Mtoto wako (aliye shule ya kutwa) anapata chakula shuleni? Kwa kiwango gani mzazi/mlezi unahusika katika kufanikisha hilo?

JF Toons

Digital Art by JF
Feb 19, 2024
32
66
chakula shuleni.PNG

Serikali imeweka utaratibu wa kuhakikisha huduma muhimu ya chakula na lishe inapatikana kwa Wanafunzi wa elimu ya msingi.

Kulingana na Mwongozo wa Kitaifa wa Utoaji wa Huduma ya Chakula na Lishe kwa Elimumsingi, wazazi na Wadau wanatakiwa kuchangia vitu mbalimbali ikiwemo;

  • Chakula
  • Mafuta
  • Sukari
  • Chumvi pamoja na mahitaji mengine ya kupikia
  • Posho ya mtunza stoo
Malipo ya Wapishi

Hii yote ni katika kuhakikisha Wanafunzi wanapata huduma hiyo muhimu wawapo Shuleni.

Je, ulikuwa unafahamu kuhusu hilo? Kwa kiasi gani wewe Mzazi/Mlezi unatekeleza wajibu huu?
 
Hilo ni jukumu la Serikali kwa asilimia 1000. Ujamaaa umetuharibu sana, Wazazi wanalipa kodi, ni jukumu la Serikali kulisha Watoto. Hii nchi watawala wana raha sana make majukumu mengi wanasaidiwa na still wanawakamua raia kodi kubwa sana
 
Wazazi wanapewa jukumu zito, alipe Kodi zote halafu hasaidiwi lolote, bora ada itolewe serikali ifanye mambo mengine ya kimaendeleo ikiwepo madarasa na barabara kwani Hali ni mbaya katika shule za serikali
 
Back
Top Bottom