Wabunge CCM wamsafisha Lowassa.

Gumzo

JF-Expert Member
Jan 2, 2012
211
7
Sakata hilo, lilibuka juzi usiku, katika kikao cha Wabunge wa CCM, ambacho kilikuwa kinajadili tatizo la umeme, hali iliyomfanya Mbunge wa Simanjiro, Christopher Ole Sendeka (CCM), kuibuka na na hoja ya kutaka viongozi wa wizara hiyo wawajibishwe.
Hoja ya Sendeka, ilimlenga Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo na Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Eliakim Maswi, wawajibishwe kwa kukiuka Sheria ya Manunuzi ya Umma.

Kwa mujibu wa chanzo cha kuaminika kutoka ndani ya kikao hicho, kilisema kuwa hoja hiyo ya Ole Sendeka, ilionekana ni mwiba kwake, hali iliyomfanya Mbunge wa Mwibara, Kangi Lugola (CCM), kunyanyuka na kumuumbua ole Sendeka.

Lugola, alisema alifuatwa na Ole Sendeka, huku akiahidi kumhonga fedha ili aweze kumuunga mkono hoja yake ya kutaka Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo na Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Eliachim Maswi, wawajibishwe na Bunge.

"Hoja ya Ole Sendeka, ilimfanya Kangi Lugola kunyanyuka na kuanza kutoa maelezo ambayo kulikuwa na lengo la kutaka kukwamisha bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini. Alipinga wazi kuwawajibisha viongozi wa wizara hiyo, huku akifananisha kinachotaka kufanywa ni sawa na lililomtokea Lowasa.

"Alisema katika ripoti ile ya kamati teule ya Bunge, ilipelekea kumwajibisha Lowassa na baada ya muda iligundulika ilijaa upotoshaji mwingi na kusisitiza katu wabunge hawapo tayari kurudia makosa ya mwaka 2008, ambapo vilitolewa vielelezo vya mitaani," alisema mtoa habari huyo.

Baada ya maelezo ya Lugola, naye Mbunge wa Same Mashariki, Anne Kilango (CCM), aliunga mkono hoja hiyo na kusema kuwa mwaka 2008, Bunge liliaminishwa Lowassa, alikuwa mhusika na Richmond, kutokana na jambo hilo kukosa ushahidi alitahadharisha kutorudiwa kwa makosa tena.

"Kilango, alisema wabunge waliamini alikula fedha kwa kulipwa na Richmond, lakini hakuna ukweli, hivyo hakuna sababu ya kumwajibisha Waziri wa Nishati wala Katibu Mkuu wake.

BOFYA HAPA KWA HABARI KAMILI GUMZO LA JIJI
 
Sakata hilo, lilibuka juzi usiku, katika kikao cha Wabunge wa CCM, ambacho kilikuwa kinajadili tatizo la umeme, hali iliyomfanya Mbunge wa Simanjiro, Christopher Ole Sendeka (CCM), kuibuka na na hoja ya kutaka viongozi wa wizara hiyo wawajibishwe.
Hoja ya Sendeka, ilimlenga Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo na Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Eliakim Maswi, wawajibishwe kwa kukiuka Sheria ya Manunuzi ya Umma.
Kwa mujibu wa chanzo cha kuaminika kutoka ndani ya kikao hicho, kilisema kuwa hoja hiyo ya Ole Sendeka, ilionekana ni mwiba kwake, hali iliyomfanya Mbunge wa Mwibara, Kangi Lugola (CCM), kunyanyuka na kumuumbua ole Sendeka.
Lugola, alisema alifuatwa na Ole Sendeka, huku akiahidi kumhonga fedha ili aweze kumuunga mkono hoja yake ya kutaka Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo na Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Eliachim Maswi, wawajibishwe na Bunge.
"Hoja ya Ole Sendeka, ilimfanya Kangi Lugola kunyanyuka na kuanza kutoa maelezo ambayo kulikuwa na lengo la kutaka kukwamisha bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini. Alipinga wazi kuwawajibisha viongozi wa wizara hiyo, huku akifananisha kinachotaka kufanywa ni sawa na lililomtokea Lowasa.
"Alisema katika ripoti ile ya kamati teule ya Bunge, ilipelekea kumwajibisha Lowassa na baada ya muda iligundulika ilijaa upotoshaji mwingi na kusisitiza katu wabunge hawapo tayari kurudia makosa ya mwaka 2008, ambapo vilitolewa vielelezo vya mitaani," alisema mtoa habari huyo.
Baada ya maelezo ya Lugola, naye Mbunge wa Same Mashariki, Anne Kilango (CCM), aliunga mkono hoja hiyo na kusema kuwa mwaka 2008, Bunge liliaminishwa Lowassa, alikuwa mhusika na Richmond, kutokana na jambo hilo kukosa ushahidi alitahadharisha kutorudiwa kwa makosa tena.
"Kilango, alisema wabunge waliamini alikula fedha kwa kulipwa na Richmond, lakini hakuna ukweli, hivyo hakuna sababu ya kumwajibisha Waziri wa Nishati wala Katibu Mkuu wake.

BOFYA HAPA KWA HABARI KAMILI GUMZO LA JIJI

Kwa wabunge wa CCM is OK, hakuna atakaye ona ajabu! Lakini wajue LOWASA si msafi hata kidogo!
 
HATIMAYE wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), wameibuka na kumsafisha Waziri Mkuu aliyejiuzulu, Edward Lowassa, huku wakidai taarifa ya Kamati teule iliyokuwa ikiongozwa na Waziri wa sasa wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe, ilijaa upotoshaji.

Yaani wanakumbuka shuka wakati kumekucha.
 
