Wafungwa Gerezani

Bishanga

JF-Expert Member
Jun 29, 2008
15,323
10,063
Kila kukicha tunasikia malalamiko ya wafungwa nchini mwetu kuhusiana na lishe mbovu. Mimi nina wazo na wadau wa JF naomba tulijadili:
Kwa kuwa bajeti ya serikali inatengwa kwa ajili ya kila mfungwa kwa mlo wake wa siku,na kwa kuwa kiwango hicho kinajulikana,basi ni bora uwekwe utaratatibu wa kupata makandarasi wa nje (catering outsourcing) ambao watakua wanapika chakula nje ya magereza lakini chini ya usimamizi wa askari magereza na baadae kubeba hicho chakula na kuwagawia wafungwa. Kwa utaratibu huu itajulikana kabisa gereza lina wafungwa kadhaa hivyo zipelekwe sahani kadhaa za chakula ambacho kitakuwa ni kwa mujibu wa official ration ya mfungwa,mathalan wali,maharage,mchicha,kipande cha tunda etc. Nashauri hivi kwa sababu inasemekena on paper wafungwa huwa wanapewa vyakula vyote hivi ingawa physically hawavioni. Wadau mnaonaje wazo hili,si litasaidia kuondoa udokozi na kuwaongezea lishe wafungwa wetu?
 
Kila kukicha tunasikia malalamiko ya wafungwa nchini mwetu kuhusiana na lishe mbovu. Mimi nina wazo na wadau wa JF naomba tulijadili:
Kwa kuwa bajeti ya serikali inatengwa kwa ajili ya kila mfungwa kwa mlo wake wa siku,na kwa kuwa kiwango hicho kinajulikana,basi ni bora uwekwe utaratatibu wa kupata makandarasi wa nje (catering outsourcing) ambao watakua wanapika chakula nje ya magereza lakini chini ya usimamizi wa askari magereza na baadae kubeba hicho chakula na kuwagawia wafungwa. Kwa utaratibu huu itajulikana kabisa gereza lina wafungwa kadhaa hivyo zipelekwe sahani kadhaa za chakula ambacho kitakuwa ni kwa mujibu wa official ration ya mfungwa,mathalan wali,maharage,mchicha,kipande cha tunda etc. Nashauri hivi kwa sababu inasemekena on paper wafungwa huwa wanapewa vyakula vyote hivi ingawa physically hawavioni. Wadau mnaonaje wazo hili,si litasaidia kuondoa udokozi na kuwaongezea lishe wafungwa wetu?

wazo zuri Bishanga.......
.......sijui utaratibu ukoje huko Jela, Je wafungwa wanajipikia au wanapikiwa.......

pili kunahitajika kuwa na taarifa rasmi kuonyesha kuwa kweli hayo mambo ya chakula kibovu yapo huko.....ili hat akama hiyo taarifa tunaituma vyombo vya kutetea haki za binadamu walau inakuwa na substance in it.........

Taarifa hiyo yaweza kutoka kwa wafungwa wenyewe au au NGO moja ya haki za binadamu kama watafanya huo uchunguzi..........
 
Hivi wewe bishanga na huyo anaekusapoti mkosirias kweli?! Ukiboresha msosi gerezani population yote jobless itakimbilia huko. Kuna wa2 hawajui watakula nn wakiskia mabadiliko haya wote watafanya uhalifu wakafungwe! Gerezan pasiwe mahala pa kuvutia wa2 bwana. Alaaa! Hii ndo itawatisha wa2 na watajitoa uhalifuni. NAWASILISHA.
 
Kwa nchi za Afrka jela ni jeneza la kukupeleka kaburini... kwa nchi za Ulaya jela ni sawa kitanda cha kukutibu na kukutengeneza ili uje kuwa raiya mwema. (kwa baadhi ya kesi).
 
Hivi wewe bishanga na huyo anaekusapoti mkosirias kweli?! Ukiboresha msosi gerezani population yote jobless itakimbilia huko. Kuna wa2 hawajui watakula nn wakiskia mabadiliko haya wote watafanya uhalifu wakafungwe! Gerezan pasiwe mahala pa kuvutia wa2 bwana. Alaaa! Hii ndo itawatisha wa2 na watajitoa uhalifuni. NAWASILISHA.


duuhh eti wewe ndio uko....."sirias".........haya bana
 
Hivi wewe bishanga na huyo anaekusapoti mkosirias kweli?! Ukiboresha msosi gerezani population yote jobless itakimbilia huko. Kuna wa2 hawajui watakula nn wakiskia mabadiliko haya wote watafanya uhalifu wakafungwe! Gerezan pasiwe mahala pa kuvutia wa2 bwana. Alaaa! Hii ndo itawatisha wa2 na watajitoa uhalifuni. NAWASILISHA.
Tripo omba Mungu yasisikute na hujafa hujaumbika,jela ni kwa kila binadamu kuanzia Marais (Kaunda,Chiluba,Mandela,Rais wa Taiwan na Korea) hadi sisi watu wa kawaida. Hilo moja ,la pili wewe hujawahi kuwa na ndugu yako aliyefungwa? alikusimuliaje alipotoka? La tatu hakuna hakimu wala jaji wala kifungu cha sheria kinachosema starvation ni sehemu ya adhabu. Na mwisho wangapi maskini wanafungwa wakati hawana hatia kwa vile tu walikosa uwezo wa kuwa na wakili?
 
