Wadaiwa sugu benki ya CRDB wataka Dr. Kimei asijiuzulu

Dickson Mpemba

JF-Expert Member
Jan 21, 2010
353
151
Nimepokea taarifa za baadhi ya wanahisa wenzangu wanaomba Dr Kimei aendelee kama Mkurugenzi Mtendaji kwa mshangao mkubwa na masikitiko.

1. Dr Kimei amekua mkurugenzi mtendaji wa CRDB kwa takribani miaka 20 sasa.

Yaani toka muhula wa kwanza wa Mkapa, mihula miwili ya Kikwete na sasa muhula wa kwanza wa Magufuli. Yaani toka Gavana Dr Idris Rashid, Mpaka Dr Balali, Mpaka Prof Ndulu na sasa Prof Luoga. Yaani toka wakati wa benki zisizo zaidi ya 10 mpaka sasa mabenki ya 57. Yaani toka wakati simu ni Tritel na TTCL mpaka sasa enzi za Mpesa, Tigo pesa na airtel money.

Hili sio jambo zuri kwa utamaduni wa kikampuni na utawala bora (Corporate Culrure and Governance). Kampuni hupaswa kua na utofauti wa menejimenti wa muda hadi muda kwa manufaa ya kibiashara na hata katika misingi ya utawala bora wa uendeshaji.

Nchi sio Benki. Lakini Hata katiba za nchi na taasisi mbali mbali kidemokrasia zinatambua hili. Hutoa nafasi kwa mtu kurudia uongozi mara kadhaa na kisha anapisha wengine. Ukomo wa muda katika uongozi flani na kuleta uongozi mpya kabisa ni kama kubonyeza refresh ama kuzima na kuwasha upya gari. Gari hili la CRDB kwa miaka 20 halijawahi kuzimwa ili tufungue mbele na tuchunguze vizuri chini ya boneti. Je? injini za mikakati na mauzo ziko sawa ama ni mbwembwe na uzoefu wa dereva unalolikongoja mbele. Je? breki za utawala bora na misingi ya usimamizi wa fedha zinafanya kazi ama ufundi na umahiri wa dereva ndio unatawala? Je hali ya ufanisi wa injini ni kama rangi nzuri za matangazo lukuki na nyimbo bwerere tunazoona kwa nje ya gari?

Bila kubadilisha uongozi wanahisa wenzangu tutajuaje kama kuna hizo shida na kuzitatua?

2. Bila kushangaza, na kwa kuegemea kabisa CRDB ni kati ya benki zimekua na viashiria vya kutokua na utawala bora mzuri. Jumla ya Mikopo mibaya ya CRDB peke yake ni TZS 459 Bil asilimia 14.54 ya mikopo yao yote. Hii ni juu ya kikomo cha asilimia 5 kilichowekwa na BOT. Robo ya mikopo isiolipika ya soko lote ni ya CRDB peke yake.

Misingi ya mikopo mibovu haichezi mbali na utawala bora wa mfumo mzima wa ukopeshaji. Leo tunashangilua uongozi huu uendelee zaidi?

3. Mkakati wa benki hii hauleweki eleweki. Baada ya mwanzo mzuri sana na mageuzi makubwa sifa na mafanikio haya yakazaa kubweteka na ubeberu. Zikaja EPA, Ikaja Mikopo ya mashaka kwenye kilimo hasa Pamba na matatizo mengineyo. Kwa sasa wapo kwenye kila kitu bila hasa mantiki thabiti ya ufanisi. Mara waje na bidhaa hii mara ile. Mara wajenge mabranch kisiasa na kuongeza mabranch kipindi wenzau wanapunguza. Mara wako china desk, mara hiki mara kile.

Ndugu wanahisa wenzangu wa CRDB bila shaka Dr Kimei ametuoa sehemu flani na kuchangia sana ukuaji na historia ya benki yetu. Neno kuu hapa ni "yetu", benki inapasa kuwa yetu na si yake (japokua inasemekana ana hisa kwa mbadala). Tunahitaji Kiongozi mpya mwenye mkakati mahiri zaidi kutupeleka mbele. Kama bodi ya CRDB 1998 ingekomaa na wakuregenzi hao hao kwa maslahi binafsi ama maono finyu tungeonja wapi matunda ya kazi za Dr Kimei. Na je CRDB isiwe na maisha baada ya Kimei, la hasha!

Sasa basi kazi yake nzuri au la iizinishwe na kujaribiwa kwa kutazamwa kutumia nyakati asiekuwepo yeye kama kiongozi.

Apishe na ajikite kutuletea jembe haswa. Si la kuficha maovu yake bali la kupeleka taasisi hii nyeti sana kwa maendeleo ya Tanzania Juu na juu zaidi. Akuze mitaji yetu wanahisa.

