Kansigo
JF-Expert Member
- Nov 4, 2010
- 2,670
- 2,156
Mh. Job Ndugai ameteuliwa kuwa mgombea rasmi wa nafasi ya Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha CCM.
Mbunge wa Kongwa na aliyekuwa naibu spika bunge la 10 lililoisha, Job Ndugai amepitishwa na kamati kuu ya chama cha mapinduzi kugombea nafasi ya uspika wa bunge la Jamhuri ya muungano wa Tanzania baada ya wagombea wengine wawili waliopitishwa mwanzo kujitoa.
==============
Mbunge wa Kongwa na aliyekuwa naibu spika bunge la 10 lililoisha, Job Ndugai amepitishwa na kamati kuu ya chama cha mapinduzi kugombea nafasi ya uspika wa bunge la Jamhuri ya muungano wa Tanzania baada ya wagombea wengine wawili waliopitishwa mwanzo kujitoa.
==============
Kamati Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) leo imemteua aliyekuwa naibu Spika wa Bunge la 10 Job Ndugai, kuwa mwakilishi wa chama hicho atakayegombea nafasi ya uspika wa bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ambaye atapigiwa kura na wabunge wa hapo kesho kuwania nafasi hiyo.
Kwa mujibu wa taarifa ya chama hicho iliyotolewa na Dodoma kupitia Katibu wa Itikadi na Unezi, Nape Nauye, amesema Dkt. Tulia Mwansasu na Mbunge wa Afrika Mashariki, Abdulla Ally Mwinyi waliamua kujitoa katika nafasi hiyo hivyo kumpa nafasi Job Ndugai kupita bila kupingwa.
Wakati mchakato wa kumpata mwakilishi atakayewakilisha vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) katika kinyang'anyiro cha nafasi ya uspika ukiendelea, imebainika kuwa Goodluck Ole Medeye, ndiye atakayesimama katika nafasi hiyo.
Ole Medeye, aliyewahi kuwa Mbunge wa Arumeru Magharibi kupitia CCM aliwahi pia kuwa Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya makazi katika utawala wa awamu ya nne wa Rais mstaafu Jakaya Kikwete (CCM), imeelezwa ndiye atakayewania nafasi hiyo.
Umoja wa Vyama unaofahamika kama Ukawa unaundwa na vyama vya Chadema, Chama cha Wananchi (CUF), NCCR-Mageuzi na NLD.
Soma zaidi =>Ndugai ateuliwa kuiwakilisha CCM Uspika
Last edited by a moderator: