Elections 2010 Wafuasi wa CCM wadaiwa kumpiga mwandishi wa Mwananchi

Iko siku mtasikia Ikulu imevunjwa na MWEKEZAJI! Haya ndiyo matokeo ya ubinafsishaji na uuzwaji wa rasilmali za nchi kiholela. Itafikia siku tutadaiwa KODI ya kutembea kwa miguu, kwani hata barabara zitakuwa zimeuzwa pia.

Unatarajia nini kwa fisadi, zaidi ya ufisadi?

Ukichagua hovyo, ukatendewa hovyo, usiseme hovyo! - Jenerali Ulimwengu
 
Ni vema jina la Mwandishi liwekwe rasmi kwenye ORODHA ya Mashujaa wa Ukombozi. Nchi inapokombolewa inakuwa na hata mashahidi. Lengo la kumpiga huyo mwandishi ni kutishia waandishi wa habari wote. Ni tumaini langu kwamba Chama cha Waandishi wa Habari Tanzania kitajitokeza mapema kupigania haki za mwenzao.

Taarifa zinasema CCM wameshafanya Vurugu Vunjo vile vile, hata wakavunja kioo cha gari la Mrema. Hawataishia hapo.

Kumbukeni kulikwa na semina ya wana CCM huko Moshi na Kikwete akawahutubia. Aliwaambia hii serikali ni yao, wanaweza kufanya chochote na hakuna mtu wa kuwauliza. Walipomaliza semina wakapita barabarani wakipiga watu. Wakaingia hata KCMC kupiga wafanyakazi na wagonjwa. Kwani hadi leo wameulizwa?

Kama kutatokea vurugu Tanzania, zitakuwa zimeanzishwa na CCM. Wana uchu wa madaraka kiasi cha kuweza hata kuua ili watawale. Yaani watawale kwa nguvu. Wamezoea mno kuhodhi madaraka.
 
Hivi ni kwa sababu wanaandika kwa kufuata maadili ya uandishi wa habari katika uchaguzi mkuu huu? Tendwa na Lewis naomba sasa mfuate sheria na haki. Mwanzo mmeto maonyo, sasa ni kutekeleza sheria - UVCCM hao chini ya engineer Ridhiwani akisaidiwa na kamanda wa chipukizi ngazi ya taifa - the son of Mama Salma Kikwete!
 
Mgombea wa CCM jimbo la Kwimba ni SHARIF MANSOOR
Ambaye ni;
1. Mweka Hazina wa CCM mkoa wa Mwanza
2. Mmiliki wa vituo vya Mafuta kikiwemo kilichovunjwa na Magufuli barabara ya Makongoro kisha Serikali ikaamriwa kulipa mabilioni ya fidia
3.Ndio mfadhili mkuu wa ziara za viongozi wa kitaifa/CCM kwa kuchangia gharama za Chakula na mengineyo kutoka mfukoni mwake
4. Ni M burushi
5.
6.
7.

so.........what?
 
Ni vema jina la Mwandishi liwekwe rasmi kwenye ORODHA ya Mashujaa wa Ukombozi. Nchi inapokombolewa inakuwa na hata mashahidi. Lengo la kumpiga huyo mwandishi ni kutishia waandishi wa habari wote. Ni tumaini langu kwamba Chama cha Waandishi wa Habari Tanzania kitajitokeza mapema kupigania haki za mwenzao.

Taarifa zinasema CCM wameshafanya Vurugu Vunjo vile vile, hata wakavunja kioo cha gari la Mrema. Hawataishia hapo.

Kumbukeni kulikwa na semina ya wana CCM huko Moshi na Kikwete akawahutubia. Aliwaambia hii serikali ni yao, wanaweza kufanya chochote na hakuna mtu wa kuwauliza. Walipomaliza semina wakapita barabarani wakipiga watu. Wakaingia hata KCMC kupiga wafanyakazi na wagonjwa. Kwani hadi leo wameulizwa?

Kama kutatokea vurugu Tanzania, zitakuwa zimeanzishwa na CCM. Wana uchu wa madaraka kiasi cha kuweza hata kuua ili watawale. Yaani watawale kwa nguvu. Wamezoea mno kuhodhi madaraka.

Mwandishi aliyepigwa ni yule ambaye alifukuzwa katika msafara wa JK,

Waandishi wa Mwananchi wafukuzwa msafara wa JK
Thursday, 26 August 2010

Kizitto Noya
WAANDISHI wa Kampuni ya Mwananchi Communications Limited (MCL) wamefukuzwa kwenye kampeni za kumnadi mgombea urais kwa tiketi ya CCM, Jakaya Kikwete.

Ray Naluyaga, ambaye anaandikia gazeti la The Citizen, na Frederick Katulanda wa Mwananchi, walifukuzwa kwa nyakati tofauti kwenye kampeni zilizofanywa katika mikoa ya Geita na Kagera.

Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba alikanusha chama hicho kutimua waandishi kwenye msafara wa Kikwete akisema anaamini waandishi hao wamefukuzwa na mtu aliyemwita kuwa ni mhuni na si CCM kama chama.

Waandishi hao walifukuzwa kutokana na chama hicho kueleza kutofurahishwa na habari iliyoripotiwa na gazeti hili juzi ikiwa na kichwa kisemacho "JK ahaha kunusuru mpasuko CCM".

Akielezea mkasa huo, Naluyaga alisema alifukuzwa Ikulu saa 1:30 asubuhi jana mjini Bukoba ambako msafara wa mgombea huyo ulipokuwa ukijiandaa kwa safari ya kuelekea Wilaya ya Misenyi.

"Mimi nilifika Ikulu leo (jana) saa1:30 na kukuta waandishi wenzangu wakiwa wamevalia jaketi zilizoandikwa 'Kikwete Press 2010," alisema Naluyaga na kuongeza:

"Nikaenda kuripoti kwa (Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais) Salva Rweyemamu, lakini yeye akaniambia nimsubiri (mratibu wa habari wa timu ya Kikwete) Muhingo (Rweyemamu) kwa kuwa yeye (Salva) ni mshauri tu wa masuala ya habari."

Naluyaga alisema baada ya Muhingo, Mhariri Mtendaji wa magazeti ya New Habari Corporation ambaye sasa anafanya uratibu wa kampeni za urais za CCM, kuwasili alimtaka aendelee kusubiri kwa kuwa jina lake limepelekwa Ikulu kujadiliwa kwanza.

Muhingo, ambaye kampuni yake huzalisha magazeti ya Mtanzania, Rai, Bingwa na The African, pia alikuwepo kwenye timu ya kampeni ya Kikwete mwaka 2005 wakati mwenyekiti huyo wa CCM akiwania kuingia Ikulu kwa mara ya kwanza.

Katika kampeni za mwaka 2005, Muhingo alimfukuza mwandishi wa Mwananchi baada ya kutofurahishwa na habari alizokuwa akiandika.

"Msafara unaanza na yeye (Muhingo) akaendelea kuniambia subiri; subiri; subiri. Baadaye akasema suala langu ni gumu hivyo siwezi kwenda na msafara wao," alisema Naluyaga na kubainisha kuwa ndani ya Ikulu hiyo kulikuwa na makada kadhaa wa CCM, akiwamo mwenyekiti Kikwete, Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Khamis Kagasheki na Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk Deodorous Kamala.

Alisema ingawa Muhingo hakumweleza sababu za jina lake kupelekwa Ikulu kujadiliwa, makada mbalimbali wa CCM walimwambia kuwa tatizo ilikuwa habari iliyoripotiwa na gazeti hili juzi.

"Wengine walisema kampuni ya Mwananchi ni hatari sana kwa sababu ni kampuni binafsi inafanya kazi zake bila upendeleo. Lakini kama issue (suala) ni kampuni binafsi, mbona kulikuwa na waandishi wengi wa kampuni binafsi," alihoji Naluyaga.

Lakini jana Muhingo alikanusha kumfukuza Naluyaga akisema "Atakuwa amekwambia uongo. Kwa nini nimfukuze mwandishi? After all (zaidi ya yote) tunahitaji coverage (taarifa zitoke)".

Muhingo alieleza kuwa ni kweli alimwacha Naluyaga Ikulu ndogo ya mjini Bukoba, lakini si kwa sababu hakutaka aripoti matukio ya kampeni za CCM bali ni kwa sababu ya uhaba wa magari ya kusafiria.

"Tulitegemea tuwe na magari mawili ya waandishi, lakini tukapata moja tu na mimi nilikuwa na waandishi kumi niliotoka nao Dar es Salaam sasa katika mazingira hayo, unamchukua aliyeanzia Bukoba ama, unaendelea na wale ulioanza nao Dar es Salaam,"alihoji Muhingo.

Awali Katulanda alisema alidokezwa suala la kufukuzwa kwa waandishi wa Mwananchi juzi na Muhingo majira ya saa 4:00 asubuhi wakati Kikwete alipokuwa anahutubia kwenye Uwanja wa Katoro mjini Geita.

Alisema siku hiyo mara baada ya Kikwete kupanda jukwaani na kuanza kuhutubia, aliitwa na Muhingo, anayeshughulikia mambo ya habari.

"Akaniambia twende huku. Nikamuuliza wapi? Akasema twende. Akanipeleka mahala ambako nisingeweza kumsikiliza Kikwete anavyozungumza na kuniuliza:
"Kwa nini umeandika habari hiyo? Wewe huoni unatuharibia? Kuna vitu vingi vya kuandika ikiwamo wilaya mpya kuanzishwa mwezi Januari, lakini bado uliona hiyo ndio habari. Mimi ni mtu muhimu hata huko Mwananchi; jina langu limo kwenye usajili wa gazeti lenu na nitakufukuza kwenye msafara wetu," alieleza Katulanda akimnukuu Muhingo.

