Kaplizer
JF-Expert Member
- Apr 27, 2014
- 710
- 569
WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI
WAOMBAJI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA MAFUNZO YA UALIMU NGAZI YA STASHAHADA YA JUU (MIAKA 3) MWAKA WA MASOMO 2014/2015
MAELEKEZO:
Waombaji waliochaguliwa kujiunga na Mafunzo ya Ualimu mwaka wa masomo 2014/2015 wanatakiwa kuripoti katika Vyuo walivyopangiwa tarehe 06/10/2014. Fomu za maelekezo (Joining Instructions) zitatolewa na chuo husika na zitatumwa kwa waliochaguliwa tu. Waliochaguliwa wanatakiwa kufika vyuoni wakiwa na mahitaji yaliyoainishwa kwenye fomu ya kujiunga na Chuo. Aidha, fomu hizi zinapatikana pia kwenye Tovuti ya Wizara:www.moe.go.tz; NACTE:www.nacte.go.tz; na TAMISEMI: www.pmoralg.go.tz
Muhimu:
1. Waombaji waliochaguliwa ni wale wenye ufaulu wa Daraja la I hadi III
2. Waliochaguliwa wanatakiwa kuwasilisha Vyeti halisi vya Baraza la Mitihani la Tanzania Kidato cha NNE na SITA (CSEE na ACSEE) na vyeti vya kuhitimu Elimu ya Sekondari na Mafunzo ya Ualimu.
3. Ada ya mafunzo Stashahada ya Juu ni 600,000/= kwa mwaka (Muhula wa kwanza 300,000/= na muhula wa pili 300,000/=)
4. Wanafunzi watakaosajiliwa Chuoni ni wale waliopo kwenye orodha hii tu na SIYO vinginevyo, waweza pata orodha hyo kwa kufungua kiunganishi kimoja wapo hapo chini.
Stashahada_ya_juu_elimu_maalum.pdf
Stashahada_ya_juu_lugha.pdf
Stashahada_ya_juu_sayansi_na_hisabati.pdf
Stashahada_ya_kawaida_elimu_ya_awali.pdf
Stashahada_ya_kawaida_elimu_ya_michezo.pdf
Stashahada_ya_kawaida_elimu_ya_msingi.pdf
Attachments
-
stashahada_ya_juu_elimu_maalum.pdf390.7 KB · Views: 364
-
stashahada_ya_juu_lugha.pdf254.1 KB · Views: 213
-
stashahada_ya_juu_sayansi_na_hisabati.pdf531.7 KB · Views: 490
-
Stashahada_ya_kawaida_elimu_ya_awali.pdf4.9 MB · Views: 1,088
-
stashahada_ya_kawaida_elimu_ya_michezo.pdf341.6 KB · Views: 305
-
stashahada_ya_kawaida_elimu_ya_msingi.pdf830.9 KB · Views: 756