Hee kweli ccm imefika mwisho km lowasa sio fisadi...........yaani watu watatu (lowasa,rostam na kikwet) walijiundia kampuni feki na kujichotea milioni 155 kila siku mnasema hakuhusika?........du!...hii nchi ukifikiria sana unaweza kuwa kichaa ni bora kuvuta unga uwe teja yaani usiwe na akili timamu
 
Ubinafsi wa hao watu ndo unaoliangamiza taifa, lakini nafurahi kuwa wanazidi kujifuta kwenye mioyo ya Watanzania!!!!
 
Wamegundua hakuwa na kosa kwasababu aliamlishwa na Dr Dr Dr Kikwete au bado sijaelewa..
 
Ni ukweli uliyowazi kuwa kuondoka kwa Lowassa nchi imeshuhudia ombwe la utendaji kazi.Watanzania tuna tabia ya kusahau ya nyuma.Tukumbuke uwanja wa mnazi mmoja ulivyokuwa tayari umeuzwa kwa mwarabu, nani alichukua maamuzi magumu kuzuia na kuwaambia wananchi wachukue mabati yaliyokuwa yamezungushiwa.Nani alivunja mkataba mbovu wa dawasco.Nani alisimama kidete Umoja wa Mataifa kuhakikisha Tanzania inatumia maji ya Ziwa Viktoria, hadi Kenya, Uganda, Ethiopia nazo zinafuata mfano wa Tanzania, Shinyanga wanayaita maji ya Lowassa.Kwa dunia ya sasa, Tanzania inatakiwa kuongozwa na mijitu kama Lowassa haigopi kupitisha maamuzi
 
Magamba wameangalia kundini hawaoni wa kumsimamisha 2015 sasa wanaanza rasmi kumsafisga fisadi kuelekea 2015 kwa matumaini kwamba ikifika 2015 atakuwa msafi sana tena ananukia manukato na akitumia mabilioni yake aliyoyapata kifisadi basi itakuwa rahisi kuchakachua uchaguzi na yeye kutinga Ikulu. Kweli magamba hawajali kabisa maslahi ya nchi bali yale ya chama chao.
 
Magamba wameangalia kundini hawaoni wa kumsimamisha 2015 sasa wanaanza rasmi kumsafisga fisadi kuelekea 2015 kwa matumaini kwamba ikifika 2015 atakuwa msafi sana tena ananukia manukato na akitumia mabilioni yake aliyoyapata kifisadi basi itakuwa rahisi kuchakachua uchaguzi na yeye kutinga Ikulu. Kweli magamba hawajali kabisa maslahi ya nchi bali yale ya chama chao.

BAK, let's be honest.. hivi unajua kuwa asilimia 99.98 ya Wabunge wa CCM ni wabunge wa matumbo yao.. wana uhakika mkubwa wa kutorudi bungeni, na mbaya zaidi ni pale CCM ikikosa urais, kutoka madarakani, wanajua hata hivyo walivyojilimbikizia vitakuwa mashakani, ni lazima sasa hivi watabadirika wote na kuwa pamoja, ili wamuweke mtu atakaye weza kuwahakikishia CCM wanabaki madarakani. Kazi kubwa watanzania tunayo kuondokana na hili kundi la wezi.
 
wamesha msafisha amesafishika?????????,mana uchafu alionao hata akichunwa ngozi yake bado atakuwa lowasa fisadi.
 
zamani issue kama hii ungekuta anne kilango ni anaichachafya serikali lakini siku hizi kila hoja anaikubali sijui ni kanyamazishwa au na yeye yuko kwenye msururu wa hela za tanesco dah si mchezo
 
Hawa hakika wanapoteza muda wao. Wanachofanya ni sawa na kumfufua maiti jambo ambalo haliwezekani. Anyway, watakufa na Lowassa wao kama siyo CCM yao.
 
nimeona EL akiwa na vikao na wabunge ndani ya kikao cha bunge!naona wabunge wenzake wanamkubali
 
Ni ukweli uliyowazi kuwa kuondoka kwa Lowassa nchi imeshuhudia ombwe la utendaji kazi.Watanzania tuna tabia ya kusahau ya nyuma.Tukumbuke uwanja wa mnazi mmoja ulivyokuwa tayari umeuzwa kwa mwarabu, nani alichukua maamuzi magumu kuzuia na kuwaambia wananchi wachukue mabati yaliyokuwa yamezungushiwa.Nani alivunja mkataba mbovu wa dawasco.Nani alisimama kidete Umoja wa Mataifa kuhakikisha Tanzania inatumia maji ya Ziwa Viktoria, hadi Kenya, Uganda, Ethiopia nazo zinafuata mfano wa Tanzania, Shinyanga wanayaita maji ya Lowassa.Kwa dunia ya sasa, Tanzania inatakiwa kuongozwa na mijitu kama Lowassa haigopi kupitisha maamuzi

Nimeichukia sana CCM kwa uzembe na kutokuwajibika, hasa baada ya kuamua kunyonya wafanyakazi na upuuzi wa SSRA. hata hivyo, tukiacha zazba, nchi ijayo baada ya miaka hii mingi 2.5 (mingi kuliko umri wa uhuru) hivi iliyobaki ya JK, Nikiambiwa nitaje pendekezo la uzalendo na kuangalia mbele na hali tuliyonayo leo, na ukweli wa Mwanakata huu, pendekezo langu ni Zitto, Lowassa (Ubove wake sio sawa na faida zake, watendaji watawajibika, wizi wake kama -upo, ila riba yake sio sawa na asiye mwizi halafu hazalishi), wa tatu ni Dr Magufuli. Dr Slaa, mbowe, Sitta, mwakyembe, mwanry etc nawakubali ila wapewe wizara
 
Back
Top Bottom