Rare Sapphire
JF-Expert Member
- Jul 24, 2021
- 576
- 1,626
Mwabukusi ameyasema hayo katika mkutano na waandishi unaendelea wakati huu tar 5/9/2023 akiwa pamoja na Dr. Slaa, akisema wao watasimamia kwenye sheria na wanachotaka ni IGA kuondolewa.
Mwabukusi amesema wameonewa sababu maandamano ni haki ya kikatiba, akiongeza unapokuwa na cheo usiongozwe na mamlaka bali uongozwe na utu ili uweze kutafsiri ssheria kwa namna inayostahili.
Akisema yeye haogopi mtu yoyote, bali anawaheshimu, na heshima hii ipo pale tu kwa watu wanaofata Katiba na Sheria za nchi. Na kama wamekosa basi waadhibiwe kwa Sheria, na sio kutafuta makosa kuhalalisha kukamatwa kwao.
Pia soma: Mkutano wa waandishi wa habari unaoendelea muda huu ambapo Dkt. Slaa, Mwabukusi wanazungumza