka 2019 bila kutulipa stahiki za mafao yetu kwa mifuko ya NSSF na PSSSF kwa mujibu wa Sheria.

Ambapo alifafanua kuwa; Mtendaji mkuu Hussein Bashe, aliwaondoa kazini kwa lazima wafanyakazi wote bila kutangaza kwa umma sababu ya kufanya hivyo kama sheria inavyotaka.

Kwa upande wake Mshauri katika kikao hicho waliokuwa wafanyakazi wa New Habari (2006), Mzee Balinagwe Mwambungu alitoa kilio chake kwa wadaiwa hao Rostam Aziz na Hussein Bashe, kuwa kwa sasa wanaishi kwa mateso huku pesa zao zikiwa zipo kwa wadaiwa.

"Wapo wenzetu wametangulia mbele za haki na familia zao tuonao hapa wakidai malipo ya wapendwa wao.

Waliotangulia mbele za haki ni pamoja na: Aliyekiwa Mhariri Kanda ya Kaskazini, Elia Mbonea, Mhariri wa Maudhui ya Habari wa kampumi, Mwalimu Chrysotom Rweyemamu, Mhariri wa Habari wa gazeti la Rai, Innocent Mnyuku, Mhariri wa Makala wa gazeti la Rai, Mayege Mayege, Mhariri wa michezo, Asha Muhaji.

Pia wengine Afisa Utawala Msaidizi, Benjamin Mhina pamoja na Katibu Muhtasi Roida Kiverege. Hawa wote wametangulia mbele za haki na bado wanadai mafao yao kupitia kwa familia zao ambazo zinaishi kwa shida" alisema Mzee Mwambungu.

Hata hivyo kwa kauli moja wawakilishi hao wametangaza kufanya maandamano ya amani yasiyokuwa na ukomo nyumbani kwa Rostam Aziz na ofisini kwake, na pia maandamano hayo ya amani kwa Hussein Bashe na ofisini kwenye mifuko ya hifadhi ya Jamii.


Wafanyakazi hao zaidi ya 200 ni pamoja kutoka Tanzania nzima wakiweno Waandishi wa habari ambao ndo kundi kubwa, watu wa IT, Madereva, Walinzi, wafagiaji, mafundi mitambo na wengine wengi.

Mwisho.


Caption :

Katibu wa Waliokuwa Wafanyakazi wa New Habari (2006) Ldt, Bi. Arodia Peter akizungumza na Waandishi wa Habari (Hawapo pichani) mapema leo Februari 3.2022. Dar es Salaam.
IMG-20220203-WA0038.jpg

IMG-20220203-WA0041.jpg

IMG-20220203-WA0044.jpg
 
Na Andrew Chale, Dar es Salaam.

WAFANYAKAZI zaidi ya 200, Waliokuwa wakifanyakazi katika kampuni ya New Habari (2006) Ltd, wametoa siku 14 kwa Mmiliki wa Kampuni hiyo, Mfanyabiashara na Bilionea Rostam Aziz awe amepeleka fedha za mafao katika mifuko ya Hifadhi ya Jamii ikiwemo NSSF na PSSSF kiasi cha zaidi ya Bilioni 3.

Akizungumza mbele ya Waandishi wa Habari mapema leo Februari 3. 2022, Katibu wa waliokuwa wafanyakazi wa New Habari (2006) Ltd, Arodia Peter alisema licha ya kusubiria kwa muda mrefu taratibu za kisheria dhidi ya mfanyabiashara huyo pamoja na Mbunge wa Nzega Mjini ambaye pia ni Waziri wa Kilimo
Hussein Bashe kushindwa kuwasilisha mafao yao kwenye mifuko licha ya kuwakata michango kwa miaka zaidi ya 10.

"Walikuwa wanatukata mishahara yetu kila mwezi pamoja na michango ya mwajiri kwa mujibu wa sheria kwa zaidi ya miaka 10.

Licha ya kuhoji, Mwajili alituhaminisha kuwa anapeleka makato yetu katika mifuko husika...

Lakini tunashangaa Watendaji wa mifuko hiyo kutochukua hatua yoyote kwa mwajiri kwa zaidi ya miaka 10 tofauti na sheria ya mifuko hiyo unayoelekeza." Alisema Arodia.

Na kuongeza kuwa;
"Tunapenda kufikisha taarifa na kilio chetu kwa Rais Samia Suluhu Hassan juu ya madhila yanayotupata na yanayoendelea dhidi ya Rostam Aziz na Afisa Mtendaji Mkuu, Mbunge na Waziri wa kilimo Hussein Bashe kwani wameshindwa kabisa kutupelekea mafao yetu katika mifuko ya Hifadhi ya Jamii." alisema Arodia.

