Wakazi wa Dar wao wamezoea kuona wenzao wa mikoa mingine wakiandamana na kupigwa mabomu kwa kutetea haki zao. Wakazi wa Dar wanawacheka na kuwadharau. Wakati Dar ndio tuseme mji mkuu kwa Tanganyika yaani kwa kuwa na wakazi wengi wao ndio walitakiwa wawe wa kwanza katika chachu ya maendeleo. Matokeo yake Dar wanaongoza kwa Starehe utafikiri ndio Sodoma na Gomora, Hawajali. Mikoa mingine inaandamana kwa ajili ya wezi/Mafisadi ambao hata hawa2jui lakini kutona na uchungu wa nchi yao wako radhi kutoa maisha yao. Dar ndio Mafisadi wote wanaishi na wanapishana nao lakini wako kimya na kuwashangilia. Nilitegemea kuwa maendeleo yataanzia dar kumbe hakuna kitu wamebakia kushabikia wenzao mikoani wanavyotwangwa virungu. Maendeleo, mapinduzi mara nyingi huletwa na miji mikuu. Lakini kwa Dar hakuna. Acha wanywe maji ndio watajua kuwa kumbe zinatakiwa mifereji. Viongozi serikalini wao wanajua inapotokea majanga kwao ni deal kwa misaada ukusanywa lakini matokeo yake wala hatujui zilitumikaje, na hata kama walengwa walipata. Kwani hatujawai kusikia tukipewa matumizi jinsi michango ilivyotumika baada ya majanga. Inabidi wakazi wa Dar kuamka sasa.