Nchi yetu iko katika hatari kubwa ya kuingia katika machafuko ya kidini yanayotokana na kufumbiwa macho chokochoko za kidini ambazo zimeanza muda mrefu sasa. Uvumilivu miongoni mwa waumini wa dini kuu chini yaani uislamu na ukristo ambao umekuwepo nchini toka uhuru sasa unatoweka kwa kasi ya ajabu.
Nimesoma kinachoitwa "waraka wa waislamu" nimeweka inverted commas kwa sababu sikubaliani kabisa na title hiyo. Kilichomo ndani ya waraka huo hakina sifa ya kuitwa waraka wa waislamu kwani ni dhihaka na tusi kubwa kwa waislamu wengi ambao ni wastaarabu, wastahimilivu na wasomi. waraka umejaa ujinga mtupu ukisherehesha na matukio ya kubuni ya uongo na ya kiwango cha chini sana ndiyo maana nasema haustahili kuitwa waraka wa waislamu, ungefaa kuitwa "waraka wa ponda kwa waislamu ambao ni wajinga"
Waraka unajaribu kutuaminisha kuwa Mhe Hadji Mponda na Mhe. Mustapha Mkullo walipoteza nafasi zao za uwaziri kwa shinikizo la wakristo bila kujali tuhuma mbalimbali zilizoelekezwa kwao ikiwamo ubadhirifu na kushindwa kumudu majukumu yao. Tunafahamu Mhe Mponda alishindwa kushughulikia ipasavyo mgogoro wa madaktari na serikali, pia ili lazimu awajibike kwakuwa MSD iliyo chini ya wizara yake ililitia hasara taifa la zaidi ya shs 5bilioni kwa kusababisha dawa zenye thamani ya pesa hiyo kuharibika kwa kufikia mwisho wa muda wake wa matumizi(expiry) bila kuzisambaza mahospitalini ambako zilikuwa zikihitajika sana na wagonjwa wakifariki kwa kuzikosa dawa hizo. Pamoja na Mhe Mponda mwingine aliyewajibika katika hili ni Mhe Dr Lucy Nkya aliyekuwa naibu waziri, lakini waraka haumtaji kwa kuwa ni mkristo hivyo hoja ya udini inayojengwa itavurugika.
Mhe Mkulo pamoja na kushindwa kabisa majukumu yake kama waziri wa fedha alikuwa na tuhuma za kuuza kinyemela kwa kampuni ya METL kiwanja mali ya PSRC. Pia Mkulo alishinikiza kuvunjwa kwa taasisi ya CONSOLIDATED HOLDING LIMITED na kuhamishiwa shughuli zake kwa msajili wa hazina. Hapa lengo lilikuwa ni kuwalinda wadaiwa sugu ambao bado hawajamaliza kulipa madeni yatokanayo na ununuzi wa mashirika ya umma. CHL ni mrithi wa iliyokuwa ikiitwa PSRC. Mhe Zitto Kabwe ndiye aliyeibua sakata hili lakini waraka haumtaji kwakuwa ni muislamu ili kujenga dhana kuwa Mkullo aling'olewa kwa shinikizo la wakristo.
Waraka una maelezo marefu lakini yasiyoeleweka juu ya chadema kuwa chama cha kikristo ambacho waislamu tumetakiwa kujiepusha nacho bila kutueleza na kutuelekeza chama cha kukiunga mkono ambacho bila shaka ni cha kiislamu. Jambo lingine ni mali nyingi zinazomilikiwa na makanisa kuwa eti imewezeshwa na mfumo kristo uliopo nchini. Nasema huu ni ujinga na uongo wa mchana kweupe kwani taasisi za kikristo toka kabla ya uhuru pamoja na kuandaa waumini wao kiroho hazipata kuwa nyuma katika kushughulikia huduma za kijamii kwa waumini wao pamoja na wasiokuwa wakristo. Wakristo walimiliki shule na hospitali nyingi ambazo zimehudumia watanzania wote bila ubaguzi. Baba yabgu mzazi ambaye ni mwislamu alisoma katika shule za kikristo yaani st mary na st andrews. Shukrani za pekee kwa baba wa taifa(mkristo) ambaye alitaifisha shule za kanisa ili kuwezesha waislamu kusoma katika shule hizo, pamoja na hatua hiyo ya kizalendo kuna waislamu wenzetu ambao wanamdhihaki mzee huyo kwa udini, huku ni kukosa shukrani kwa kiwango cha juu sana.
Najiuliza bila hatua hiyo ya Nyerere wazee wetu wa kiislamu wangesoma wapi ilhali Mazengo sec schoo, Mkwawa sec. school, Tosamaganga, Musoma alliance, Pugu, Minaki, Malangali, Rugambwa, Forodhani zilikuwa mali ya madhehebu ya kikristo. Narudia kuandika tena kuwa waraka huu ni janga na ni kielelezo kuwa waislamu bado tunasafari ndefu ya kuutokomeza ujinga kama wanaojiita viongozi wetu wa uislamu wanaweza kuandika waraka muflisi kama huu.
