Wakili Mwabukusi kachukua point zote kuhusu mkataba wa DP World

Yesu Anakuja

JF-Expert Member
Apr 10, 2019
9,502
19,304
Mwanasiasa ambaye hakuwa anavuma sana, lakini kwa muda mfupi amebeba point zote katia mfukoni. hii ni kwasababu ameongea kile kilichopo mioyoni mwa watanganyika, na watu wanaona kama yeye ndio mkombozi wao and trust me, Serikali iende naye polepole manake kufanya chochote kwa mwabukusi kutaleta taharuki kubwa mno kwani ana sapoti ya majority ya Watanganyika ila ni kimya kimya. Ukitaka kujua kuwa wananchi wengi hawaitaki hii DP WORLD angalia namna Mwabukusi alivyotrendi.

Jamaa alishafanya kazi kama Mwanasheria wa Serikali huko wizarani vya kutosha, anajua anachoongea na ni wachache sana wanaweza kubishana naye kwa hoja, pia amekuwa wakili wa kujitegemea miaka ya kutosha, na hadi leo. Na inasemekana misimamo yake hata mahakamani ndio iko hivyo hivyo, hanaga mchezo kwenye mambo ya msingi hivyo anavyoongea ndivyo alivyo.

imagine angekuwa na chama chake, angekuwa na supporters wengi sana kwa muda mfupi. zamani wanasema alikuwa CHADEMA, ndio alikuwa anatetea wafuasi wa CHADEMA mahakamani Mbeya, akaona wanamzingua akaenda zake kwa NCCR Mageuzi. nadhani sasa hivi anaweza kurudi CHADEMA au abaki NCCR.
 
Mwanasiasa ambaye hakuwa anavuma sana, lakini kwa muda mfupi amebeba point zote katia mfukoni. hii ni kwasababu ameongea kile kilichopo mioyoni mwa watanganyika, na watu wanaona kama yeye ndio mkombozi wao. and trust me, serikali iende naye polepole manake kufanya chochote kwa mwabukusi kutaleta taharuki kubwa mno kwani ana sapoti ya majority ya Watanganyika ila ni kimya kimya. ukitaka kujua kuwa wananchi wengi hawaitaki hii DP WORLD angalia namna mwabukusi alivyotrendi.

Jamaa alishafanya kazi kama mwanasheria wa serikali huko wizarani vya kutosha, anajua anachoongea na ni wachache sana wanaweza kubishana naye kwa hoja, pia amekuwa wakili wa kujitegemea miaka ya kutosha, na hadi leo. na inasemekana misimamo yake hata mahakamani ndio iko hivyo hivyo, hanaga mchezo kwenye mambo ya msingi. hivyo anavyoongea ndivyo alivyo.

imagine angekuwa na chama chake, angekuwa na supporters wengi sana kwa muda mfupi. zamani wanasema alikuwa chadema, ndio alikuwa anatetea wafuasi wa chadema mahakamani mbeya, akaona wanamzingua akaenda zake kwa NCCR mageuzi. nadhani sasaivi anaweza kurudi chadema au abaki nccr.
Hiki chuma kinatisha,,Nami CCM nakisikiliza Ila Jamaa mkali Mno.Yuko seriously Mnoo
 
WAKILI BONIFACE MWABUKUSI;KAMA HAMTATUSIKILIZA,TUTAZUNGUMZA LUGHA MTAKAYOTUSIKILIZA,HATUTARUHUSU MZANZIBARI KUFANYA MAMBO YA HOVYO KWENYE MALI ZA TANGANYIKA.

"Wazee wangu wa Mbeya nipo hapa kuwahakikishia Tanganyika hailiwi tena,tutafuatilia hatua kwa hatua kwenye mikataba ya Mali zote za Tanganyika" Wakili Boniface Mwabukusi

"Mkataba unatakiwa ujisimamie na ujitetee,ila watu wanautetea bila "baseline" za data na facts kwenye mkataba huo,hakuna research wala data, mkataba hauna data ambazo ni measured kisayansi watu wanacheza na maneno tu ambayo hayapo kwenye mkataba" Wakili Boniface Mwabukusi

"Mkataba wa bandari ni batili, chochote kilichofanywa nje ya sheria na nje ya katiba kirekebishwe" Wakili Boniface Mwabukusi.

"Tanganyika ni nchi kama ilivyo Zanzibar,hatutaruhusu Mzanzibari kufanya mambo ya hovyo kwenye Mali za Tanganyika,kama ambavyo Mtanganyika hawezi kufanya mambo ya hovyo kwenye Mali za Zanzibar" Wakili Boniface Mwabukusi.

"Ndoa ya Tanganyika na Zanzibar ilikuwa ndoa ya utotoni sasa tumekua tunataka tuongee tukubaliane Mali za Tanganyika ziwe chini ya Mtanganyika na Mali za Zanzibar ziwe chini ya Mzanzibari" Wakili Boniface Mwabukusi.

"Waziri Mkuu alitudanganya kuhusu kifo cha Hayati Rais John Pombe Magufuli na hajawahi kuomba radhi,na leo anatudanganya kuhusu mkataba wa bandari,akae pembeni kumsaidia Rais" Wakili Boniface Mwabukusi

"Waziri Mkuu atujibu,sheria sura 449 na sheria sura 450 kuhusu Ulinzi wa rasilimali za nchi na kuhusu ushughulikiwaji wa vifungu vyenye utata walizifuata,je vipengele vya mkataba wa bandari vinaoana na vipengele hivi vya sheria yetu" Wakili Boniface Mwabukusi.

"Waziri Mkuu atujibu,kwa nini bunge linataka kubadili sheria sasa hivi ziendane na mkataba huu wa bandari" Wakili Boniface Mwabukusi

"Tuliibinafsisha Tanesco kwa Net Solution tulipata faida gani na leo Tanesco ya nani? Tulileta watu TRL wakaishia kubeba vichwa vya treni kurudi navyo India,tulifanya hivyo hivyo kwa NBC kuuzwa bei ya kutupwa,na leo mnatuambia mna muujiza kwenye kuibinafsisha bandari" Wakili Boniface Mwabukusi

"Kama mkataba ni sahihi,Waziri Mkuu anatuambiaje tukusanye maoni,nani anakusanya maoni,yaende wapi,ya nini? kama mkataba tayari umeshapita" Wakili Boniface Mwabukusi

"Wakati nchi yetu ina Kiongozi mwenye element za Uzalendo watu fulani hawakuonekana kabisa,sasa hivi wamerudi wanatukana hadi Mahakama, Watanzania angalieni walioko nyuma ya huu mkataba"Wakili Boniface Mwabukusi.

"Kila uovu juu ya Tanganyika tutaukabili kwa jina lake na kila muovu tutamkabili kwa jinsi anavyokuja,hii ni nchi yetu hatutamuchia mtu mwingine aitetee" Wakili Boniface Mwabukusi

"Mabadiliko ya sheria yanayokwenda kufanyika ni matusi kwa Tanganyika,narudia tena Tanganyika ni nchi kama ilivyo Zanzibar" Wakili Boniface Mwabukusi.

"Tunatoa onyo kwa Kiongozi mwingine kudhani anaweza kuingia mikataba ya kuuza nchi akabaki salama,wasituchezee" Wakili Boniface Mwabukusi

"Tunawaomba Watanzania wa dini zote,Waislamu, Wakristo,Wachungaji na Mashehe na WA jadi,tufunge tarehe 14,15,16 kuomba mapenzi ya Mungu yakafanyike kwa Tanganyika na Tanzania,ahsanteni sana"Wakili Boniface Mwabukusi
 
Back
Top Bottom