Wafanyakazi washinikiza FAO la kujitoa

mgomba101

JF-Expert Member
Oct 21, 2011
1,817
706
WAFANYAKAZI wa migodi wametaka Sheria ya Mifuko ya Hifadhi ya Jamii (SSRA) irudishwe bungeni kwenye mkutano ujao ili kipengele cha fao la kujitoa kiondolewe mara moja.

Mbele ya wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Huduma za Jamii jana, wafanyakazi hao walisema kuwa kupelekwa sheria katika Bunge lijalo kutasaidia kupata haki na si kusubiri miaka 55 wakati migodi mingine imeanza kufungwa.

Mwakilishi wa Katibu wa Chama Wafanyakazi wa Migodi na Viwanda Tanzania (Tamiko), Benjamin Dotto, alisema kuwa sheria hiyo ni kandamizi kwa wafanyakazi wa migodi huku fedha yao ikitumika kutekeleza miradi ya serikali ambayo haina faida kwa wafanyakazi.

Dotto alisema kuwa wafanyakazi wa migodi wanafanya katika mazingira magumu hali ambayo fedha zinaweza kuwasaidia katika maisha kutokana na athari zinazotokana na sumu ya migodi, kwamba hawana uwezo wa kufika miaka hiyo kama sheria inavyosema.

Aliongeza kuwa msimamizi wa mifuko ya hifadhi ya jamii atokane na wafanyakazi ili aweze kusimamia haki na sheria zinazomnufaisha mfanyakazi.

“Wafanyakazi wa migodi wako katika mazingira magumu kutokana na kazi wanazofanya ambapo hawawezi kusubiri miaka hiyo ambayo sheria hiyo inataka huku wakiwa wameathirika na migodi,” alisema Dotto.

Mwenyekiti wa Kamati ya Wachimba Migodi, Joseph Mgire, alisema kuwa amani itatoweka kama sheria hiyo haitatekelezwa katika wakati muafaka.

Mgire alisema kuwa wafanyakazi wa migodi wako katika mikataba ambayo haieleweki kutokana na makampuni hayo wakati wowote yanaweza kufungwa na kulazimika kusubiri miaka 55 kuweza kupata mafao yao.
 
Ni wakati muafaka kwa wafanyakazi wote nchini kuungana pamoja kupinga sheria hii ya kipuuzi.
 
sijui tunangoja nini! na kilaaniwe chama cha mafisadi! nangoja kipenga kilie, nitakuwa wa kwanza barabarani
 
Alafu nikimwangalia mwangalia hivi kabaka, naona kama analipepo la kutokubali sheria hii irudi. Yupo tayari kuipigania mpaka tone la mwisho la damu. Kwa hiyo hii sheria ikirudi labda 2015.
 
Mbona ,wafanyakazi wa Migodi ndiyo wanalalamika peke yao, Wafanyakazi wa idara zingine vip?
 
wawakilishi wetu, wabunge, hawakuwa makini katika kupitisha sheria hiyo. pili, baadhi ya watu wasiopenda maendeleo ya wafanyakazi katika nchi hii walichomeka vipengele ambavyo havikuwemo awali na wameonekana mashujaa!!!!!!!!
 
Binafsi siku ya jana nimesikitika sana!

Yaani wafanyakaza wa migodini tuu ndiyo waliojitokeza kutetea fao la kujitoa ?tena kwa kuchangishana

Yaani wafanyakazi wa Tanzania huu unyonge na uoga ktk kutetea maslahi yetu sijui utaisha lini?
 
ccm na serikali yake wasiporejesha fao la kujitoa watashuhudia maandamano ambayo hawajawahi kuyaona. watajuta. Maandamano yakigoma yatafuatwa na migomo ya wafanyakazi. wasituchezee.
 
wawakilishi wetu, wabunge, hawakuwa makini katika kupitisha sheria hiyo. pili, baadhi ya watu wasiopenda maendeleo ya wafanyakazi katika nchi hii walichomeka vipengele ambavyo havikuwemo awali na wameonekana mashujaa!!!!!!!!
mkuu nilimsikia mnyika JJ akisema jamaa walichomeka kipengele hicho baada ya kupitishwa bungeni na kupeleka kwa mkulu kumwaga wino,
viongozi wetu ndo wanatusaliti.
hapa inabodi wafanyakazi wote tokamae watupe haki zetu.

mbona fao la wabunge hawasubir miaka 55? wao miaka 5 tu wanachukua!!!!!!!!
 
Back
Top Bottom