Wakati umefika wa kutumia Kiswahili kama lugha ya kufundishia

Mwanafalsafa

Platinum Member
Jun 24, 2007
662
851
Nimepitia matokeo ya NECTA kidato cha pili na kugundua jambo lifuatalo.

Shule za Kata zina ufaulu hafifu sana (mwingi ni wa daraja F) katika masomo yote isipokuwa somo la Kiswahili. Somo la Kiswahili ndo limezibeba shule za kata zisitumbukie shimoni kabisa.

Mifano michache ni hii hapa (ikiwemo shule ya Mburahati ambayo imevuma hapa JF kwa jinsi ilivyopata sifuri nyingi):

323779606_698245588689978_4510308771840051701_n.jpg

324193560_2400184843479780_1612401865335268357_n.jpg

324190579_1593813264380472_595721074968337409_n.jpg

323434706_542115801219215_4641989480315909996_n.jpg

324927454_1260729894484863_7300559445759523903_n.jpg


Hii maana yake nini?
Hii maana yake ni kwamba Kiswahili kinaeleweka vizuri zaidi. Wanaosoma shule za kata mara nyingi ni watoto wa maskini ambao elimu ya msingi waliipata kwenye shule za serikali ambazo huwa zinatumia Kiswahili. Kwa hiyo wanapoingia kidato cha kwanza wanakutana na Kiingereza kinawasumbua.

Ila utafiti zaidi unahitajika ili kujua ufaulu wao ulikuwaje kwenye shule za msingi walikotoka ambako walikuwa wanatumia Kiswahili.

Wazazi maskini hawana hata bajeti za kuwalipia watoto hawa wakasome masomo ya ziada ya Kiingereza (yaani "twisheni" au "English course"). Kwenye hizi shule ndo kuna watoto wa wale akina mama wanaolea peke yao, ambao wanatembeza mabeseni ya matunda na mihogo mibichi barabarani kutafuta pesa.

Kwa wale wanaosemaga kwamba maarifa mengi yako kwa Kiingereza, jibu ni kwamba Kiingereza kinatafsirika. Lakini tusijidharau na lugha yetu ya Kiswahili hata siku moja. Hakuna jamii iliyoweza kupiga hatua kwa kujidharau.

Hata hao Waingereza wenyewe walikuwa koloni la Ufaransa na walikuwa wanatumia Kifaransa kama lugha rasmi ya serikali na sheria.

Lakini mambo makubwa walianza kuyafanya walipoachana na Kifaransa (ambacho walikitumia kwa miaka 700) na kukumbatia Kiingereza kama lugha ya serikali na ya sheria.
 
Je huko primary mbona ufaulu wao bado ni hafifu na wanatumia Kiswahili?

Mkuu Jambo la kwanza unabidi ufahamu kuwa shule za kata zimezidiwa na idadi ya wanafunzi

Mfano Temeke secondary Kuna wanafunzi 1200+ na waalimu wapo 10 tu sasa hapo hata wakitumia Kiswahili watatobowaje?

Then shule kukosa miondombinu Bora Kama Wanafunzi 100+ kukaa darasa moja.

Pia maadili sifuri umalaya umekita mizizi achilia mbali uvutaji wa bangi kwa vijana wa kiume.
 
Nilikuwa nafikiria tu wachina wao wanafundishiwa na lugha zao mama na wakipata ajira nje za nchi zao wanafanya kazi kulingana na mafundisho ya lugha za nchi yao na wanapata mafanikio makubwa sana katika kazi zao!!

English ifundishwe ila isitumike katika kufundishia kila somo,

Watakuja wapitishe kiswahili nacho kifundishwe kwa kingereza, kwani nchi haina lugha yake???

Kujua kingereza vizuri sio kipimo cha kuwa unajua kufanya kazi yako kwa usahihi kingereza ni lugha tu ya kuwasiliana.
 
Kweli Mkuu Tena Kuanzia chini kabisa
Mtoa Mada anataka kuwaangamiza vijana ambao hawana hatia

Sijui amewahi kufika shule za kata akaona hali ilivyo
Katika hizo shule nilizozitolea mfano nimeshawahi kuishi jirani na shule za Makamba, Turiani na Makoka. Ziko vizuri. Hazina msongamano wa wanafunzi, hazina uhaba wa walimu, zina umeme, zina maabara na hiyo ya Turiani ina mpaka maabara ya kompyuta.

Lugha yetu sisi ni Kiswahili. Sasa hivi tumeshapitisha kwamba hata lugha ya kisheria ni Kiswahili.

Najua kwa ambao tumeshasoma na kuhitimu kwa kutumia Kiingereza tunaweza kuona ni ngumu sana. Lakini shule ya msingi mie nilisoma kwa Kiswahili na ndo maana nina uhakika Kiswahili kinaweza kutumika kama lugha ya kufundishia.

