Wajumbe tume ya katiba hawajapata barua zao hadi sasa, wengi hawajajiuzulu kazi zao

Mikael Aweda

JF-Expert Member
Dec 17, 2010
2,973
3,901
Wakuu mpaka leo, pamoja na kuwa wajumbe wa tume ya katiba wameshaapishwa bado hawajapewa mkataba(barua) itakayowapa ujasiri wa kuacha ajira zao ili waanze kazi hiyo mpya waliyopewa na JK mwanahalisi linaripoti.
Gazeti linadai pia kuwa hadi leo tarehe 2 may wajumbe hawajawahi kukaa kikao cho chote cha maandalizi ya kazi hii nzito na muhimu kwa ajili ya mustakabali wa nchi yetu.
Jambo hili inakwenda kinyume na kauli ya Rais kuwa tumeamua kuwaapisha mapema zaidi (badala 30 april) ili wajiandae kuacha kazi zao mapema.
Mmoja wa wajumbe wa tume hiyo aliongea na mwanahalisi alisema, tangu tuapishwe hatukuwa na mawasiliano na Serikali wa mkiti wetu (Warioba)
Warioba alitumiwa msg ktk simu yake na mwanahalisi lakini hakujibu kabisa.
Kabla ya kutumiwa msg, gazeti linadai kuwa alipigiwa simu na kuwajibu kuwa yuko ktk kikao cha ccm (yeye ni balozi wa Nyumba kumi) na akawaambia hawezi kuongea kwa kuwa wako ktk uchaguzi.

My take;
Ninaanza kuelewa hoja na msimamo wa Mwanakijiji kuhusu katiba mpya ninaousoma magazetini na JF.
 
Wakuu mpaka leo, pamoja na kuwa wajumbe wa tume ya katiba wameshaapishwa bado hawajapewa mkataba(barua) itakayowapa ujasiri wa kuacha ajira zao ili waanze kazi hiyo mpya waliyopewa na JK mwanahalisi linaripoti.
Gazeti linadai pia kuwa hadi leo tarehe 2 may wajumbe hawajawahi kukaa kikao cho chote cha maandalizi ya kazi hii nzito na muhimu kwa ajili ya mustakabali wa nchi yetu.
Jambo hili inakwenda kinyume na kauli ya Rais kuwa tumeamua kuwaapisha mapema zaidi (badala 30 april) ili wajiandae kuacha kazi zao mapema.
Mmoja wa wajumbe wa tume hiyo aliongea na mwanahalisi alisema, tangu tuapishwe hatukuwa na mawasiliano na Serikali wa mkiti wetu (Warioba)
Warioba alitumiwa msg ktk simu yake na mwanahalisi lakini hakujibu kabisa.
Kabla ya kutumiwa msg, gazeti linadai kuwa alipigiwa simu na kuwajibu kuwa yuko ktk kikao cha ccm (yeye ni balozi wa Nyumba kumi) na akawaambia hawezi kuongea kwa kuwa wako ktk uchaguzi.

My take;
Ninaanza kuelewa hoja na msimamo wa Mwanakijiji kuhusu katiba mpya ninaousoma magazetini na JF.


Mkuu, nadhani wanasubiri Fungu, nijuavyo serikali imefulia
 
Mkuu, nadhani wanasubiri Fungu, nijuavyo serikali imefulia


If that is the case, tunahitaji kufikiri upya kama taifa kama tutafika 2015 salama, achilia mbali kuwa na au kutokuwa na katiba mpya.
 
Nakumbuka waliiambiwa kuwa wataanza kazi mwezi huu , na ndio kwanza watu wanatoka kwenye Mei Mosi, wengine wapo kwenye matayarisho ya budget.

Hivi lakini kwanini waache kazi , hapo mbona sijafahamu, kwani hii si ni kazi ya muda tu. nahisi wangeeomba likizo tu kwa manufaa ya TAIFA
 
Back
Top Bottom