Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 50,956
- 22,148
Wabunge waache kuendekeza vitendo vya uvunjaji wa sheria
Na Mhariri
29th May 2009
Jana vyombo kadha vya habari, viliripoti habari zikiwanukuu baadhi ya Wabunge wa Kamati ya Fedha na Uchumi wakieleza hofu yao kuhusiana na hatua ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT) kuidhibiti Taasisi ya upatu ya Development Entrepreniurship Community Initiatives (Deci).
Wabunge hao walisema kuwa uamuzi wa kuidhibiti taasisi hiyo, utawaweka wao (Wabunge) katika hali ngumu ya kisiasa katika Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika mwishoni mwa mwaka ujao.
Walijenga hoja yao iliyoonekana ikilenga kuwashawishi maofisa waandamizi wa BoT juzi wakati walipokutana nao kupokea ripoti ya mwelekeo wa bajeti ya mwaka ujao wa fedha 2009/2010, ili walegeze msimamo wao dhidi ya Deci.
Kimsingi, wabunge hao wengi kutoka chama tawala Chama Cha Mapinduzi (CCM) walitoa hoja hiyo ili wao na chama chao waonekane kuwa wanawajali Watanzania.
Kitendo hicho tunakichukulia kuwa baadhi ya Wabunge wanashindwa kutekeleza majukumu yao waliyopewa na Katiba ya nchi ya kushauri, kufuatilia na kukosoa utendaji mbovu wa serikali.
Tunashindwa kuelewa inakuwaje Wabunge wakadiriki kuingilia kati kutetea watuhumiwa wa kuvunja sheria za nchi wasichukuliwe hatua na taasisi husika kwa kutumia kisingizio cha Uchaguzi Mkuu wa mwakani?
Taarifa zilizoko ni kwamba Deci ilikuwa inaendesha shughuli zake kinyume cha sheria na shughuli hizo zikasimamishwa na serikali baada ya kubainika kuwa wananchi wengi wamepoteza fedha zao katika upatu.
Tusingependa kunukuu maneno yaliyotolewa na baadhi ya Wabunge hao walioonyesha kukerwa na hatua ya BoT, lakini Wabunge, tena wale ambao ni wajumbe wa Kamati ya Fedha na Uchumi, badala ya kuibebesha lawama BoT kwa kushindwa kusimamisha shughuli za Deci mapema, nao walikuwa na jukumu la kuihoji serikali baada ya kuona shughuli za Deci zikiendelea.
Kwa kuwa Wabunge wanaishi katika maeneo mbalimbali ya nchi yetu, bila shaka waliwaona wananchi wao wakishiriki katika upatu huo lakini hawakuchukua hatua za kuwapa tahadhali. Kwa hiyo kama ni lawama za kutokuwajibika kwa kutotoa taarifa basi hawawezi kujivua lawama hizo.
Kwa kuwa BoT imeingilia kati kwa ajili ya kuokoa fedha za wananchi hata kama imechelewa kuchukua hatua lakini ni jambo la busara kwa Wabunge kuliacha suala hilo kwa taasisi hiyo ambayo jukumu lake kubwa ni kusimamia mambo yote ya fedha nchini.
Tunawashauri Wabunge kuacha kutetea shughuli za Deci kwa kuhofia kushindwa katika uchaguzi wa mwakani bali waliache suala hilo kwa BoT na vyombo vya sheria. Wanaopaswa kulihofia hilo ni wale waliohusika kwa njia moja ama nyingine kuwashawishi wapigakura wao kujiunga katika upatu huo.
Kwa bahati mbaya imejengeka tabia mbaya kwa watu walioko katika nafasi mbalimbali za uongozi nchini kuweka pembeni sheria badala yake kutetea vitendo vya uvunjaji wa sheria hasa unapofika wakati wa uchaguzi kwa lengo la kujifanya kuwa wanawajali wananchi.
Kwa mfano, katika maeneo mengi ya mijiji, shughuli za biashara ambazo zinachafua mazingira zimerejea upya na ya viongozi wanasita kuchukua hatua wakidai wahusika waachwe kwa kuwa uchaguzi unakaribia.
Tunawashauri viongozi katika ngazi zote, wakiwemo Wabunge wetu kutekeleza wajibu wao kwa dhati bila kuhofia kwamba uchaguzi mkuu unakaribia kwa kuwa kufanya hivyo ni kukiuka wajibu na ni kinyume cha utawala wa sheria.