Katulanda alisema maswali hayo yaliibua mvutano kati yake na Muhingo hasa pale aliposisitiza kuwa anaamini alichoandika ndicho wananchi wanachopaswa kujua.

Katulanda alisema kuwa Muhingo alidai habari iliyoripotiwa na gazeti hili juzi kwamba Kikwete alitumia mkutano wa kampeni kwenye Jimbo la Buchosa kutuliza wimbi la mpasuko unaoonekana kukikumba chama hicho tawala baada ya kumalizika kwa kura za maoni za kuteua wagombea ubunge na udiwani zilizosababisha wanachama wengi kukimbilia upinzani.

Akizungumza na Mwananchi, Makamba alisema: "Ili uamuzi uwe wa chama lazima ufikiwe na Kamati Kuu, Nec au uamuzi afanye katibu mkuu. Vikao hivi havikufanyika kokote na mimi (katibu mkuu) sijaagiza mtu awafukuze waandishi. Fuatilia vizuri habari yako, utagundua tu kwamba yupo mhuni amekosana nao akaamua kuwafukuza."

Mhariri Mtendaji wa magazeti ya MCL, Theophil Makunga alieleza kusikitishwa na kitendo cha mratibu wa habari wa kampeni za CCM kuwafukuza waandishi wake, akisema kuwa kampuni haikutegemea kitendo hicho kufanywa na CCM.

"Sishangai sana kwani hata mwaka 2005 walimfukuza mwandishi wetu maeneo ya Ngara. Lakini nasikitika na sikutegemea hilo kufanywa na chama makini kama CCM," alisema Makunga na kuongeza.

"Hata hivyo bado ninawahakikishia wasomaji wa magazeti yetu kwamba tutafanya kila liwezekanalo kuwaletea habari zote zinazohusu kampeni zote, zikiwemo kampeni za CCM," alisema. MCL inachapisha magazeti ya Mwananchi, Mwananchi Jumapili, The Citizen, Sunday Citizen na Mwanaspoti.

Katibu wa Uenezi na Itikadi wa CCM, John Chiligati alisema hana taarifa ya tukio hilo na akalitaka gazeti hili liwasiliane na mratibu wa kampeni za chama hicho, Abdurhaman Kinana au Katibu Mkuu, Yusuf Makamba kwa maelezo zaidi.

Jana kutwa nzima, Kinana hakupatikana kuzungumzia suala hilo.

Habari inayoelezwa kulalamikiwa na CCM iliripotiwa na gazeti hili juzi kwamba Kikwete alitumia jukwaa la kampeni kunusuru mpasuko wa wanachama wanaohamia vyama vya upinzani kupinga matokeo ya kura za maoni za kupata wagombea ubunge na udiwani, akiwataka waige mfano wake wa uvumilivu.

Kikwete alisema hayo alipokuwa akizungumza kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Tarafa ya Nyehunge.

Alisema wanachama walioshindwa hawana budi kutulia na kuwapigia kampeni wagombea waliopita kupeperusha bendera ya chama hicho ili kishinde uchaguzi.

Alikuwa ameshtushwa na kitendo cha mbunge wa zamani wa Jimbo la Busega, Dk Raphael Chegeni kutoonekana katika msafara ulioenda kumlaki alipowasili na pia kutoonekana kwenye mkutano wa hadhara kwenye jimbo hilo ambalo makada wanne wa CCM wamefungua kesi kumpinga mgombea wa CCM, Dk Charles Tizeba.

Kikwete alisema kuwa walioshindwa hawana budi kuiga mfano wake kwa kuwa baada ya kushindwa na Benjamin Mkapa mwaka 1995 kuwania tiketi ya CCM ya kugombea urais, alivumilia na mwaka 2005 akapata nafasi hiyo kwa ushindi wa kishindo.

Kikwete aliongoza awamu ya kwanza ya kura za maoni za kutafuta mgombea urais wa CCM mwaka 1995, lakini katika awamu ya pili aliangushwa na Benjamin Mkapa ambaye baadaye alishinda uchaguzi na kuwa rais wa serikali ya awamu ya tatu.

Kikwete aliingia tena kwenye kinyang'anyiro cha kutafuta urais kwa tiketi ya CCM na kushinda kwa kishindo kwenye kura za maoni za chama hicho mwaka 2005.
 
Hapana ilikuwa ni Iringa pale kwenye stand ya mabasi ya Ipogolo. Sisi m kwa kukos sera sasa wana kiwewe na wanatafuta kuleta uvunjifu wa amani kila mahali katika nchi hii.
Ana bahati maana walitaka kuchomoa ndani ya kigari chake kama sio polisi kumsaidia.
Ebana poa,nashukuru.:becky:
 
Back
Top Bottom