UTANGULIZI
Tunamshukuru Mungu kwa neema alotupatia kua hai hadi sasa. Ni jambo lisilopingika kwamba, kumekuwa na changamoto kubwa hasa kwa wahudumu wa Afya kutokujali wagonjwa na mara kadhaa kutojali akina mama wajawazito. Changamoto hii hupelekea baadhi ya wajawazito ama wagonjwa kupoteza maisha kwa uzembe wa wauguzi ama wahudumu wengine wa Afya.
Katika zahanati moja, aliwahi kufariki mama aliyeenda kujifungua. Mama huyo alikosa msaada wa muuguzi kwa sababu muuguzi alikuwa aki-chat huku mama aliyetayari kujifungua akiwa anahangaika mwenyewe kitandani bila msaada hadi kupoteza maisha yake pamoja na mtoto.
MADHARA YA WAHUDUMU WA AFYA KUTOJALI WAGONJWA NA WAJAWAZITO
NINI KIFANYIKE ILI KUONGEZA UWAJIBIKAJI WA WAHUDUMU WA AFYA
HITIMISHO
Kila mhudumu wa Afya atambue kwamba kazi yake amepewa dhamana ya kusaidia afya za watu na sio kuziangamiza. Wanaohudumia akina mama wajawazito watambue kwamba na wao walizaliwa. Wanaohudumia wagonjwa watambue kwamba na wao kesho wanaweza kuwa wagonjwa, Kama uongozi wa juu wa kituo husika utasimamia maadili ya taaluma ya afya ipasavyo, na kila mhudumu akatambua wito wake ipasavyo, basi vifo vya makusudi vya wagonjwa na akina mama wajawazito vitapungua sana.
Tunamshukuru Mungu kwa neema alotupatia kua hai hadi sasa. Ni jambo lisilopingika kwamba, kumekuwa na changamoto kubwa hasa kwa wahudumu wa Afya kutokujali wagonjwa na mara kadhaa kutojali akina mama wajawazito. Changamoto hii hupelekea baadhi ya wajawazito ama wagonjwa kupoteza maisha kwa uzembe wa wauguzi ama wahudumu wengine wa Afya.
Katika zahanati moja, aliwahi kufariki mama aliyeenda kujifungua. Mama huyo alikosa msaada wa muuguzi kwa sababu muuguzi alikuwa aki-chat huku mama aliyetayari kujifungua akiwa anahangaika mwenyewe kitandani bila msaada hadi kupoteza maisha yake pamoja na mtoto.
MADHARA YA WAHUDUMU WA AFYA KUTOJALI WAGONJWA NA WAJAWAZITO
- Mgonjwa kupoteza uhai
- Kusababisha magonjwa mengine
- Kupoteza uaminifu
- Kudharau viongozi wa serikali serikali
NINI KIFANYIKE ILI KUONGEZA UWAJIBIKAJI WA WAHUDUMU WA AFYA
- Wahudumu wa Afya wapewe stahiki zao kwa wakati.
- Sheria ichukuliwe kwa wote wanaosababisha vifo vya wagonjwa au wajawazito kwa makusudi. Wanaofanya hivyo wanapaswa kupewa adhabu kama wauwaji wengine. Hii itaweka fundisho kwa wengine ili kila mtu ajue uhai ni bora kuliko fedha na madaraka. Ikiwa wakosaji watawajibishwa kwa mujibu wa sheria na sio kuwaamisha vituo vya kazi kwani hata huko waendako watarudia tabia hizo hizo.
- Semina za mara kwa mara kwa wahudumu wa Afya zifanyike. Serikali chini ya wizara husika itenge bajeti ya kutoa semina za maadili na wajibu wa wahudumu wa afya mara kwa mara ili kuamsha hali ya uwajibikaji pindi wanapokuwa katika huduma.
- Viongozi wa juu wa serikali wakemee na kulaani vitendo vya kutojali wangonjwa na wajawazito. Kwa kufanya hivyo, kila mhudumu atatambua kwamba anapaswa kutoa huduma kama taaluma yake inavyomwelekeza na kama maadili ya kazi yanavyotaka.
HITIMISHO
Kila mhudumu wa Afya atambue kwamba kazi yake amepewa dhamana ya kusaidia afya za watu na sio kuziangamiza. Wanaohudumia akina mama wajawazito watambue kwamba na wao walizaliwa. Wanaohudumia wagonjwa watambue kwamba na wao kesho wanaweza kuwa wagonjwa, Kama uongozi wa juu wa kituo husika utasimamia maadili ya taaluma ya afya ipasavyo, na kila mhudumu akatambua wito wake ipasavyo, basi vifo vya makusudi vya wagonjwa na akina mama wajawazito vitapungua sana.