Buchanan
JF-Expert Member
- May 19, 2009
- 13,199
- 1,969
Na Salim Said
WIZARA ya Elimu ya Zanzibar, imewataka walimu wa shule za serikali wanaovaa baibui kujieleza kwa maandishi sababu za kuvaa nguo hizo wawapo kazini.
Waziri wa Elimu wa Zanzibar, Haroun Ally Suleiman aliliambia gazeti hili jana kuwa wizara ina mwongozo wa mavazi kwa walimu na wanafunzi wanapokuwa shuleni hivyo hawaruhusiwi kuvaa baibui.
Alisema mwongozo huo wa mwaka 1988, ndio unaowaelekeza walimu na wanafunzi aina ya mavazi wanayopaswa kuvaa wawapo shuleni.
"Zanzibar tuna mwongozo wa mavazi kwa walimu na hata wanafunzi, ulitungwa tangu mwaka 1988," alisema Haroun. Alisema kwa mujibu wa mwongozo huo, walimu wanazuiwa kuvaa baadhi ya baibui hasa zile ambazo zinazovaliwa nyakati za jioni visiwani.
Kwa habari zaidi soma Mwananchi.
WIZARA ya Elimu ya Zanzibar, imewataka walimu wa shule za serikali wanaovaa baibui kujieleza kwa maandishi sababu za kuvaa nguo hizo wawapo kazini.
Waziri wa Elimu wa Zanzibar, Haroun Ally Suleiman aliliambia gazeti hili jana kuwa wizara ina mwongozo wa mavazi kwa walimu na wanafunzi wanapokuwa shuleni hivyo hawaruhusiwi kuvaa baibui.
Alisema mwongozo huo wa mwaka 1988, ndio unaowaelekeza walimu na wanafunzi aina ya mavazi wanayopaswa kuvaa wawapo shuleni.
"Zanzibar tuna mwongozo wa mavazi kwa walimu na hata wanafunzi, ulitungwa tangu mwaka 1988," alisema Haroun. Alisema kwa mujibu wa mwongozo huo, walimu wanazuiwa kuvaa baadhi ya baibui hasa zile ambazo zinazovaliwa nyakati za jioni visiwani.
Kwa habari zaidi soma Mwananchi.