Watanzania siku watakapo juwa nini maana ya kuwa mtu huru... na kuthamini uhuru waliokuwa nao, Na serikali ikisha weza kutambua michango binafsi ya raiya wake, ndipo hapo tutakapo anza kulalamikia kuwepo na hali nzuri magerezani.

Kama serikali inashindwa kulipa walimu, waganga na wauguzi n.k, nk. Vipi itaweza kuwahudumia wafungwa, nasi raiya tumekaa na kuridhika na hali hii... Kunaitajika mapinduzi ya kifikra kwanza.
 
Kila kukicha tunasikia malalamiko ya wafungwa nchini mwetu kuhusiana na lishe mbovu. Mimi nina wazo na wadau wa JF naomba tulijadili:
Kwa kuwa bajeti ya serikali inatengwa kwa ajili ya kila mfungwa kwa mlo wake wa siku,na kwa kuwa kiwango hicho kinajulikana,basi ni bora uwekwe utaratatibu wa kupata makandarasi wa nje (catering outsourcing) ambao watakua wanapika chakula nje ya magereza lakini chini ya usimamizi wa askari magereza na baadae kubeba hicho chakula na kuwagawia wafungwa. Kwa utaratibu huu itajulikana kabisa gereza lina wafungwa kadhaa hivyo zipelekwe sahani kadhaa za chakula ambacho kitakuwa ni kwa mujibu wa official ration ya mfungwa,mathalan wali,maharage,mchicha,kipande cha tunda etc. Nashauri hivi kwa sababu inasemekena on paper wafungwa huwa wanapewa vyakula vyote hivi ingawa physically hawavioni. Wadau mnaonaje wazo hili,si litasaidia kuondoa udokozi na kuwaongezea lishe wafungwa wetu?

Hilo wazo ni zuri na moja katika majukumu aliyopewa Masha ni kuhakikisha namna ya misosi, malazi na makazi ya wafungwa yanabadilika kufikia hadi ya kibanadam, kwani kwa sasa (na ndivyo alivyokuta JMK alipoingia madarakani) hayo mambo muhimu hata wanyama wanafugwa kwa vizuri zaidi ya hawa binadam wenzetu. JMK kaanza na usafiri wa wafungwa, kauboresha na unajionesha, ingawa watendaji walipiga panga hata kwenye hayo magari. Na tutunai kuwa bajeti ijayo itakuwa na mifedha ya kujenga jela za kisasa> Moja ya njia alizotumia JMK kupunguza msongamano na hicho kibajeti kidogo cha wafungwa wanachopata angalau kisaidie ni kuongeza majaji na kuongeza miundo mbinu mahakamani ili kesi zimalizwe haraka. itasaidia kwa kiasi chake na hili la makandarasi wa chakula laja na linatakiwa liwe ni kwa ajili ya chakula cha askari jela na wafungwa, ili wasihamasishe askari jela kuwaibia chakula chao wafungwa, kitakapoboreshwa bajeti ijayo. Kama haikuwa hivyo basi Masha ajuwe ndio safari mwakani.
 
wazo zuri ila kwa serikali yetu hilo haliwezekani, si unajua nchi ya kitu kidogo
 
Yeah Jamaa angu alipotoka gerezan alinisimulia ma-men wanaolewa! Msosi upo but sio ku-starve kama usemavyo. Kwality obviously sio km ya home. Kuna mambo ya ku-solve kwanza hapa. Alieiba kuku, simu, pochi nk, aliyempiga raisi kibao, na vi2 km hivyo nao anafungwa! Y?! Wapo wengi sana wa namna hii! Wanajaza magereza. Msongamano! Huduma kama msosi zitakua za chini pia. Hawa wangefanyishwa community services 2 km kusafisha masoko, barabara na vi2 km ivyo sio kuwalundika na waliobaka vitoto vichanga, walioua, au walio vunja bank huko gerezani. Tukifanya hivi hata 2takua na wafungwa wale sirias wachache na huduma zitaboreshwa ofcoz lazima pia management fisadi ipigwe chini.
 
Back
Top Bottom