Rostam Aziz na Hussein Bashe walituondoa kazini Mei 31 mwaka 2019 bila kutulipa stahiki za mafao yetu kwa mifuko ya NSSF na PSSSF kwa mujibu wa Sheria.

Ambapo alifafanua kuwa; Mtendaji mkuu Hussein Bashe, aliwaondoa kazini kwa lazima wafanyakazi wote bila kutangaza kwa umma sababu ya kufanya hivyo kama sheria inavyotaka.

Kwa upande wake Mshauri katika kikao hicho waliokuwa wafanyakazi wa New Habari (2006), Mzee Balinagwe Mwambungu alitoa kilio chake kwa wadaiwa hao Rostam Aziz na Hussein Bashe, kuwa kwa sasa wanaishi kwa mateso huku pesa zao zikiwa zipo kwa wadaiwa.

"Wapo wenzetu wametangulia mbele za haki na familia zao tuonao hapa wakidai malipo ya wapendwa wao.

Waliotangulia mbele za haki ni pamoja na: Aliyekiwa Mhariri Kanda ya Kaskazini, Elia Mbonea, Mhariri wa Maudhui ya Habari wa kampumi, Mwalimu Chrysotom Rweyemamu, Mhariri wa Habari wa gazeti la Rai, Innocent Mnyuku, Mhariri wa Makala wa gazeti la Rai, Mayege Mayege, Mhariri wa michezo, Asha Muhaji.

Pia wengine Afisa Utawala Msaidizi, Benjamin Mhina pamoja na Katibu Muhtasi Roida Kiverege. Hawa wote wametangulia mbele za haki na bado wanadai mafao yao kupitia kwa familia zao ambazo zinaishi kwa shida" alisema Mzee Mwambungu.

Hata hivyo kwa kauli moja wawakilishi hao wametangaza kufanya maandamano ya amani yasiyokuwa na ukomo nyumbani kwa Rostam Aziz na ofisini kwake, na pia maandamano hayo ya amani kwa Hussein Bashe na ofisini kwenye mifuko ya hifadhi ya Jamii.


Wafanyakazi hao zaidi ya 200 ni pamoja kutoka Tanzania nzima wakiweno Waandishi wa habari ambao ndo kundi kubwa, watu wa IT, Madereva, Walinzi, wafagiaji, mafundi mitambo na wengine wengi.

Mwisho.


Caption :

Katibu wa Waliokuwa Wafanyakazi wa New Habari (2006) Ldt, Bi. Arodia Peter akizungumza na Waandishi wa Habari (Hawapo pichani) mapema leo Februari 3.2022. Dar es Salaam.View attachment 2106448
View attachment 2106451
View attachment 2106452
Sasa kama hawakuchangiwa mafao hawawezi kulipwa..

Hapa ni sheria kuchukua mkondo wake kwa nini mwajiri hakupeleka michango yao? Na je wao walikuwa wanakatwa? Mwisho je hawakujiunga na vyama vya wafanyakazi?

Ila tuache utami maisha ya biashara miaka 6 iliyopita yalikuwa magumu Sana watu wengi walikuwa wahanga nikiwemo mimi.
 
WALIOKUWA WAFANYAKAZI WA NEW HABARI (2006) LTD WATOA SIKU 14 KWA MFANYABIASHARA ROSTAM AZIZ KULIPA MAFAO YAO
Screenshots_2022-02-03-14-36-34.png
Screenshots_2022-02-03-14-39-08.png
Screenshots_2022-02-03-14-38-11.png
Screenshots_2022-02-03-14-37-20.png



Na Andrew Chale, Dar es Salaam.

WAFANYAKAZI zaidi ya 200, Waliokuwa wakifanyakazi katika kampuni ya New Habari (2006) Ltd, wametoa siku 14 kwa Mmiliki wa Kampuni hiyo, Mfanyabiashara na Bilionea Rostam Aziz awe amepeleka fedha za mafao katika mifuko ya Hifadhi ya Jamii ikiwemo NSSF na PSSSF kiasi cha zaidi ya Bilioni 3.

Akizungumza mbele ya Waandishi wa Habari mapema leo Februari 3. 2022, Katibu wa waliokuwa wafanyakazi wa New Habari (2006) Ltd, Arodia Peter alisema licha ya kusubiria kwa muda mrefu taratibu za kisheria dhidi ya mfanyabiashara huyo pamoja na Mbunge wa Nzega Mjini ambaye pia ni Waziri wa Kilimo
Hussein Bashe kushindwa kuwasilisha mafao yao kwenye mifuko licha ya kuwakata michango kwa miaka zaidi ya 10.

