Waislam wa Tanzania na tatizo la udini katika Wizara ya Elimu

Mohamed Said

JF-Expert Member
Nov 2, 2008
20,922
30,271
UM5d4OfKGZAOGzoyOL2k5ofU7gKUq8up-rSPW94rWq1CU0oly4DuZx0nhqPDBRsHV1Y1-QwcV7s6cEfgbDES2YV1DERqomujIb8mhJE0ThZ38ztuIb7yN3F-JAIBLHNYQ-ZS95Gsgnt3ftui-8GfkgJ1U7JyLXPmpYiUd0m7o1FtBE_QkdyKIHzyiqHeZKffKBAnnGXheHLdhvU0FaGpK9clckpP1nq9L1Q95c_d_t0X_Usrdu0FFRv3dAES0GmlBUD_sRVoUBfiJrkIzDJ1RSLnYHhm6ZJlotJWcHhOesANLUPU3pErqJRACQkqIjrU1ZeUosCWXHzwxciZB2kqvbxbC2dXxeWquDhnvP7F1hgeGqld21AEp4bFHUu-DiZeMNpIwWkW9IVkWSqXTQTW1ToO1PqqSozdgk2BBWPBZILvEmedz2-3Qi9R3Andwtl-xxxU2e9Jp4PbiVvlgJhkzzr2PH-hRg4gxEe64ogHNac_vJZbOj98n_dKdKuQVZKOsSovFVnXp18c5bGYKCwq--ISKgPCAbeQAZPbbXpGSQ4tpWL91wZOniRFzxcedUjRd6Bx=w480-h320-no

Maandamano ya Waislam Dhidi ya NECTA Chini ya Dr. Joyce Ndalichako
Ndugu Waziri,

Kwa muda mrefu sasa, kumekuwa na maswali mengi wakijiuliza Waislamu, moja likiwa inakuwaje katika maeneo yenye Waislamu wengi ambapo idadi ya wanafunzi Waislamu inakuwa zaidi ya asilimia 70, lakini wanapochaguliwa kwenda sekondari, idadi ya watoto wa Kiislamu huporomoka na kuwa chini ya asilimia 20.

Swali na kitendawili hiki kimekuwepo kwa muda mrefu bila kupatiwa majibu. Hata lilipofikishwa Bungeni mwaka 1999 na aliyekuwa Mbunge wa Kigamboni, Mzee Kitwana Selemani Kondo, bado halikupatiwa jibu.

Akihoji juu hali hiyo, Mzee Kitwana Kondo alitoa mfano jinsi hali ilivyokuwa katika shule ya Pembamnazi iliyokuwa na Waislamu watupu na kwa miaka mingi mfululizo kulikuwa hakuna hata mtoto mmoja aliyekuwa akichaguliwa kwenda sekondari kutoka katika shule hiyo. Aidha alisema kuwa, katika mkoa wa Dar es Salaam na Pwani, takwimu zinaonyesha kuwa idadi ya watoto wa Kiislamu katika shule za msingi ilikuwa zaidi ya asilimia 70 lakini inapokuja kuchaguliwa kwenda sekondari, idadi ya Waislamu iliporomoka na kuwa chini ya asilimia 20.

Akizungumza Bungeni tarehe 2 Februari, 1999 alisema kuwa katika watoto waliofanya mtihani wa darasa la saba mwaka 1998, idadi ya Waislamu ilikuwa asilimia 71 na Wakristo 29%. Hata hivyo akasema, ilipotoka orodha ya waliochaguliwa kwenda sekondari, idadi ya Wakristo ikawa asilimia 79 (79%) na Waislamu 21%.

Je, hiyo ilikuwa na maana kuwa watoto wa Kiislamu kwa asili yao hawana akili? Alitaka kujua Mzee Kitwana Kondo. Lakini hakuweza kupata jibu.

Mheshimiwa Waziri,
Ni wazi kuwa Waziri wa Elimu au Waziri Mkuu ambaye ndiye msimamizi wa mambo ya serikali Bungeni asingeweza kutoa majibu ya uhakika kwa sababu swali lilihitaji kufanyika uchunguzi huru wa kina na makini kwanza.

Mheshimiwa Waziri,
Mwaka 1987 aliyekuwa Waziri wa Elimu, Profesa Kighoma Ali Malima, aliweka utaratibu mpya wa ufanyaji wa mtihani wa darasa la saba ambapo namba zilitumika toka kufanya mtihani, kusahihisha na kuchagua wanafunzi wa kwenda kidato cha kwanza. Namba zilivishwa majina baada ya taratibu zote hizo kukamilika. Mwaka huo idadi ya watoto wa Kiislamu waliokwenda kidato cha kwanza iliongezeka kwa asilimia 40 ikilinganishwa na miaka ya nyuma.

