Elon J
JF-Expert Member
- Sep 30, 2022
- 630
- 1,846
Baadhi ya wanafunzi waliotakiwa kujiunga na kidato cha kwanza katika maeneo mbalimbali ya Kanda ya Ziwa wamegoma kuripoti shuleni kwa kigezo kuwa wenzao waliomaliza kidato cha nne, sita na chuo kikuu wapo mitaani bila ajira.
Wanafunzi hao wamesema hali hiyo imewakatisha tamaa ya kuendelea na masomo ya sekondari badala yake kuamua kutafuta shughuli nyingine za kiuchumi ikiwemo mafunzo ya ufundi.
Kwa mujibu wa gazeti la Nipashe, mmoja wa wazazi wa watoto ambao hawajaripoti shuleni, mkazi wa Kata ya Turwa wilayani Tarime mkoani Mara, Elizabeth Charles amesema binti yake alikataa kuandikishwa na kutaka apelekwe chuo cha ufundi cherehani kutokana na wahitimu wengi kuwa mitaani bila kazi maalum.
Wanafunzi hao wamesema hali hiyo imewakatisha tamaa ya kuendelea na masomo ya sekondari badala yake kuamua kutafuta shughuli nyingine za kiuchumi ikiwemo mafunzo ya ufundi.
Kwa mujibu wa gazeti la Nipashe, mmoja wa wazazi wa watoto ambao hawajaripoti shuleni, mkazi wa Kata ya Turwa wilayani Tarime mkoani Mara, Elizabeth Charles amesema binti yake alikataa kuandikishwa na kutaka apelekwe chuo cha ufundi cherehani kutokana na wahitimu wengi kuwa mitaani bila kazi maalum.