Tatizo letu ni ushamba tu wa kumuabudu mzungu. Watu wa Asia (China na Japan na Korea) mbona wanaelimisha watu wao na wanafanya mambo makubwa kwa kutumia lugha zao.
 
Katika hizo shule nilizozitolea mfano nimeshawahi kuishi jirani na shule za Makamba, Turiani na Makoka. Ziko vizuri. Hazina msongamano wa wanafunzi, hazina uhaba wa walimu, zina umeme, zina maabara na hiyo ya Turiani ina mpaka maabara ya kompyuta.

Lugha yetu sisi ni Kiswahili. Sasa hivi tumeshapitisha kwamba hata lugha ya kisheria ni Kiswahili.

Najua kwa ambao tumeshasoma na kuhitimu kwa kutumia Kiingereza tunaweza kuona ni ngumu sana. Lakini shule ya msingi mie nilisoma kwa Kiswahili na ndo maana nina uhakika Kiswahili kinaweza kutumika kama lugha ya kufundishia.

Tatizo letu ni ushamba tu wa kumuabudu mzungu. Watu wa Asia (China na Japan na Korea) mbona wanaelimisha watu wao na wanafanya mambo makubwa kwa kutumia lugha zao.
Mkuu hilo Jambo , haliwezekani .

Nyie mbona watoto wenu mnawapeleka shule nzuri zenye kila kitu . Then mnaleta siasa katika shule za dumu Fagio.
 
Mchawi ni lugha kuanzia awali...

Mtaala wa lugha ya kiingereza shule za awali serikali ilichemka, haueleweki kabisa..
 
Kuna kitabu ameandika Galabawa na wenzake(Galabawa et ell)1986.Kinaitwa Language cross in teaching.kimejadili hili kwa urefu na mapana yake.Tatizo wa TZ tunachelewa kuamua.
 
Miaka ya 90 kupata A ya Kiswahili ilikuwa muujiza! Tulikuwa tunapiga A za physics, chemistry, mathematics lakini sio Kiswahili. Nashangaa sana kwamba siku hizi A ya Kiswahili ndio rahisi zaidi! Nikwambie tu hata ufundishaji uwe kwa lugha ipi, kusukuma, kihehe, kimasai,etc tatizo sio lugha ya kufundishia bali mfumo mzima wa elimu. Tena kama tunataka elimu yetu na wasomi wetu wawe dhaifu zaidi ndani na nje ya nchi basi tudharau lugha ya kiingereza.

Usiseme mbona wachina, wajapani, wakorea, wameweza? Ndio ni kwa mamia ya miaka na hata hivyo mwisho wa siku wanajifunza kiingereza vizuri sana ili kupata yale ya kimagharibi. Pia hayo ni mataifa yenye kujiweza tangu enzi za kale.
Nimepitia matokeo ya NECTA kidato cha pili na kugundua jambo lifuatalo.

Shule za Kata zina ufaulu hafifu sana (mwingi ni wa daraja F) katika masomo yote isipokuwa somo la Kiswahili. Somo la Kiswahili ndo limezibeba shule za kata zisitumbukie shimoni kabisa.

Mifano michache ni hii hapa (ikiwemo shule ya Mburahati ambayo imevuma hapa JF kwa jinsi ilivyopata sifuri nyingi):

323779606_698245588689978_4510308771840051701_n.jpg

324193560_2400184843479780_1612401865335268357_n.jpg

324190579_1593813264380472_595721074968337409_n.jpg

323434706_542115801219215_4641989480315909996_n.jpg

324927454_1260729894484863_7300559445759523903_n.jpg


Hii maana yake nini?
Hii maana yake ni kwamba Kiswahili kinaeleweka vizuri zaidi. Wanaosoma shule za kata mara nyingi ni watoto wa maskini ambao elimu ya msingi waliipata kwenye shule za serikali ambazo huwa zinatumia Kiswahili. Kwa hiyo wanapoingia kidato cha kwanza wanakutana na Kiingereza kinawasumbua.

Ila utafiti zaidi unahitajika ili kujua ufaulu wao ulikuwaje kwenye shule za msingi walikotoka ambako walikuwa wanatumia Kiswahili.

Wazazi maskini hawana hata bajeti za kuwalipia watoto hawa wakasome masomo ya ziada ya Kiingereza (yaani "twisheni" au "English course"). Kwenye hizi shule ndo kuna watoto wa wale akina mama wanaolea peke yao, ambao wanatembeza mabeseni ya matunda na mihogo mibichi barabarani kutafuta pesa.

Kwa wale wanaosemaga kwamba maarifa mengi yako kwa Kiingereza, jibu ni kwamba Kiingereza kinatafsirika. Lakini tusijidharau na lugha yetu ya Kiswahili hata siku moja. Hakuna jamii iliyoweza kupiga hatua kwa kujidharau.

Hata hao Waingereza wenyewe walikuwa koloni la Ufaransa na walikuwa wanatumia Kifaransa kama lugha rasmi ya serikali na sheria.

