Lyimo
JF-Expert Member
- Mar 7, 2006
- 3,826
- 2,017
Aliyekuwa Waziri wa Ulinzi nchini Ujerumani Bw. zu Guttenberg amewajibika kwa kujiuzulu nafasi hiyo baada ya kubainika sehemu kubwa ya degree yake ya filosofia (uzamivu) alinakili kwa wengine bila kuwataja (Plagiarisim).
Habari zaidi BBC News - German Defence Minister Guttenberg resigns over thesis
Hapa Tanzania kunamalalamiko ya viongozi wetu kadhaa kuwa taaluma zao si za kiuhalali na hivyo kupewa majukumu mazito kulingana na taaluma hizo. Hawa walibainishwa kama MAFISADI WA ELIMU na Bw. Kainerugaba Msemakweli ambaye aliandika kitabu kuhusiana, ila nNi mawaziri wawili tu kwa kumbukumbu zangu (Mbunge wa Ukonga) Bw. Makongoro na Diallo walifungua kesi lakini wanazikimbia, na karibuni zitafutwa. Wengine hawakujitokeza hata kujisingizia kukanusha. Kwanini watanzania hatulipigii kelele hili, inawezekana aina hii ya ufisadi ni kikwazo katika maendeleo ya nchi yetu. Na pia inachochea wengine kutafuta njia za mkato kama hizi. Nawakilisha.
Habari zaidi BBC News - German Defence Minister Guttenberg resigns over thesis
Hapa Tanzania kunamalalamiko ya viongozi wetu kadhaa kuwa taaluma zao si za kiuhalali na hivyo kupewa majukumu mazito kulingana na taaluma hizo. Hawa walibainishwa kama MAFISADI WA ELIMU na Bw. Kainerugaba Msemakweli ambaye aliandika kitabu kuhusiana, ila nNi mawaziri wawili tu kwa kumbukumbu zangu (Mbunge wa Ukonga) Bw. Makongoro na Diallo walifungua kesi lakini wanazikimbia, na karibuni zitafutwa. Wengine hawakujitokeza hata kujisingizia kukanusha. Kwanini watanzania hatulipigii kelele hili, inawezekana aina hii ya ufisadi ni kikwazo katika maendeleo ya nchi yetu. Na pia inachochea wengine kutafuta njia za mkato kama hizi. Nawakilisha.