"Walikuwa wanatukata mishahara yetu kila mwezi pamoja na michango ya mwajiri kwa mujibu wa sheria kwa zaidi ya miaka 10.

Licha ya kuhoji, Mwajili alituhaminisha kuwa anapeleka makato yetu katika mifuko husika...

Lakini tunashangaa Watendaji wa mifuko hiyo kutochukua hatua yoyote kwa mwajiri kwa zaidi ya miaka 10 tofauti na sheria ya mifuko hiyo unayoelekeza." Alisema Arodia.

Na kuongeza kuwa;
"Tunapenda kufikisha taarifa na kilio chetu kwa Rais Samia Suluhu Hassan juu ya madhila yanayotupata na yanayoendelea dhidi ya Rostam Aziz na Afisa Mtendaji Mkuu, Mbunge na Waziri wa kilimo Hussein Bashe kwani wameshindwa kabisa kutupelekea mafao yetu katika mifuko ya Hifadhi ya Jamii." alisema Arodia.

Rostam Aziz na Hussein Bashe walituondoa kazini Mei 31 mwaka 2019 bila kutulipa stahiki za mafao yetu kwa mifuko ya NSSF na PSSSF kwa mujibu wa Sheria.

Ambapo alifafanua kuwa; Mtendaji mkuu Hussein Bashe, aliwaondoa kazini kwa lazima wafanyakazi wote bila kutangaza kwa umma sababu ya kufanya hivyo kama sheria inavyotaka.

Kwa upande wake Mshauri katika kikao hicho waliokuwa wafanyakazi wa New Habari (2006), Mzee Balinagwe Mwambungu alitoa kilio chake kwa wadaiwa hao Rostam Aziz na Hussein Bashe, kuwa kwa sasa wanaishi kwa mateso huku pesa zao zikiwa zipo kwa wadaiwa.

"Wapo wenzetu wametangulia mbele za haki na familia zao tuonao hapa wakidai malipo ya wapendwa wao.

Waliotangulia mbele za haki ni pamoja na: Aliyekiwa Mhariri Kanda ya Kaskazini, Elia Mbonea, Mhariri wa Maudhui ya Habari wa kampumi, Mwalimu Chrysotom Rweyemamu, Mhariri wa Habari wa gazeti la Rai, Innocent Mnyuku, Mhariri wa Makala wa gazeti la Rai, Mayege Mayege, Mhariri wa michezo, Asha Muhaji.

Pia wengine Afisa Utawala Msaidizi, Benjamin Mhina pamoja na Katibu Muhtasi Roida Kiverege. Hawa wote wametangulia mbele za haki na bado wanadai mafao yao kupitia kwa familia zao ambazo zinaishi kwa shida" alisema Mzee Mwambungu.

Hata hivyo kwa kauli moja wawakilishi hao wametangaza kufanya maandamano ya amani yasiyokuwa na ukomo nyumbani kwa Rostam Aziz na ofisini kwake, na pia maandamano hayo ya amani kwa Hussein Bashe na ofisini kwenye mifuko ya hifadhi ya Jamii.


Wafanyakazi hao zaidi ya 200 ni pamoja kutoka Tanzania nzima wakiweno Waandishi wa habari ambao ndo kundi kubwa, watu wa IT, Madereva, Walinzi, wafagiaji, mafundi mitambo na wengine wengi.
 
Hivi wandishi wa habari ni vilaza kiasi hiki?
Hawajui hatua za kufanya?
Shauri hili lafaa kupelekwa wizara ya kazi na wawe na mwanasheria.
Wao wanafikiri haki inapatikana press conference,,
 
Halafu huyu Rostam ndo kapata asilimia nyingi Williamson Diamonds Mwadui. Yaani nawaonea huruma wafanyakazi. Mafisadi makubwa haya Rostam na huyu msomali Bashe.
Share au hisa kwa kiswahili huwa zinauzwa, hazigawiwi kama sandakslawe.
Mfano wewe kama una hela za kutosha unaweza kuwa mmiliki wa kampuni ya Apple. ,
Pesa zako tu
 
Ilikua kampuni kubwa sana nini?, Rostam kainunua toka kwa ulinwengu, haizidi hata miaka kumi nyuma,,, leo inadaiwa bilioni 3tena za mafao,, kwa wafanyakazi 200 tu,,
Mbona hesabu hazikai sawa?
Usisahau interest ya 20% ya mshahara iliyotakiwa kuwasilishwa kwa wakati katika mifuko
 
Kampuni si ni an individual?

Filisi kampuni kama bado ipo mchukue cha kwenu..., itakuwa sio hekima pesa itoke Williamson Diamond au Taifa Gesi ili iweze kulipia huku
 
Back
Top Bottom