Nawasilisha.
 
watu wanahofia hisa zao bana...
Hisa zinalindwa na perfomance na faida siyo Bad loan na madeni yasiyolipika kwa sababu watu walikopeshwa kirafiki rafiki bila kufuata taratibu zinazostahili. Mfano bank valuers wanapo over value collateral na kupelekea hasara tunazoziona sasa kwani watu wanaacha makusudi ku service mikopo yao na Bank ikiweka sokoni dhamana hizo wanashindwa ku recover hata nusu ya pesa zilizokopwa.
 
Hisa zinalindwa na perfomance na faida siyo Bad loan na madeni yasiyolipika kwa sababu watu walikopeshwa kirafiki rafiki bila kufuata taratibu zinazostahili. Mfano bank valuers wanapo over value collateral na kupelekea hasara tunazoziona sasa kwani watu wanaacha makusudi ku service mikopo yao na Bank ikiweka sokoni dhamana hizo wanashindwa ku recover hata nusu ya pesa zilizokopwa.
Msingi mkubwa wa kulinda na kukua kwa hisa ni confidence. Na confidence hiyo inaweza kusababishwa na uwepo wa management inayoaminika na soko.
 
Madeni yasiyolipika (bad debts) ni lugha tu ya kihasibu (financial rhetoric) yani deni lililozidi miezi mitatu, mwaka na zaidi kutegemeana na policy ya kampuni. Lakini kiuhalisia madeni hayo yanalipika hasa pale benki itapoamua kuuza dhamana ya defaulers ili kulipia deni. So wanahisa na depositors msiwe na wasi wasi. Bado fedha zenu ziko salama kwa kuwa asilimia kubwa ya madeni haya yametokana na secured loans.
 
Madeni yasiyolipika (bad debts) ni lugha tu ya kihasibu (financial rhetoric) yani deni lililozidi miezi mitatu, mwaka na zaidi kutegemeana na policy ya kampuni. Lakini kiuhalisia madeni hayo yanalipika hasa pale benki itapoamua kuuza dhamana ya defaulers ili kulipia deni. So wanahisa na depositors msiwe na wasi wasi. Bado fedha zenu ziko salama kwa kuwa asilimia kubwa ya madeni haya yametokana na secured loans.
Kuna technical term hapo moja mleta mada kaitumia kasema wathaminishaji wana ' over value collateral'. Mtu ana nyumba ya mil 20 lkn afisa mikopo anaandika nyumba ina thamani ya mil 100 sababu tu anajua kuna percent yake,hiyo ni kweli hata mimi kuna jamaa namjua alikuwa akifanya hiyo michezo kwa benki siku ya mwisho anawaachia nyumba wanauza .
Anachoongea jamaa ni kweli hisa zao haziko mikoni salama
 
Kuna technical term hapo moja mleta mada kaitumia kasema wathaminishaji wana ' over value collateral'. Mtu ana nyumba ya mil 20 lkn afisa mikopo anaandika nyumba ina thamani ya mil 100 sababu tu anajua kuna percent yake,hiyo ni kweli hata mimi kuna jamaa namjua alikuwa akifanya hiyo michezo kwa benki siku ya mwisho anawaachia nyumba wanauza .
Anachoongea jamaa ni kweli hisa zao haziko mikoni salama
Noted!
 
Kuna technical term hapo moja mleta mada kaitumia kasema wathaminishaji wana ' over value collateral'. Mtu ana nyumba ya mil 20 lkn afisa mikopo anaandika nyumba ina thamani ya mil 100 sababu tu anajua kuna percent yake,hiyo ni kweli hata mimi kuna jamaa namjua alikuwa akifanya hiyo michezo kwa benki siku ya mwisho anawaachia nyumba wanauza .
Anachoongea jamaa ni kweli hisa zao haziko mikoni salama
Hii ikifanyika na valuer wa Crdb na mteja akapewa mamilioni ya fedha na akashindwa kurejesha mkopo na bank ikakuta hakuna cha kuuza ili kurejesha hizo fedha ni nini hatima yake. Nani wa kushitakiwa au hakuna kesi?
 
Ukiachilia mbali NMB, bank inayo fata kwa performance nzuri ni CRDB, kama kweli na wewe ni mwana HISA wa hiyo bank, sidhani kama ungependa ku risk pesa zako kwa kumleta CEO mpya wakati kibiashara wewe kama mwana hisa, gawio lako lipo vizuri. ITV hawaja badiri managing director kwa muda mrefu sana, yaani nimekua namsikia Ms. Joyce Muhavile for years this is to say, Reginald Abraham Mengi anacho angalia ni nini anapata kutokana na uwekezaji wake, habadiri tu mtu eti kwasababu anataka new figure, anaweza kubadiri mtu na biashara ikafanya vizuri zaidi but again, unaweza kubadiri MD halafu biashara ikaporomoka so kubadiri uongozi kwenye taasisi ambazo sio za kisiasa wala sio sifa, ni UFANISI
 
Kuna technical term hapo moja mleta mada kaitumia kasema wathaminishaji wana ' over value collateral'. Mtu ana nyumba ya mil 20 lkn afisa mikopo anaandika nyumba ina thamani ya mil 100 sababu tu anajua kuna percent yake,hiyo ni kweli hata mimi kuna jamaa namjua alikuwa akifanya hiyo michezo kwa benki siku ya mwisho anawaachia nyumba wanauza .
Anachoongea jamaa ni kweli hisa zao haziko mikoni salama
Hisa haziko salama wakati ukitoa TBL, CRDB ndiyo kampuni inayoperform vizuri DSE..

