Smokey D
JF-Expert Member
- Jan 30, 2013
- 2,631
- 2,086
Watu wanaenda kutoa shukrani kwa wazee na mizimu yao wewe unataka uende nao amini nakuambia huwa migombani wanaenda wanafamilia tu matambiko na umwagaji damu unafanyika wewe utabaki jikoni ukichochea moto wa kisusio.kama una rafiki mchaga...muombe,mlilie December akiwa anaenda kwao na ww uende hata kwa gharama zako uone wanapokutana,majadiliano,mazungumzo,Target ktk biashara ndani ya mwaka mzima,ukifanikiwa kusikiliza tu amini nakwambia ukirudi utakua mpya kama upo sirias na maisha kuna kitu utakua umeongeza
Ila wachaga ni watu wakuhastle sana na nidhamu ya pesa huo ndio utafutaji wewe kama unatumia pesa kiholela ndugu mafanikio utayaskia kwa wenzako tu
Na hawa watu ninao wajua wanaumwa vidonda vya tumbo wako radhi wajinyime kula ili afanikishe jambo lake.
Kuna mmoja alianguka chini na kuzimia mida ya saa kumi, tukamwaisha hospital baada ya vipimo nesi anatuambia tutafute mtori tukaleta akapewa na drip za kutosha jamaa akawa fiti, kumbe ni njaa ilimwangusha na mfukoni alikuwa na kama laki nne na chenchi hivi alikuwa mfanyabiashara ya hardware.