Hata hivyo, mara aliondolewa Waziri Malima katika wizara hiyo na utaratibu wa zamani ukarejeshwa ambapo yalikuwa yakichaguliwa majina na idadi ya Waislamu ikaporomoka na kurudi chini ya asilimia 20.

Mheshimiwa Waziri,
Hali kama hii hapana shaka inazua maswali mengi ambayo yanahitaji majibu na majibu hayo hayawezi kupatikana bila ya kufanyika uchunguzi.

Labda tuongeze mifano ili kuliweka wazi zaidi jambo hili. Mwaka 1983 mwanafunzi aliyekuwa akiitwa Kopa Abdallah akisoma katika shule ya msingi Kichangani, Kilosa, alikosa kuchaguliwa kwenda sekondari. Yeye binafsi, wazazi wake na hata walimu wake hawakuamini matokeo yale kutokana na alivyokuwa akifanya vizuri kuliko wanafunzi wote. Baadae ilikuja kugundulika kuwa nafasi yake alipewa mwanafunzi aliyekuwa akiitwa Antoni Samirani ambaye alikuwa na uwezo mdogo sana ikilinganiswa na Abdallah. Kilichofanyika ni kuwa jina la Abdallah lilifichwa na baadae Antoni akapewa jina hilo kimya kimya na kwenda kusoma sekondari akitumia jina Abdallah wakati yeye ni Antoni.

Taarifa zinasema kuwa Kopa Abdallah alipogundua hakuweza kufanya kitu akaishia kuwa dereva.

Hali kama hiyo ilimkuta pia Adam Ramadhani aliyekuwa akisoma shule ya msingi Rutihinda jijini Dar es Salaam na kumaliza darasa la saba mwaka 1999. Yalipotoka matokeo ya mtihani wa darasa la saba na kuonekana kuwa Adam hakuchaguliwa, baba yake hakuamini kuwa mtoto wake anaweza kufeli kutokana na uwezo aliokuwa nao na zaidi akitizama walivyochaguliwa watoto ambao Adam alikuwa mwalimu wao shuleni na mitaani.

Katika kufuatilia suala hilo wizarani, ilikuwa aibu kwa wizara baada ya kuonekana kuwa walichaguliwa watoto wa Kikristo wenye alama za chini kabisa huku akiachwa Adam Ramadhani aliyekuwa na alama za juu kuliko wote.

Mheshimiwa Waziri,
Mifano kama hii ni mingi mno na ipo katika ngazi zote kwa maana kutoka elimu ya msingi kwenda sekondari, kutoka kidato cha nne kwenda kidato cha tano na kutoka kidato cha sita kwenda Chuo Kikuu. Kwamba hata kutoka kidato cha nne kwenda kidato cha tano, wapo watu waliopata kushuhudia majina ya wanafunzi wa Kiislamu yakiwekwa pembeni japo walikuwa na sifa za kuchaguliwa.

Mheshimiwa Waziri,
Ukiacha hujuma katika kuwaacha wanafunzi Waislamu wenye sifa kuendelea na masomo, matatizo huanzia kwenye kuamua nani amefaulu na nani kafeli. Tuhuma zilizopo ni kuwa wapo wanafunzi wanapewa madaraja ya juu wakati alama zao ni za chini na wapo wanaopewa madaraja ya chini wakati alama zao ni za juu. Na hii ni kwa masomo yote.

Mheshimiwa Waziri,
Kumekuwa na utamaduni katika nchi hii wa kukataa ukweli. Kufuatia uchunguzi uliofanywa na Kamati za Bunge, tumeshuhudia wizi na ufisadi wa kutisha ukifichuliwa Bungeni hivi karibuni hali iliyopelekea mpaka Mheshimiwa Rais kubadili Baraza lake la Mawaziri.

Sasa baada ya kuyasema yote hayo, tunasema kuwa Baraza la Mitihani la Tanzania, limekuwa likilalamikiwa kwa zaidi ya miaka 30, lakini malalamiko hayo yamekuwa yakipokewa kwa sikio la uziwi. Imefikia mahali tunasema kuwa hatuna tena imani na Baraza hilo.

