Na Restuta James 19th June 2011 Wafungwa zaidi ya 20 walio katika gereza la Maweni, mkoani Tanga, ambao wamehukumiwa kunyongwa wamegoma kula na mmoja anadaiwa kufariki dunia.
Taarifa zilizolifikia gazeti hili zinaeleza kwamba wafungwa hao wamegoma kwa siku ya tano sasa kwa madai ya kupewa chakula kibovu. Hata hivyo, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Shamsi Vuai Nahodha, amesema hana taarifa za wafungwa hao kugoma. Ndio nasikia kwako mie silijui hilo, alisema Nahodha.
Hata hivyo, aliahidi kuzifuatilia. Wakati Nahodha akieleza hayo, Waziri Kivuli wa Wizara hiyo, Godbless Lema, alithibitisha kuwepo kwa mgomo huo akieleza kwamba hadi jana, ni siku ya tano tangu wafungwa hao wagome kula.
Alisema baada ya kupata taarifa za kuwepo kwa mgomo huo, aliwasiliana na mkuu wa gereza hilo, ambaye naye alithibitisha wafungwa hao kugoma. Lakini amekanusha kuhusu huyo aliyekufa, amesema hakuna mfungwa ambaye amekufa, alisema Lema.
Lema ambaye pia ni Mbunge wa Arusha Mjini (Chadema), alisema Kambi yetu inafanya a very close follow-up (inafuatilia kwa karibu), suala hilo, lakini nasema haiwezekani wafungwa wakagoma tu kula lazima kuna tatizo lingine. Aliongeza kuwa haiwezekani wafungwa hao wakagoma tu kula kwa kuwa wanakabiliwa na changamoto nyingi ikiwemo rufaa zao kuchelewa kusikilizwa.
Nimetembelea magareza Arusha nikaingia jela ya wanawake na wanaume, niliyoyaona huko ni hatari kubwa sana, wafungwa waliokata rufaa inachukua muda mrefu kusikilizwa na wakishinikiza sana wanahamishwa gerezaasilimia 50 ya mahabusu wanakaa hadi miaka minane kesi zao hazijasikilizwa kwa kisingizio cha upelelezi kutokamilika, kwa hiyo nina amini kwamba hata hao waliogoma wana madai zaidi ya chakula, alisema.
Lema alifafanua kuwa Taarifa nilizonazo ni kwamba wafungwa sita wapo katika hali mbayanafuatilia suala hili na ikiwezekana nitaenda Tanga ili kupata ukweli wake kabla ya kulitolea taarifa rasmi, alisema. Lema alisema wafungwa hao ni waliohamishwa kutoka gereza la Ukonga. CHANZO: NIPASHE JUMAPILI
Taarifa zilizolifikia gazeti hili zinaeleza kwamba wafungwa hao wamegoma kwa siku ya tano sasa kwa madai ya kupewa chakula kibovu. Hata hivyo, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Shamsi Vuai Nahodha, amesema hana taarifa za wafungwa hao kugoma. Ndio nasikia kwako mie silijui hilo, alisema Nahodha.
Hata hivyo, aliahidi kuzifuatilia. Wakati Nahodha akieleza hayo, Waziri Kivuli wa Wizara hiyo, Godbless Lema, alithibitisha kuwepo kwa mgomo huo akieleza kwamba hadi jana, ni siku ya tano tangu wafungwa hao wagome kula.
Alisema baada ya kupata taarifa za kuwepo kwa mgomo huo, aliwasiliana na mkuu wa gereza hilo, ambaye naye alithibitisha wafungwa hao kugoma. Lakini amekanusha kuhusu huyo aliyekufa, amesema hakuna mfungwa ambaye amekufa, alisema Lema.
Lema ambaye pia ni Mbunge wa Arusha Mjini (Chadema), alisema Kambi yetu inafanya a very close follow-up (inafuatilia kwa karibu), suala hilo, lakini nasema haiwezekani wafungwa wakagoma tu kula lazima kuna tatizo lingine. Aliongeza kuwa haiwezekani wafungwa hao wakagoma tu kula kwa kuwa wanakabiliwa na changamoto nyingi ikiwemo rufaa zao kuchelewa kusikilizwa.
Nimetembelea magareza Arusha nikaingia jela ya wanawake na wanaume, niliyoyaona huko ni hatari kubwa sana, wafungwa waliokata rufaa inachukua muda mrefu kusikilizwa na wakishinikiza sana wanahamishwa gerezaasilimia 50 ya mahabusu wanakaa hadi miaka minane kesi zao hazijasikilizwa kwa kisingizio cha upelelezi kutokamilika, kwa hiyo nina amini kwamba hata hao waliogoma wana madai zaidi ya chakula, alisema.
Lema alifafanua kuwa Taarifa nilizonazo ni kwamba wafungwa sita wapo katika hali mbayanafuatilia suala hili na ikiwezekana nitaenda Tanga ili kupata ukweli wake kabla ya kulitolea taarifa rasmi, alisema. Lema alisema wafungwa hao ni waliohamishwa kutoka gereza la Ukonga. CHANZO: NIPASHE JUMAPILI