NAWASILISHA
Nimesoma kinachoitwa "waraka wa waislamu" nimeweka inverted commas kwa sababu sikubaliani kabisa na title hiyo. Kilichomo ndani ya waraka huo hakina sifa ya kuitwa waraka wa waislamu kwani ni dhihaka na tusi kubwa kwa waislamu wengi ambao ni wastaarabu, wastahimilivu na wasomi. waraka umejaa ujinga mtupu ukisherehesha na matukio ya kubuni ya uongo na ya kiwango cha chini sana ndiyo maana nasema haustahili kuitwa waraka wa waislamu, ungefaa kuitwa "waraka wa ponda kwa waislamu ambao ni wajinga"
Waraka unajaribu kutuaminisha kuwa Mhe Hadji Mponda na Mhe. Mustapha Mkullo walipoteza nafasi zao za uwaziri kwa shinikizo la wakristo bila kujali tuhuma mbalimbali zilizoelekezwa kwao ikiwamo ubadhirifu na kushindwa kumudu majukumu yao. Tunafahamu Mhe Mponda alishindwa kushughulikia ipasavyo mgogoro wa madaktari na serikali, pia ili lazimu awajibike kwakuwa MSD iliyo chini ya wizara yake ililitia hasara taifa la zaidi ya shs 5bilioni kwa kusababisha dawa zenye thamani ya pesa hiyo kuharibika kwa kufikia mwisho wa muda wake wa matumizi(expiry) bila kuzisambaza mahospitalini ambako zilikuwa zikihitajika sana na wagonjwa wakifariki kwa kuzikosa dawa hizo. Pamoja na Mhe Mponda mwingine aliyewajibika katika hili ni Mhe Dr Lucy Nkya aliyekuwa naibu waziri, lakini waraka haumtaji kwa kuwa ni mkristo hivyo hoja ya udini inayojengwa itavurugika.
Mhe Mkulo pamoja na kushindwa kabisa majukumu yake kama waziri wa fedha alikuwa na tuhuma za kuuza kinyemela kwa kampuni ya METL kiwanja mali ya PSRC. Pia Mkulo alishinikiza kuvunjwa kwa taasisi ya CONSOLIDATED HOLDING LIMITED na kuhamishiwa shughuli zake kwa msajili wa hazina. Hapa lengo lilikuwa ni kuwalinda wadaiwa sugu ambao bado hawajamaliza kulipa madeni yatokanayo na ununuzi wa mashirika ya umma. CHL ni mrithi wa iliyokuwa ikiitwa PSRC. Mhe Zitto Kabwe ndiye aliyeibua sakata hili lakini waraka haumtaji kwakuwa ni muislamu ili kujenga dhana kuwa Mkullo aling'olewa kwa shinikizo la wakristo.
Waraka una maelezo marefu lakini yasiyoeleweka juu ya chadema kuwa chama cha kikristo ambacho waislamu tumetakiwa kujiepusha nacho bila kutueleza na kutuelekeza chama cha kukiunga mkono ambacho bila shaka ni cha kiislamu. Jambo lingine ni mali nyingi zinazomilikiwa na makanisa kuwa eti imewezeshwa na mfumo kristo uliopo nchini. Nasema huu ni ujinga na uongo wa mchana kweupe kwani taasisi za kikristo toka kabla ya uhuru pamoja na kuandaa waumini wao kiroho hazipata kuwa nyuma katika kushughulikia huduma za kijamii kwa waumini wao pamoja na wasiokuwa wakristo. Wakristo walimiliki shule na hospitali nyingi ambazo zimehudumia watanzania wote bila ubaguzi. Baba yabgu mzazi ambaye ni mwislamu alisoma katika shule za kikristo yaani st mary na st andrews. Shukrani za pekee kwa baba wa taifa(mkristo) ambaye alitaifisha shule za kanisa ili kuwezesha waislamu kusoma katika shule hizo, pamoja na hatua hiyo ya kizalendo kuna waislamu wenzetu ambao wanamdhihaki mzee huyo kwa udini, huku ni kukosa shukrani kwa kiwango cha juu sana.
Najiuliza bila hatua hiyo ya Nyerere wazee wetu wa kiislamu wangesoma wapi ilhali Mazengo sec schoo, Mkwawa sec. school, Tosamaganga, Musoma alliance, Pugu, Minaki, Malangali, Rugambwa, Forodhani zilikuwa mali ya madhehebu ya kikristo. Narudia kuandika tena kuwa waraka huu ni janga na ni kielelezo kuwa waislamu bado tunasafari ndefu ya kuutokomeza ujinga kama wanaojiita viongozi wetu wa uislamu wanaweza kuandika waraka muflisi kama huu.
NAWASILISHA