Mheshimiwa Waziri,
Ili kupata ukweli wa malalamiko na shutuma hizi, na ili kujibu lile swali juu ya watoto wa Kiislamu ambalo halikupata jibu Bungeni, tunaitaka serikali kufanya yafuatayo:


  1. Tume huru iundwe kuchunguza Baraza la Mitihani la Tanzania na utendaji wake kazi kwa kipindi cha miaka kumi iliyopita.
  2. Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani (NECTA) ajiuzulu mara moja ili kulinda heshima ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzaani na Baraza la Mitihani. Watendaji wakuu wa kitengo cha mitihani na wanaohusika na mfumo wa Kumputa ya Baraza la Mitihani nao wawajibishwe mara moja.
  3. Hatua za kisheria na kibinadamu zichukuliwe dhidi ya watumishi wa Baraza la Mitihani watakaothibitika kuhusika na kashfa hii.
  4. Muundo wa Baraza la Mitihani uzingatie uwiano wa kidini, kitendo cha chombo nyeti kama hiki kujazana watu wa dini moja kunaliondolea Baraza la Mitihani sura ya kitaifa, kwani takwimu zinaonyesha Makatibu Wakuu Watendaji na Manaibu Katibu Wakuu wamekuwa Wakristo na Wenyeviti wa Baraza hilo ni Wakristo tangu lilipoanzishwa mwaka 1973, mpaka hii leo na takwimu tunazo.

Mheshimiwa Waziri,

Tunaomba ieleweke kuwa tunachotaka ni kupatikana haki na kufanyika uadilifu kwa watu wote. Hatudai wala hatutaki upendeleo kwa Waislamu na wala hatutaki kuona mtu yeyote anaonewa au kuporwa haki yake, awe Mwislamu au mtu wa dini nyingine.

Tunachoamini ni kuwa kama Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi haina cha kuficha, basi itaunda Tume hiyo kwa haraka na kuhakikisha kuwa ni Tume ya kuaminika itakayofanya kazi yake kwa umakini, kwa kina na kwa uadilifu wa hali ya juu kabisa.

Lakini kama Wizara yako itaona kuwa haiwezi kuunda Tume ya uchunguzi, tunacho kuhakikishia ni kuwa sisi tutafanya kila liwezekanalo na kwa namna yoyote kuhakikisha kuwa Tume hiyo inaundwa. Na ikigundulika kuwa kuna hujuma zinafanyika katika utendaji wa Baraza, basi itabidi uwajibikaji uanze kwenye Wizara kabla ya kuwawajibisha watendaji wa Baraza la Mitihani.

Ni imani yetu kuwa utayapokea madai ya Waislamu na kuyafanyia kazi kwa umakini na kwa haraka ili kujenga mustakbali mwema wa nchi hii na watu wake.

Tunaomba kuwasilisha,

Mwenyekiti,

Baraza Kuu la Jumuiya na Taasisi za Kiislamu

Juni 8, 2012
 
Mambo mengine yanaongozwa na hisia sana. Ila kuna mambo ya msingi lazima dini zetu zibadili. Moja ni kuwa watoto wetu tuwape muda wa kusoma zaidi ya kujifunza kuendesha mihadhara na kupiga madufu. Asilimia kubwa ya wanafunzi wa kiislam wanatumia kusali zaidi ya kujisomea. Nimeona wengi sana, Kule Tanga. Mwanafunzi yuko radhi kutoka darasani ili tu asikose ibada. Ingawa si mbaya!!

Mwaka jana kule Ifunda kuna dogo alikwenda akawa anakwenda hadi darasani na kanzu. Mgogoro uliotokea ulipelekea shule kufungwa. Na matukio kama haya si machache.

Sasa utafananisha vipi na mtu anayewaza shule na kupata muda wa kujisomea.

Cha msingi lazima tuamini dini zipo. Pia tujue huku si Arabauni ambako dini na shule ni kitu kimoja.

Angalia hata shule zetu za kiislam zinafanya nini?? Au tunataka matokea pasipokufanyia madhaifu yetu.

Ukweli ni kuwa waliojitambua wanashinda na tukiishi kuwa tunaonewa kila siku tutaishia kuwa watumwa wa milele.

Kingine cha kuangalia miaka ya hivi karibuni wizara ya elimu imekwa chini ya mawaziri waislam kuna kilichotokea? Kwa maana hapatakiwi upendeleo wa namna yoyote.

Ndo maana Ndalichako alipotoka Kawambwa alimteuwa Mkristo mwingine. Mbona husemi kwa nini asiteuliwe muislam?

Hakuna njia tukaze tu. Mimi watoto wangu nawapa kinachotakiwa katika wakati mwafaka.
 
1. Waislam mbona hamjalalamika kuhusu uteuzi wa WILLIAM LUKUVI ambaye kwenye hii video hapa chini aliamua kuwatukana waislam na wazanzibari kuwa ni ma extremists?

2. Waislam pamoja na mapesa mlio nayo mnashindwa kuwa na vyombo vya habari vyenu ambayo vinaendana na karne tuliyonayo.

3. Kwa nini hamjalalamika au kufungua kesi ya mahakamani dhidi ya serikali kufanya upendeleo kwa bakwata ambayo ni NGO kama NGO zinginezo kama zile zinazotazama wanyama na misitu?

