Wabunge waliotumia huduma za 'VIP Class' badala ya 'Business Class' kwenye Ndege watakiwa kujilipia

BARD AI

JF-Expert Member
Jul 24, 2018
3,379
8,123

Spika wa Bunge, Dkt. Tulia Ackson amesema ofisi yake tayari imepokea majina ya Wabunge waliofanya safari za nje ya Nchi na kukiuka maelekezo ya madaraja waliyopaswa kutumia hivyo wataandikwa barua ili walipe gharama hizo.

Kwa mujibu wa Spika, Wabunge wanastahili kupewa tiketi za 'Business Class' na huduma zilizopo chumba cha daraja hilo hilo na sio VIP ambayo ina gharama za ziada na Ofisi ya Katibu wa Bunge imekuwa ikitoa maelekezo kuhusu matumizi ya madaraja hayo.
 
Mbona wanakuwa hawana huruma na wapiga kura wao? Wengine hawana aibu majimbo yao yamechoka huduma za kijamii ni mbovu halafu wanataka kulipiwa gharama kubwa
 
View attachment 2577279
Spika wa Bunge, Dkt. Tulia Ackson amesema ofisi yake tayari imepokea majina ya Wabunge waliofanya safari za nje ya Nchi na kukiuka maelekezo ya madaraja waliyopaswa kutumia hivyo wataandikwa barua ili walipe gharama hizo.

Kwa mujibu wa Spika, Wabunge wanastahili kupewa tiketi za 'Business Class' na huduma zilizopo chumba cha daraja hilo hilo na sio VIP ambayo ina gharama za ziada na Ofisi ya Katibu wa Bunge imekuwa ikitoa maelekezo kuhusu matumizi ya madaraja hayo.
Hata hiyo business class ni bado ni hasara kwa nchi.nadhani ingeweka kwa viongozi wakuu wa mihimili tuu na wasaidizi wao wa karibu.raisi,makamu,waziri mkuu,katibu mkuu kiongozi ikulu. na wakuu wa mihimili mingine.

Mbona wengine tunapandaga nao vichater plane ambavyo havina classes na mambo yanakwenda vizuri tuu
 
Mbona wanakuwa hawana huruma na wapiga kura wao? Wengine hawana aibu majimbo yao yamechoka huduma za kijamii ni mbovu halafu wanataka kulipiwa gharama kubwa
Ubinafsi husababisha mimba mtoto anaezaliwa (mbunge) anakuwa mchoyo hawa ndio wabunge wetu. Hawajali kuhusu hali za wanao wawakilisha.

Angalia hata posho zao utaelewa, mtu mmoja aliwahi kusema ukitegemea mwanasiasa abadilishe maisha yako ni sawa na kusubiri meli airport.

Hawajali na hawatakaa wajali... Nchi ngumu hii tupambane pasipo kuwategemea wawakilishi wetu.

Cheers!!
 
Back
Top Bottom