Mpui Lyazumbi
JF-Expert Member
- Sep 1, 2010
- 1,856
- 371
Heshima mbele watanzania. Katika kibwagizo cha kile kipindi cha dakika45 kinachorushwa na itv, waziri sitta anatupiwa swali na uchokozi kuhusu msimamo wake kwenye swala la Richmond. Bila kumumunya maneno anabainisha kuwa Richmond ni kikundi cha "wahuni" wachache na hivyo si haki wala wajibu wa watanzania kulipa deni/tozo yoyote. Hayo nimeyaona kwenye kibwagizo kunachoashiria kuwa kipindi hicho kitarushwa ama leo(jumatatu) au jumatatu yoyote saa 3 usiku. Anaponichanganya ni hapa:-
- Kwenye ile ripoti ni kipi kilisalia anachokijua yeye?
- Kama ni kikundi cha wahuni ni kwa nini tulitumia nguvu nyingi na kodi zetu kwenye swala la "wahuni".
- Wakati ule alishindwa nini kusimamia haki na wajibu wa watanzania kwenye sakata hili.
- Anashindwa nini kuweka ukweli bayana, na swala hili liishe ili tuanze ukurasa upya.
- ....
- .......aaagrr