Wabunge kupiga kura ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu Pinda?

Kwa mahesabu ya haraka kwa wabunge wa CCM ni vigumu kutoa saini, ila hata kama wa CCM watapinga kimahesabu na kihalisia ukijumuisha wabunge wa CHADEMA 49 na wa CUF 35, saini 70 zinapatikana ambazo ni muhimu kuitisha kura ya imani kumuondoa Waziri Mkuu ambayo ni ya siri! Sasa kesho ni siku rasmi ya kupembenua mchele na mpunga tutege maskio na macho yetu kusikia na kuona CUF wataegemea wapi au watacheza namba ipi pinzani au tawala na mbali ya swala hili nyeti kwa Taifa tukumbuke Wabunge wa CUF wana bifu na Mizengo Pinda pale alipowakera kwa kuwaambia Wazanzibari Zanzibar si nchi, sasa tutafahamu vizuri kama kweli walikereka au ni zile siasa za changu changu chako chetu! Hili la uzembe wa Pinda katika serikali ya Jamhuri haliwahusu! Kesho hali halisi, itikadi na mrengo wa CUF kisiasa utajulikana ulipo au umefikia wapi haswa tunapotazama siasa za Upinzani Tanzania! Kesho CUF pia watajipambanua vizuri kama wao ni CCM B au CCM C kiufupi watasuka au kunyoa! Wazee wa Pemba wanawaangalia CUF msishangae M4C ikaitwa kule....ni hayo tu!
 
Waziri mkuu mwenyewe uso umekunjana muda wote. Hujui muda gani anacheka na muda gani amekasirika. I can imagine leo hii sura yake ikoje.
 
Naona shutuma zote za upungufu ulioibuliwa na CAG unaelekezwa kwa mtoto wa mkulima. Siyo haki. Tusome katiba ya JMT. Waziri Mkuu kama walivyo Mawaziri, Makatibu Wakuu, Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Mashirika ya Umma na wenyeviti wa Mabodi wote ni wateule wa Rais hata kama anashauriwa na WM. Baada ya uteuzi kufanyika mwenye mamlaka ya kikatiba kuwajibisha wateule wake ni Rais. Pengine tuna kumbukumbu fupi lakini wakati wa kipindi cha kwanza cha serikali hii, Waziri wa Utalii aliamua kumwajibisha Mkurugenzi wa Wanyama Pori. Jamaa yule alikataa na kukumbusha Waziri wake kuwa wote walikuwa wateule wa mamlaka moja na hivyo hakuwa na mamlaka juu yake. Cha kushangaza Waziri aliondoka kwenye wizara hiyo na kumwacha Mkurugenzi akidunda. Kwa hiyo tusimbebeshe mzigo usistahili mtoto wa mkulima. Msingi wa matatizo tunayoshuhudia ni Katiba yetu mbovu. Tukikubali hivyo tutaacha kukimbizan ana kivuli.

Sokoine na Mrema walikuwa hawajui katiba yetu?. Acha upuuzi wako.
 
kesho wabunge waoga watajifanya wagonjwa or wata sepa wasiudhulie kukwepa kuangusha saini!!!:A S-rap:
 
jaman inasikitisha,lakin inatia uchungu kwamba mtanzania mwenyewe anaepigiwa kelele kalala usingizi wa pono na kujifunika shuka la kijan hana habari.
mungu ibariki tanzania,
mungu wabariki wanaharakati wa kweli.
 
Orodha ya watakaoweka saini isambazwe WANANCHI WATUFAHAMU NA KUTUTOFAUTISHA. Siko tayari kuchanganywa na watu wabadhilifu wasiowajibika etu tu kwa sababu ya chama au mshahara wa MBunge!
 
Hata kama watanzania tunaonekana kuwa mataahira, nadhani mwisho wa ubwege wetu uwe huu na kuhakikisha Chama Cha Majambazi hakirejei. Cha mno ni kuandaa kesi dhidi ya mafisadi wakubwa kama hawa tutakapokuwa tumeangusha genge zima la majambazi.
 
usitegemee kitu toka CCM B juzi hapa wamepewa nafasi moja EALA kwa kupigiwa kura na wabunge woote wa CCM A; sasa kwa mantiki hiyo watarudisha fadhila ila itakuwa mbaya kwao haswa kuhusu swala zima la imani ya jamii kwao! we si umeona Prof. Mapumba na Mtatiro walivyo kimya hawajasema lolote mpaka sasa! Natabiri 2015 CUF hawapati hata kiti kimoja bara!
 
Naomba kuuliza swali hapa, Great Thinkers.

Hivi kweli tatizo ni Pinda au tatizo ni Kikwete? Nauliza hivi kwa sababu wakati wa sakata la Jairo, Pinda alishaashiria kwamba Jairo atajiuzulu lakini baada ya kuzungumza na Kikwete akaambiwa asubiri mpaka Kikwete arejee nchini. Sote tunajua yaliyotokea. Marehemu Sokoine na Kawawa waliwahi kuwa mawaziri wakuu chini ya utawala wa Mwalimu.