Watanzania mnachotwa sana na blah blah na majungu ya kwenye mitandao
 
miaka 20 kweli katika nchi ya watu milion 50...

hata kama una perform wapishe wengine nao waonyeshe uwezo wao..
 
Ukiachilia mbali NMB, bank inayo fata kwa performance nzuri ni CRDB, kama kweli na wewe ni mwana HISA wa hiyo bank, sidhani kama ungependa ku risk pesa zako kwa kumleta CEO mpya wakati kibiashara wewe kama mwana hisa, gawio lako lipo vizuri. ITV hawaja badiri managing director kwa muda mrefu sana, yaani nimekua namsikia Ms. Joyce Muhavile for years this is to say, Reginald Abraham Mengi anacho angalia ni nini anapata kutokana na uwekezaji wake, habadiri tu mtu eti kwasababu anataka new figure, anaweza kubadiri mtu na biashara ikafanya vizuri zaidi but again, unaweza kubadiri MD halafu biashara ikaporomoka so kubadiri uongozi kwenye taasisi ambazo sio za kisiasa wala sio sifa, ni UFANISI
Mkuu ITV unaiona ina maendeleo gani,program za kizee,graphics za mwaka arubaini na saba,logo ya mwaka tisini,ni sababu tu watazamaji wengi wa hyo chanel nao wanafanana nayo na kinachowasaidia ni ile kuwa na watangazaji wazuri ingawa wengi wao wanakimbilia kwenye vyombo vyengine,ila kizazi cha sasa hakuna anayeangalia hiyo stesheni,taarifa yao ya habari ni kama tbc tu,ni kuonyesha mawaziri na watendaji wa serikali wakizindua miradi na ugomvi wa wakulima na wafugaji,wanasavaivu sababu ya ukongwe tu.
 
Mkuu ITV unaiona ina maendeleo gani,program za kizee,graphics za mwaka arubaini na saba,logo ya mwaka tisini,ni sababu tu watazamaji wengi wa hyo chanel nao wanafanana nayo na kinachowasaidia ni ile kuwa na watangazaji wazuri ingawa wengi wao wanakimbilia kwenye vyombo vyengine,ila kizazi cha sasa hakuna anayeangalia hiyo stesheni,taarifa yao ya habari ni kama tbc tu,ni kuonyesha mawaziri na watendaji wa serikali wakizindua miradi na ugomvi wa wakulima na wafugaji,wanasavaivu sababu ya ukongwe tu.
Swali ni je; ITV inakimbiza mjini au laa!?
 
Swali ni je; ITV inakimbiza mjini au laa!?
Keeping up with the kardashians inakimbiza mjini na hivi sasa ni season ya 14.kukimbiza is not equal to ubora.nadhani inakimbiza zaidi shamba huko na sio mjini na huko nako ni kutokana na mazoea
 
Keeping up with the kardashians inakimbiza mjini na hivi sasa ni season ya 14.kukimbiza is not equal to ubora.nadhani inakimbiza zaidi shamba huko na sio mjini na huko nako ni kutokana na mazoea
Sijui takwimu unazo tumia mwenzangu ni zipi? Ujue sometimes unaweza kua unakipenda kitu au unakichukia wewe binafsi then usiwe mpinzani au mahaba tu kwa vile wewe unakipenda kitu hicho au unakichukia; super brand kwa upande wa TV stations bado ITV inaongoza na kwa upande wa radio ni clouds, hao ni wataalamu baada ya kufanya utafiti wao (vigezo walivyo tumia mi na wewe hatujui) ndio wakaja na matokeo hayo. Uipende au uichukie hilo sio suala langu. Bishana na takwimu sasa. Kuhusu kukimbiwa na wafanyakazi hilo wala sio jambo la AJABU, hakuna kampuni nzuri duniani eti wafanyakazi wake eti hua hawaachi kazi, hiyo kawaida sana. Hivi unajau mfungaji bora wa ligi mwaka hu amekua anakwenda na kurudi Simba mara kadhaa!? Hi ni kwasababu ya maslahi; sitashangaa nikisikia Simba wamemsajiri Kaseja tena mwaka hu
 
Back
Top Bottom