4. Hivi Tatizo la waislam 2015 ni Joyce Ndaluchako au kula lingine? Maaana mimi siamini tatizo ni huyu mama bali naamini tatizo ni MFUMO K na mfano mzuri ndio huuu

5. Mbona mmenyamaza kimya baada ya BAKWATA kumwalika Kasim Majaliwa kuwa mgeni rasmi kwenye siku ya Maulid huku wakijua wazi kuwa SI muislam (alikuwa muislam kisha aka ritadi kumfuata mkewe) wakati huo huo mnajua wazi kuwa BAKWATA ni mafisadi na hawalipi kodi.

Narudia maneno ya Jenerali Ulimwengu. Tusiburuzane kwenda peponi, Tatizo la waislam Tanzania si hawa Wagala. Tatizo liko ndani ya nyumba yetu wenyewe. Haiwezekani tunataka kupigana Jihadi kwenye nyumba zetu ili hali Nafsi zetu haziko sawa.

Hebu mie ngoja nipate Witri
 
Inawezekana madai ya tamko yana ukweli au hayana ukweli lakini kinachonipa shida, kwa nini madai ambayo yalitolewa tamko mwaka 2012 yameanza tena kurudiwa rudiwa katika kipindi hiki ambacho utawala mpya wa Rais Magufuli umemaliza kuunda Baraza la Mawaziri juzi tarehe 23 Dec 2015.

Kwa nini Awamu iliyopita(awamu ya nne) haikushinikizwa kuunda tume ili kujibu madai yaliyotolewa kwenye tamko.

Kama serikali haikuunda tume kama ilivyotakiwa, kwa nini watoa tamko hawakuunda tume yao kama walivyosema,
Lakini kama Wizara yako itaona kuwa haiwezi kuunda Tume ya uchunguzi, tunacho kuhakikishia ni kuwa sisi tutafanya kila liwezekanalo na kwa namna yoyote kuhakikisha kuwa Tume hiyo inaundwa. Na ikigundulika kuwa kuna hujuma zinafanyika katika utendaji wa Baraza, basi itabidi uwajibikaji uanze kwenye Wizara kabla ya kuwawajibisha watendaji wa Baraza la Mitihani.

Why now?
 
Ndugu Saidi: uchaguzi unekwisha nji imepiga hatua. Zile hoja za udini sasa zimevadilika na kuwa za ukanda na hata ukabila; wewe unataka kuturudisha nyuma.

Tanzania ta leo sioni dalilu zozote za udini labda mzianze, mara nyingi huingizwa kama Rais ni mkristo. Hoja na data za 2012 kwa hali ilivyo sasa hazina mshiko tena, hizo 71% si ukweli, na mabadiliko yaliyodhaniwa yatakuja yako bado hayapo.

Dawa ni kusoma kwa bidii tu.
 
Ukweli kama husomi utafeli.. hata somo la dini kama husomi utafeli.. wasisingizie Necta.. wala ndarichako.. mashuleni tunajijua.. hata wakristo ambao wao ni dini tuu wanadiriki hata kuamini Mungu atatoa majibu. HAKUA MAX ZA BURE KAMA HUSOMI.. HATA UKIANDAMANA.. BADILIKENI
 
Bangi waliovuta, ni "Bangi kwa jamii" (Max)
Hawajui kuwa Dini ni bangi ambayo husababisha kufanya usiyotarajia!!
Wamebadili kila kitu hadi kuvaa shela mashuleni ili wafaulu lakini bado watoto wanafeli tu.
Jibu ni jepesi sana, uislamu sio kila kitu,mambo mengine yanajitosheleza nje ya Dini.
Ni vyema wabadilike ama mifumo ya Elimu itawameza tu.
 
Waziri Ndalichako ayafanyie kazi malalamiko haya, Haiwezekani section nzima ya jamii inalalamika halafu hatua za kiuchunguzi hazifanyiki ipasavyo. Waislamu wana hoja ya msingi hapa!

Tumekuwa na Jk, Shein kisha Gharib na Kinana na Kawambwa kelele hizi zilifia. Leo amewekwa huyu mama kelele zimeanza kuratibiwa. Mimi nasema waruhusuni watoto wenu washindane hasa kwenye elimu dunia. Madrasa yawe na siku maalum. Pia msiwarithishe chuki zisizo na maana itawafanya wanaposhindwa kufikia malengo watajua kuna jamii inayoamini tofauti nao inawafelisha. SI SAWA WAACHENI WASHINDANE
 
Mh!!! mmeanza na udini, mmezoea awamu ya nne mmebebwa sana nyinyi. Sasa mmeona awamu hii hamna dezo mmeanza kelele. Someni kwa bidii punguzeni kushindisha watoto madrasa mtafaulu. Tena nakukumbusha mheshimiwa Magufuli hii awamu ya tano ni yetu watoto wa nyumba kubwa( Sara).
 
Back
Top Bottom