Ndetirima
JF-Expert Member
- Oct 4, 2011
- 1,008
- 784
Propaganda za kuelekea uchaguzi mkuu wa 2015 kuna mengi yatajitokeza. Mi nakushauri kijana kama unatafuta umaarufu kwa kupitia marehemu ujue unajitafutia matatizo, fanya kazi za halali ujipatie kipato cha halali na Mungu atakulinda na kukubariki vinginevyo Mungu atakuacha uangamie. Jeshi la Polisi lilishafanya kazi yake na kumaliza na wewe kutoa ushahidi wako, kama ulidanganya na kuficha ukweli inamaana wewe ulihusika moja kwa moja na kifo cha marehemu Wangwe kwa hiyo adhabu uliyopewa ya uzembe haikustahili bali ulitakiwa ushitakiwe kwa kuua kwa kukusudia na adhabu yake iwe ni kunyongwa mpaka ufe.