Wakazi wa mkoa wa Lindi wameridhia kumpa muwekezaji hekari 1000 kwaajili ya uwekezaji

Mwalimu wa tuisheni

JF-Expert Member
Oct 19, 2019
5,476
8,600


Wakazi wa mkoa wa Lindi wameridhia kumpa muwekezaji hekari 1000 kwaajili ya uwekezaji.
---
Mgogoro uliodumu kwa zaidi ya miaka 12 baina ya Mwekezaji pamoja na Wananchi wa Kijiji cha Kichonda katika Halmashauri ya Wilaya ya Liwale Mkoani Lindi umetatuliwa na Naibu Waziri wa Ardhi Geofrey Pinda baada ya Wananchi wa kijiji hicho kuridhia kumpatia hekari 1000 Mwekezaji huyo.

Taarifa zinaeleza kuwa Wananchi hao wameridhia kutoa ardhi hiyo kwa lengo la kuchocheza maendeleo ya kijiji hicho. Msosa Said ambaye ndiye Mwekezaji ndani ya kijiji hicho anaeleza kuwa baada ya kukubaliwa kuwekeza katika eneo hilo Wanakijiji watanufaika kwa kupata elimu ya kilimo biashara, Watapata ajira na kufanya biashara.

Waziri Pinda anaeleza kuwa Wizara imeshakaa na Mwekezaji huyo na kwa kuanzia watampa hati ya awali (hati ya kimila).

Source: ITV habari

My take: Je, na wao wamemuuzia muwekezaji, au wamenunuliwa..?

Tujadili kwa hoja sio matusi
 
Jaman lindi pabaya....hasalindi mjini, Kuna maeneo unawaza utaishije pale, yaan maisha magumu sana hasa kwa wanawake Lindi, kwa umri Mimi dada yenu kikongwe....Lindi mjini mwaka 2100 itaifikia Arumeru ya 1990
 
Jaman lindi pabaya....hasalindi mjini, Kuna maeneo unawaza utaishije pale, yaan maisha magumu sana hasa kwa wanawake Lindi, kwa umri Mimi dada yenu kikongwe....Lindi mjini mwaka 2100 itaifikia Arumeru ya 1990
Unaifananisha LINDI na Arusha(Arumeru) ambapo kila mwaka serikali hupeleka huko miradi ya serikali na kujenga majengo ya taasisi mbali mbali.Tumia akili yako vizuri.
 
Jaman lindi pabaya....hasalindi mjini, Kuna maeneo unawaza utaishije pale, yaan maisha magumu sana hasa kwa wanawake Lindi, kwa umri Mimi dada yenu kikongwe....Lindi mjini mwaka 2100 itaifikia Arumeru ya 1990
Lindi ni mkoa unaokua kwa kasi, ukiona muwekezaji ujue mahali salama
 
Viongozi wa ccm walisema mradi wa ges ukianza mji wa lindi utakua ni mji wa kisasa.

Huyo muwekezaji ni muarabu ama?
 
Back
Top Bottom