mbingunikwetu
JF-Expert Member
- Feb 17, 2015
- 13,664
- 18,039
Kuna mambo mengine huwa yanakera sana!! Kama Rais Samia anaamini kwa dhati IMANI ya CCM kuwa binadamu wote ni sawa na kuwa kila mtu anastahili heshima ya kutambuliwa na kuthaminiwa utu wake, inakuwaje akaona kuwa watumishi wengine wanastahili mafao kwa kikokotoo cha asilimia 33% wakati wabunge wao wanakomba zote kwa kikokotoo cha asilimia 100%.
Hapo imani yake kama mwana CCM iko wapi? Utaaminije kuwa wanadamu wote ni sawa wakati mmoja unampa mafao asilimia 100% wakati mwingine unampa asilimia 33%, halafu utarajie kuwa huyu uliyempa asilimia 33% ataona unathamini utu wake sawa na huyu uliyempa asilimia 100%? Tuambizane ukweli hapo hakuna cha usawa wala nini zaidi ya upendeleo wa wazi! Suluhu ni moja tu, wote wapate asilimia 33% au wote wapate asilimia 100%.
Vinginevyo mama atuambie hawa wanaopata asilimia 100% wana ziada gani katika utu wao? na hawa wanaopata asilimia 33% wana upungufu gani katika utu wao??. Kama kikokotoo cha asilimia 33% kinafaa basi kifae kwa wote! na kama hakifai kisifae kwa wote!!
Poleni sana watumishi wa umma ambao mliokuwa PPF na NSSF kabla ya wote kuhamishiwa PSSSF maana MPAKA LEO mkistaafu mmekuwa mkipewa mafao kwa kikokotoo cha asilimia 25% wakati wenzenu waliokuwa LAPF na PSPF wanapata mafao kwa kikokotoo cha asilimia 50%, na serikali ilifumbia macho double standard hii!!
Hebu kwa wasiozijua imani na ahadi za wana ccm (ambao ndio waliounda serikali iliyoko madarakani) niwatupie hapa muone kama wenyewe wanazitekeleza au ni kiini macho:
AHADI ZA WANACHAMA WA CHAMA CHA MAPINDUZI
(1) Binadamu wote ni ndugu zangu na Afrika ni moja
(2) Nitaitumikia nchi yangu na watu wake wote
(3) Nitajitolera nafsi yangu kuondosha umaskini, ujinga, magonjwa na dhuluma.
(4) Rushwa ni adui wa haki, sitapokea wala kutoa rushwa.
(5) Cheo ni dhamana, sitatumia cheo changu wala cha mtu mwingine kwa faida yangu.
(6) Nitajielimisha kwa kadri ya uwezo wangu na kuitumia elimu yangu kwa faida ya wote.
(7) Nitashjirikiana na wenzangu wote kujenga nchi yetu.
(8) Nitasema kweli daima, fitina kwangu mwiko.
(9) Nitakuwa mwanachama mwaminifu wa CCM na raia mwema wa Tanzania na Afrika.
Karibuni kwa mjadala (bila matusi)!
Hapo imani yake kama mwana CCM iko wapi? Utaaminije kuwa wanadamu wote ni sawa wakati mmoja unampa mafao asilimia 100% wakati mwingine unampa asilimia 33%, halafu utarajie kuwa huyu uliyempa asilimia 33% ataona unathamini utu wake sawa na huyu uliyempa asilimia 100%? Tuambizane ukweli hapo hakuna cha usawa wala nini zaidi ya upendeleo wa wazi! Suluhu ni moja tu, wote wapate asilimia 33% au wote wapate asilimia 100%.
Vinginevyo mama atuambie hawa wanaopata asilimia 100% wana ziada gani katika utu wao? na hawa wanaopata asilimia 33% wana upungufu gani katika utu wao??. Kama kikokotoo cha asilimia 33% kinafaa basi kifae kwa wote! na kama hakifai kisifae kwa wote!!
Poleni sana watumishi wa umma ambao mliokuwa PPF na NSSF kabla ya wote kuhamishiwa PSSSF maana MPAKA LEO mkistaafu mmekuwa mkipewa mafao kwa kikokotoo cha asilimia 25% wakati wenzenu waliokuwa LAPF na PSPF wanapata mafao kwa kikokotoo cha asilimia 50%, na serikali ilifumbia macho double standard hii!!
Hebu kwa wasiozijua imani na ahadi za wana ccm (ambao ndio waliounda serikali iliyoko madarakani) niwatupie hapa muone kama wenyewe wanazitekeleza au ni kiini macho:
IMANI YA CCM
- Binadamu wote ni Sawa
- Kila mtu anastahili heshima ya kutambuliwa na kuthaminiwa utu wake
- Ujamaa na kujitegemea ndiyo njia pekee ya kujenga jamii ya watu walio sawa na huru
AHADI ZA WANACHAMA WA CHAMA CHA MAPINDUZI
(1) Binadamu wote ni ndugu zangu na Afrika ni moja
(2) Nitaitumikia nchi yangu na watu wake wote
(3) Nitajitolera nafsi yangu kuondosha umaskini, ujinga, magonjwa na dhuluma.
(4) Rushwa ni adui wa haki, sitapokea wala kutoa rushwa.
(5) Cheo ni dhamana, sitatumia cheo changu wala cha mtu mwingine kwa faida yangu.
(6) Nitajielimisha kwa kadri ya uwezo wangu na kuitumia elimu yangu kwa faida ya wote.
(7) Nitashjirikiana na wenzangu wote kujenga nchi yetu.
(8) Nitasema kweli daima, fitina kwangu mwiko.
(9) Nitakuwa mwanachama mwaminifu wa CCM na raia mwema wa Tanzania na Afrika.
Karibuni kwa mjadala (bila matusi)!