Kuna baadhi ya maamuzi ambayo walichukua bila kushauriana na Mwalimu na hata kama Mwalimu hakukubaliana nao lakini alikuwa na uungwana wa kutosha kuyaacha yaendelee. Mawaziri wanaotuhumiwa ubadhirifu wamewekwa pale na Kikwete, sidhani kama Pinda ana mamlaka yoyote ya kuwafukuza kazi bila idhini ya rais. Sasa Pinda akijiuzulu ndiyo iweje? Imwachie mlango Kikwete kukwepa lawama na kumchagua swahiba wake Asha Rose Migiro? Nasikia anasubiria sana kiti hicho.
 
wabunge wa ccm majasiri kama kina Filikunjombe watatoa na watawashawishi wenzao weeengi! sahihi 70 zitatosha!
 
usitegemee kitu toka CCM B juzi hapa wamepewa nafasi moja EALA kwa kupigiwa kura na wabunge woote wa CCM A; sasa kwa mantiki hiyo watarudisha fadhila ila itakuwa mbaya kwao haswa kuhusu swala zima la imani ya jamii kwao! we si umeona Prof. Mapumba na Mtatiro walivyo kimya hawajasema lolote mpaka sasa! Natabiri 2015 CUF hawapati hata kiti kimoja bara!
Kwa hiyo ina maana CUF wananunuliwa kwa bei ya Mbunge mmoja sio? siamini kaka duh kama ni hivyo basi tumekwisha si ajabu wanachama wake wakaendelea kujitoa...!
 
wabunge wa ccm majasiri kama kina Filikunjombe watatoa na watawashawishi wenzao weeengi! sahihi 70 zitatosha!

naelewa unachosema ila amini mida hii wabunge wa CCM wako vikaoni wanapewa jambajamba na subuthu yao wajaribu kutoa saini kwa hiyo sishangai kama wasipozitoa na pia kuna uwezekano mahudhurio yakawa hafifu mno kesho! Ikishindikana hata IGP anaweza kutumika kutangaza Al-Shabaab Dodoma kama si watu wa kutabiri matetemeko ya ardhi kutumika! Ila hata kama za CCM hazitatoka, za CUF je? zitaelekea wapi kama chama Pinzani?
 
Hapo ni mahali pazuri ambapo tumefikia kupima uwezo wa wabunge wetu kama wapo kwa maslahi ya umma au chama na binafsi.
 
Naomba kuuliza swali hapa, Great Thinkers. Hivi kweli tatizo ni Pinda au tatizo ni Kikwete? Nauliza hivi kwa sababu wakati wa sakata la Jairo, Pinda alishaashiria kwamba Jairo atajiuzulu lakini baada ya kuzungumza na Kikwete akaambiwa asubiri mpaka Kikwete arejee nchini. Sote tunajua yaliyotokea. Marehemu Sokoine na Kawawa waliwahi kuwa mawaziri wakuu chini ya utawala wa Mwalimu. Kuna baadhi ya maamuzi ambayo walichukua bila kushauriana na Mwalimu na hata kama Mwalimu hakukubaliana nao lakini alikuwa na uungwana wa kutosha kuyaacha yaendelee. Mawaziri wanaotuhumiwa ubadhirifu wamewekwa pale na Kikwete, sidhani kama Pinda ana mamlaka yoyote ya kuwafukuza kazi bila idhini ya rais. Sasa Pinda akijiuzulu ndiyo iweje? Imwachie mlango Kikwete kukwepa lawama na kumchagua swahiba wake Asha Rose Migiro? Nasikia anasubiria sana kiti hicho.

Nadhani Zitto alitoa ufafanuzi mzuri na tulio wengi tunakubaliana nao kwamba Pinda hana tatizo ila mawaziri waliotajwa wakiongozwa na waziri wa fedha ndio cancer ya nchi hii. Kwa vile bunge halina mamlaka dhidi ya mawaziri wengine wote ambao ni wateule wa rais akiwemo rais mwenye basi wakishindwa kujipima na kuwajibika wao watamwajibisha MP kwa vile wanamamlaka nae kwa vile walimpigia kura. Kwa hiyo mpira uko kwa Rais na mawaziri wenyewe kufanya maamuzi kwa kujiuzulu ama ang'olewe PM then baraza zima la mawaziri liwe limeng'oka automatically which will be very ridiculous decision from government.
Kwa upande mwingine ikifikia hatua ya PM kupigiwa kura ya NO CONFIDENCE itaathiri serikali iliyopo madarakani kwa kiwango kikubwa sana maana heshima yake itashuka na wananchi watapoteza imani na Rais kabisa.
Kazi ipo kwa JK kujipima sasa maana najua hapo Mvi nae anachekelea hiyo move maana ni wakati wake kujisafisha sasa na kurudisha imani kwa wananchi. Kwa hiyo kwa siku hz tatu hadi kufikia hiyo hatua Jumatatu taifa litakuwa linapitia kipindi kigumu sana kama JK atashindwa kuwawajibisha hao mawaziri na tutamjua fika ni mtu wa aina gani. Ila imani yangu kubwa katika kipindi cha bunge hapo baadae kuna mawaziri watakao bwaga manyaka kuiepusha serikali na aibu hii nzito.
 
Back
Top Bottom