bryan2
JF-Expert Member
- Jun 8, 2016
- 3,323
- 4,667
Tanzania nakupenda nchi yangu hongereni sana vijana wetu hakika leo mmejitoa kila mtu kafanya majukumu yake, hongera sana benchi zima la ufundi hongereni mashabiki mliojitokeza kuipa joto Taifa Stars ukubwa wa ligi yetu hakika unaanza kuonekana mpaka timu ya Taifa.
Uganda Cranes ni kati ya timu zinazotusumbua sana ukanda wetu, kwa kifupi ndio wakali wa soka kwa ukanda huu hatuna historia nzuri sana tunapokutana nao wametufunga michezo mingi zaidi yetu.
Hakika huu ni mwanzo mzuri wa benchi la ufundi chini ya kocha mpya japo baada ya kutangaza kikosi kama kawaida kuna wapiga kelele waliibuka na kuanza kujifanya nao ni makocha wa Pro UEFA, wapo waliotaka kuona wachezaji wao wanaitwa na kuzusha taarifa zao za kimbeya mitandaoni ila kocha alibaki na misimamo yake.
Yupo mchambuzi mmoja kwa asilimia kubwa leo siku nzuri baada ya Taifa Stars kushinda kwa kifupi alikuwa anataka Stars ifungwe ili aibuke na hoja zake zisizo na mashiko, huyu ndio mchambuzi aliyewaaminisha Watanzania kocha kakosea kutowaita Shomari na Tshabalala hata kufikia kusema kocha ametaka hao jamaa waitwe haraka Taifa stars baada ya picha kusambaa kocha akiwa na vijana hao.
My point is, hawa wachambuzi mimi nawaita wapiga kelele habari zao tuwe tunazisoma kama magazeti ya udaku tu hawawezi kukupa sababu yoyote ya kiufundi na kuishia kuandika udaku tu, mbaya zaidi huyo mchambuzi sio kwamba yupo kwa maslahi ya taifa bali ni mapenzi yake kwa timu wanayotoka hao wachezaji.
Hakika siyo siku nzuri kwake.
Uganda Cranes ni kati ya timu zinazotusumbua sana ukanda wetu, kwa kifupi ndio wakali wa soka kwa ukanda huu hatuna historia nzuri sana tunapokutana nao wametufunga michezo mingi zaidi yetu.
Hakika huu ni mwanzo mzuri wa benchi la ufundi chini ya kocha mpya japo baada ya kutangaza kikosi kama kawaida kuna wapiga kelele waliibuka na kuanza kujifanya nao ni makocha wa Pro UEFA, wapo waliotaka kuona wachezaji wao wanaitwa na kuzusha taarifa zao za kimbeya mitandaoni ila kocha alibaki na misimamo yake.
Yupo mchambuzi mmoja kwa asilimia kubwa leo siku nzuri baada ya Taifa Stars kushinda kwa kifupi alikuwa anataka Stars ifungwe ili aibuke na hoja zake zisizo na mashiko, huyu ndio mchambuzi aliyewaaminisha Watanzania kocha kakosea kutowaita Shomari na Tshabalala hata kufikia kusema kocha ametaka hao jamaa waitwe haraka Taifa stars baada ya picha kusambaa kocha akiwa na vijana hao.
My point is, hawa wachambuzi mimi nawaita wapiga kelele habari zao tuwe tunazisoma kama magazeti ya udaku tu hawawezi kukupa sababu yoyote ya kiufundi na kuishia kuandika udaku tu, mbaya zaidi huyo mchambuzi sio kwamba yupo kwa maslahi ya taifa bali ni mapenzi yake kwa timu wanayotoka hao wachezaji.
Hakika siyo siku nzuri kwake.