SAYVILLE
JF-Expert Member
- Mar 25, 2010
- 5,130
- 7,899
Bingwa wa mashindano ya AFCON 2023 anachukua zawadi nono ambayo haijawahi kufikiwa ya dola milioni 7, sawa na shilingi bilioni 17 na milioni 500.
Kabla mashindano ya AFCON 2023 hayajaanza, wachezaji wa South Africa "Bafana Bafana" waliingia makubaliano maalumu na Chama cha Soka cha Afrika Kusini (SAFA). Katika makubaliano hayo, walikubaliana kuwa wachezaji wa South Africa hawatapokea wala kudai posho yoyote ile ya mashindano ILA ikitokea kuwa South Africa wamechukua ndoo ya AFCON 2023, basi zawadi yote wanachukua wao wachezaji.
Hii ni kamari kubwa sana waliyoifanya wachezaji wa South Africa. Sijajua imechagizwa na nini, kwamba hawahitaji sana pesa, au ni uzalendo mkubwa walio nao kwa taifa lao, au ni ukata uliopo kwenye chama chao cha soka au ni kujiamini sana kwamba watachukua ubingwa au ni kamari tu ya kuhakikisha kuwa wanapata pesa nyingi inavyowezekana kutokana na mashindano haya. Nadhani jibu lipo mahali fulani hapa.
Pia najiuliza, hivi viongozi wa SAFA hawakuingia na tamaa wakijua hili lina uwezekano wa kutokea na maokoto yote yatabebwa na wachezaji halafu wao viongozi wa SAFA pamoja na serikali hawataambulia kitu? Au na viongozi wao nao ni wazalendo wanaona Ubingwa ndiyo muhimu kuliko vingine vyote?
Nadhani kuna faida kubwa ya uamuzi walioufanya. Kwanza unawapa hali fulani ya kutoridhika na matokeo madogo madogo. Kuna wachezaji ukishampa milioni 10 ya posho ya lazima, akajua hii inamtosha kuja kumalizia nyumba yake kule nanihii, basssiiii, shughuli yake uwanjani imeishia hapo. Atakwambia, huku akiungwa mkono na wachaa mbuzi na chawa kwamba, kwanza ndoto za ubingwa hatakiwi kuwa nazo maana hawezi kushindana na wachezaji wa PSG, Bayern Leverkusen na Man U.
Ila ona kinachoendelea sasa, Bafana Bafana haooo wanazidi kusonga mbele na wachezaji wao local wa Mamelodi Sundowns na Orlando Pirates, hawa hawa wanaocheza kila siku na TP Mazembe na Simba kwenye CAF Champions League au na Sekhukhune United na Polokwane City kwenye ligi yao ya ndani.
Wachezaji wa South Africa wangeweza kusema badala ya kurisk kukosa vyote, wachukue posho, halafu waingie makubaliano ya kugawana zawadi itakayopatikana kama wanavyofanya wengine (kumbuka kuna zawadi tokea hatua ya robo fainali ambayo kwa makubaliano haya sina uhakika kama wachezaji wa South Africa watazigusa bila kuchukua ubingwa wenyewe), lakini wao wameona ni ubingwa or nothing!
Nani aliwaroga wachezaji wa South Africa hadi wakachukua maamuzi haya ya kiduwanzi? Kwa kumalizia tu, kwa mahesabu ya haraka haraka, zawadi ya bingwa ya shilingi bilioni 17 na milioni 500 ukiigawa kwa watu 30 inakuja kama milioni 580 hivi na ushenzi. Hii siyo pesa mbaya sana ingawa kwa Mama yangu wa kule Muleba atasema hii ni pesa ya mboga tu. Kwangu mimi hii ndiyo aina ya betting ninayopenda kufanya.
Haki zote za maandiko haya zimehifadhiwa.
Kabla mashindano ya AFCON 2023 hayajaanza, wachezaji wa South Africa "Bafana Bafana" waliingia makubaliano maalumu na Chama cha Soka cha Afrika Kusini (SAFA). Katika makubaliano hayo, walikubaliana kuwa wachezaji wa South Africa hawatapokea wala kudai posho yoyote ile ya mashindano ILA ikitokea kuwa South Africa wamechukua ndoo ya AFCON 2023, basi zawadi yote wanachukua wao wachezaji.
Hii ni kamari kubwa sana waliyoifanya wachezaji wa South Africa. Sijajua imechagizwa na nini, kwamba hawahitaji sana pesa, au ni uzalendo mkubwa walio nao kwa taifa lao, au ni ukata uliopo kwenye chama chao cha soka au ni kujiamini sana kwamba watachukua ubingwa au ni kamari tu ya kuhakikisha kuwa wanapata pesa nyingi inavyowezekana kutokana na mashindano haya. Nadhani jibu lipo mahali fulani hapa.
Pia najiuliza, hivi viongozi wa SAFA hawakuingia na tamaa wakijua hili lina uwezekano wa kutokea na maokoto yote yatabebwa na wachezaji halafu wao viongozi wa SAFA pamoja na serikali hawataambulia kitu? Au na viongozi wao nao ni wazalendo wanaona Ubingwa ndiyo muhimu kuliko vingine vyote?
Nadhani kuna faida kubwa ya uamuzi walioufanya. Kwanza unawapa hali fulani ya kutoridhika na matokeo madogo madogo. Kuna wachezaji ukishampa milioni 10 ya posho ya lazima, akajua hii inamtosha kuja kumalizia nyumba yake kule nanihii, basssiiii, shughuli yake uwanjani imeishia hapo. Atakwambia, huku akiungwa mkono na wachaa mbuzi na chawa kwamba, kwanza ndoto za ubingwa hatakiwi kuwa nazo maana hawezi kushindana na wachezaji wa PSG, Bayern Leverkusen na Man U.
Ila ona kinachoendelea sasa, Bafana Bafana haooo wanazidi kusonga mbele na wachezaji wao local wa Mamelodi Sundowns na Orlando Pirates, hawa hawa wanaocheza kila siku na TP Mazembe na Simba kwenye CAF Champions League au na Sekhukhune United na Polokwane City kwenye ligi yao ya ndani.
Wachezaji wa South Africa wangeweza kusema badala ya kurisk kukosa vyote, wachukue posho, halafu waingie makubaliano ya kugawana zawadi itakayopatikana kama wanavyofanya wengine (kumbuka kuna zawadi tokea hatua ya robo fainali ambayo kwa makubaliano haya sina uhakika kama wachezaji wa South Africa watazigusa bila kuchukua ubingwa wenyewe), lakini wao wameona ni ubingwa or nothing!
Nani aliwaroga wachezaji wa South Africa hadi wakachukua maamuzi haya ya kiduwanzi? Kwa kumalizia tu, kwa mahesabu ya haraka haraka, zawadi ya bingwa ya shilingi bilioni 17 na milioni 500 ukiigawa kwa watu 30 inakuja kama milioni 580 hivi na ushenzi. Hii siyo pesa mbaya sana ingawa kwa Mama yangu wa kule Muleba atasema hii ni pesa ya mboga tu. Kwangu mimi hii ndiyo aina ya betting ninayopenda kufanya.
Haki zote za maandiko haya zimehifadhiwa.