CHANZO: NIPASHE
Na Mhariri
29th May 2009
Jana vyombo kadha vya habari, viliripoti habari zikiwanukuu baadhi ya Wabunge wa Kamati ya Fedha na Uchumi wakieleza hofu yao kuhusiana na hatua ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT) kuidhibiti Taasisi ya upatu ya Development Entrepreniurship Community Initiatives (Deci).
Wabunge hao walisema kuwa uamuzi wa kuidhibiti taasisi hiyo, utawaweka wao (Wabunge) katika hali ngumu ya kisiasa katika Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika mwishoni mwa mwaka ujao.
Walijenga hoja yao iliyoonekana ikilenga kuwashawishi maofisa waandamizi wa BoT juzi wakati walipokutana nao kupokea ripoti ya mwelekeo wa bajeti ya mwaka ujao wa fedha 2009/2010, ili walegeze msimamo wao dhidi ya Deci.
Kimsingi, wabunge hao wengi kutoka chama tawala Chama Cha Mapinduzi (CCM) walitoa hoja hiyo ili wao na chama chao waonekane kuwa wanawajali Watanzania.
Kitendo hicho tunakichukulia kuwa baadhi ya Wabunge wanashindwa kutekeleza majukumu yao waliyopewa na Katiba ya nchi ya kushauri, kufuatilia na kukosoa utendaji mbovu wa serikali.
Tunashindwa kuelewa inakuwaje Wabunge wakadiriki kuingilia kati kutetea watuhumiwa wa kuvunja sheria za nchi wasichukuliwe hatua na taasisi husika kwa kutumia kisingizio cha Uchaguzi Mkuu wa mwakani?
Taarifa zilizoko ni kwamba Deci ilikuwa inaendesha shughuli zake kinyume cha sheria na shughuli hizo zikasimamishwa na serikali baada ya kubainika kuwa wananchi wengi wamepoteza fedha zao katika upatu.
Tusingependa kunukuu maneno yaliyotolewa na baadhi ya Wabunge hao walioonyesha kukerwa na hatua ya BoT, lakini Wabunge, tena wale ambao ni wajumbe wa Kamati ya Fedha na Uchumi, badala ya kuibebesha lawama BoT kwa kushindwa kusimamisha shughuli za Deci mapema, nao walikuwa na jukumu la kuihoji serikali baada ya kuona shughuli za Deci zikiendelea.
Kwa kuwa Wabunge wanaishi katika maeneo mbalimbali ya nchi yetu, bila shaka waliwaona wananchi wao wakishiriki katika upatu huo lakini hawakuchukua hatua za kuwapa tahadhali. Kwa hiyo kama ni lawama za kutokuwajibika kwa kutotoa taarifa basi hawawezi kujivua lawama hizo.
Kwa kuwa BoT imeingilia kati kwa ajili ya kuokoa fedha za wananchi hata kama imechelewa kuchukua hatua lakini ni jambo la busara kwa Wabunge kuliacha suala hilo kwa taasisi hiyo ambayo jukumu lake kubwa ni kusimamia mambo yote ya fedha nchini.
Tunawashauri Wabunge kuacha kutetea shughuli za Deci kwa kuhofia kushindwa katika uchaguzi wa mwakani bali waliache suala hilo kwa BoT na vyombo vya sheria. Wanaopaswa kulihofia hilo ni wale waliohusika kwa njia moja ama nyingine kuwashawishi wapigakura wao kujiunga katika upatu huo.
Kwa bahati mbaya imejengeka tabia mbaya kwa watu walioko katika nafasi mbalimbali za uongozi nchini kuweka pembeni sheria badala yake kutetea vitendo vya uvunjaji wa sheria hasa unapofika wakati wa uchaguzi kwa lengo la kujifanya kuwa wanawajali wananchi.
Kwa mfano, katika maeneo mengi ya mijiji, shughuli za biashara ambazo zinachafua mazingira zimerejea upya na ya viongozi wanasita kuchukua hatua wakidai wahusika waachwe kwa kuwa uchaguzi unakaribia.
Tunawashauri viongozi katika ngazi zote, wakiwemo Wabunge wetu kutekeleza wajibu wao kwa dhati bila kuhofia kwamba uchaguzi mkuu unakaribia kwa kuwa kufanya hivyo ni kukiuka wajibu na ni kinyume cha utawala wa sheria.
CHANZO: NIPASHE