Lakini mambo makubwa walianza kuyafanya walipoachana na Kifaransa (ambacho walikitumia kwa miaka 700) na kukumbatia Kiingereza kama lugha ya serikali na ya sheria.
ia ya 90
 
Siku nikisikia kauli dhabiti kuwa, tuna tatizo kubwa la upungufu wa Waalimu wa SAIYANSI nitajua tumekusudia kuikomboa elimu yetu na kufanya watoto wafaulu zaidi. Hii ni pamoja na kuajiri waalimu kwa ajili ya kufundisha somo la HESABU katika shule za msingi na kuachana na dhana kuwa, kila mwalimu anaweza kufundisha Hesabu!
Watoto wanafeli kwa kukosa msingi mzuri hasa kwenye Saiyansi, tatizo sio Lugha!
 
wanajifunza kiingereza vizuri sana ili kupata yale ya kimagharibi
Nafikiri unaelewa kuwa wote tunaosemaga "Kiswahili iwe lugha ya kufundishia" hatusemi kuwa "Kiingereza kisifundishwe nchini Tanzania".

Kiingereza kiendelee kufundishwa kama lugha ya kigeni.

Hii akili ya kutukuza Kiingereza sijui mnaitoa wapi waTanzania wa aina yako? Ni dalili mbaya sana ya utumwa wa kifikra.

Hao waingereza wenyewe walitawaliwa na wafaransa kwa miaka 700, walikuwa wanatumia kifaransa kama lugha rasmi ya sheria, lakini baadae wakaachana nacho na kukienzi Kiingereza.

Kuhusu kujiweza hata sisi tulikuwa tunajiweza. Ni ujinga tuliopandikiziwa na wageni wakoloni ndo umesababisha watu wa ardhi hii kudhani kwamba hatuwezi kusimama wenyewe bila ya kuwategemea wazungu. Ni utumwa mbaya sana wa kifikra.

Mabadiliko yameanza. Kwenye kada ya sheria sasa hivi Kiswahili kinazidi kusonga mbele. Bunge limeshaanza kuandika sheria kwa Kiswahili. Na Mahakama za juu zimeshaanza kutumia Kiswahili. Na katika watu waliokuwa wanaona Kiswahili hakiwezekani ni wanasheria, maana wao ndo huwa wanafundishwa kwa Kiingereza kigumu. Ila wanasheria wengi hawajui kwamba hata hao waingereza wanaowaabudu sasa hivi kuna wakati walikuwa wanatumia kifaransa kama lugha yao ya sheria.

Jiamini mkuu. Hakuna kitu kizuri kama kujiamini.

Yaani ushindwe kutengeneza ndege, na maneno nayo pia ushindwe kutengeneza? Kwamba akili yako hata kutengeneza maneno tu ishindwe utegemee maneno yaliyotengenezwa na mwingereza?
 
Huenda hata kwa wenzetu Ulaya, watoto wanafaulu sana somo la kiingereza, maana ni lugha yao ya mawasiliano!
 
Na isihi serikali na watu wote. watoto wajifunze kiingereza tangu nasari aisee tena kile cha ukweli huko huko Kenda kenda. Watoto wafundishwe kujiamini achana na hiz rubbish tafiti za maprof wa chuo hapo. Mnasababisha watu wanakosa kazi huko dunian kwa kujifunza lugha za humuhumu tu na hamuwez kuwapa ajira. Achen huu ujinga jombaa. Watoto wako watatawaliwa milele wao watoto wao wapo huko fweza halafu wanakuambia wakwako wakomae na kiswahili wanakosa exposure. vitu vingi vya ukweli viko vitabuni ambavyo hawajavitasiri kuja kwenye kiswahili. Sasa watajuaje ya dunia. Hii nchi inaungese mwingi sana
 
una walimu wa kutosha

una msingi imara wa lugha ya kiingereza .

unavitendea kazi vya kufanya watoto wajifunze kirahisi kiingereza.

soko la ushindani duniani linaitaji vitu vipi
Mwanzo mgumu walimu sio zero kabisa kwamba hWana kitu kidogo kidogo wanajua na ndo kingereza kwa level ya msingi.

Wapo watoto wamefundishwa na walimu wa kwaida baadae wakaimprove kwa kujitafutia.

Hata walimu wapige cha ugoko ila katika earlier stage wanafunzi ni rahisi kuadapt lugha la kwanza mpaka la Saba wanakuwa na kitu kichwani.

Tunaweza kuanza hata leo na walimu wale wale naamini tutafika.
 
Lugha ya kiswahili haijitoshelezi kutumika kufundishia hususani masomo ya sayansi
 
Kama bajet inategemea hela kwa waingereza usidhani kwamba watakubali msome kwa kiswahili,Tena sasa hivi ndio Kuna mkazo watoto wazungumze kiingereza shuleni,na walimu hakuna kuingea kiswahili,hata mgeni aje skuli
 
Back
Top Bottom