Kalambo Junior
Senior Member
- Jul 15, 2011
- 127
- 23
Ingawa wabunge wa CCM,Alhamisi usiku walifanya kikao cha kamati ya chama kuweka mkakati wa kutoipinga bajeti ya wizara ya Nishati na Madini,lakini hali inaonyesha kuwa tofauti kabisa.Tayari, wabunge wengi wakiwamo wa CCM wametoa misimamo mikali dhidi ya bajeti hii tofauti na wizara nyingine ambazo zilipingwa na upinzani pekee.Zimesikika kauli kali za wabunge wa CCM kama vile"Hapa patachimbika" "Nitaunga mkono wapinzani kuwa serikali hii ni legelege","waziri amesema uongo" "waziri anapendelea miradi katika majimbo ya maswahiba wake"na siungi mkono hoja".Je katika hili hawa wabunge wa CCM wanamaanisha wanacho kiongea? kama ndio,je watakuwa ni wasaliti kwa serikali yao?.