Mwanafunzi mtoro
JF-Expert Member
- Aug 3, 2021
- 223
- 797
Chifu mangungo hakuwa mjinga, watanzania tulipotoshwa, tunapaswa kuiomba familia yake msamaha
Kwa miaka mingi sana chifu mangungo ameendelea kuonekana kama mfano wa kiongozi mjinga hasa pale linapotokea swala la mikataba. Lakini je Mangungo alikuwa mjinga kweli?
Chifu mangungo ni nani?
Naomba ninukuu kidogo kipande cha historia fupi kuhusu chifu Mangungo kutoka katika uzi wa ndugu humu Jf KILABA
"Mangungo simultaneously for all his people and Dr. Peters for alt his present and future associates hereby concluded a treaty of Eternal Friendship.
Mangungo offers all his territory with all its civil appurtenances to Dr. Karl Peters, as the representative of the Society for German Colonization, for the exclusive and universal utilization for German colonization.
Dr. Karl Peters, in the name of the Society for German Colonization declares his willingness to take over the territory of the Sultan Mangungo with all rights for German Colonization subject to any existing suzerainty of Mwenyi Sagara.
In pursuance thereof, Sultan Mangungo hereby cedes all the territory of Msovero, belonging to him by inheritance or otherwise for all time, to Dr. Karl Peters, making over to him at the same time all his rights.
Dr. Karl Peters in the name of the Society for German Colonization undertakes to give special...attention to Msovero when colonizing Usagara.
This treaty has been communicated to the Sultan Mangungo by the interpreter Ramzan in a clear manner and has been signed by both sides, with the observation of the formalities valid in Usagara the Sultan on direct enquiry having declared that he was not in anyway dependent upon the Sultan of Zanzibar, and that he did not even know the existence of the latter.
Sgd. Dr. KARL PETERS
Sgd. MANGUNGO
This contract has been executed legally and made valid for all time before a great number of witnesses, we testify herewith:
Kwagakinga (mark);
Sultan Mangungo’s son of Golola (mark);
Sultan Mangungo’s second son of Draman (mark);
Graf Pfeil August Otto;
Mark of the intepreter Ramazan etc.
Dr. Karl Juhlke.
Msovero Usagara November 29, 1884.
Kwa tafsiri isiyo rasmi, kwa Kiswahili unasomeka hivi:
Mangungo, Sultan wa Msovero katika Mwenyisagara, na Dk. Karl Peters. Mangungo sambamba na watu wake wote na Dk. Peters kwa niaba yake na washirika wake wengine wajao kwa pamoja wanaweka mkataba wa Urafiki wa Kudumu.
Mangungo amekubali kutoa himaya yake yote pamoja na watu wake na hadhi yake kwa Dk. Karl Peters, kama mwakilishi wa Umoja wa Ukoloni wa Kijerumani (Society for German Colonization), kwa ajili ya matumizi ya moja kwa moja ya koloni la Kijerumani.
Dk. Karl Peters, kwa niaba ya jina la Umoja wa Ukoloni wa Ujermani anatangaza dhamira yake ya kuitwaa himaya yote ya Sultan Mangungo na haki zote kwa ajili ya Koloni la Ujerumani inayohusisha kila kona na amali za Mwenyi Sagara.
Katika kutekeleza hilo, Sultan Mangungo anakabidhi himaya yote ya Msovero, inayomilikiwa na yeye mwenyewe kwa urithi au kwa namna yoyote ile kwa nyakati zote, kwa Dk. Karl Peters, na wakati huo huo kumkabidhi haki zake zote.
Dk. Karl Peters kwa niaba ya Umoja wa Ukoloni wa Kijerumani anakusudia kuweka mkazo maalum kwa eneo la Msovero wakati wa kuitawala Usagara.
Mkataba huu umewasilishwa kwa Sultan Mangungo na mkalimani Ramzan katika dhana ya wazi kabisa na umesainiwa na pande zote, kwa kuzingatia taratibu zilizopo katika Usagara, Sultan baada ya kuhojiwa moja kwa moja alikiri kwamba hakuwa na ushirika ama kutegemea kwa namna yoyote Sultan wa Zanzibar, na kwamba hakuwa hata akimfahamu.
Imesainiwa. Dk. KARL PETERS
Imesainiwa. MANGUNGO
Mkataba huu umefanyika kihalali kabisa na umehuishwa kwa nyakati zote mbele za mashahidi wengi, ambao tunakiri hapa:
Kwagakinga (dole gumba);
Golola mtoto wa Sultan Mangungo (dole gumba);
Draman mtoto wa pili wa Sultan Mangungo (dole gumba);
Graf Pfeil August Otto.
Dole gumba la mkalimani Ramazan etc.
Dk. Karl Juhlke.
Msovero Usagara Novemba 29, 1884.
KWANINI MANGUNGO ALIONEKANA MJINGA?
Historia ilipoandikwa baada ya kupata uhuru , iliwahesabu watu wote waliopambana na wazungu kama mashujaa mfano Mkwawa. Bila kujali utawala wa hao machifu kama ulikuwa wa haki au laa. Historia haikutazama watawala hawa machifu kama watu walio pambania madaraka yao bali inawahesabu kama mashujaa kwa kuwa ilipambana tu mzungu.
Baada ya uhuru watu walisoma hadithi kama "KIBANGA AMPIGA MKOLONI". waliosoma kwa kipindi hicho walimuona Kibanga kama shujaa kwa kumpiga mzungu ( mkoloni). Lakini je Kibanga wa mwaka 1960 bado ni shujaa leo hii au ataonekana anafukuza "WAWEKEZAJI" ?
Kwahiyo kama KIBANGA alionekana shujaa kwa kumpinga mkoloni kipindi cha kutaka kujitawala ni wazi historia yoyote iliyoandikwa kwa kipindi hiko ingemtazama mtu yeyote yule aliyeshirikiana na wakoloni kipindi wanaingia Afrika kama mtu mjinga na msaliti kwa jamii yake.
KWANINI NASEMA MANGUNGO SIO MJINGA?
Kilichotokea kati ya Mangungo na machifu wengine waliopigana na wazungu ni uelewa tu. Mangungo aliona mbali ambapo wengine hawakuona kwa kipindi kile. MANGUNGO aliwaona wazungu kama wawekezaji mapema sana kuliko machifu wenzake. Kile alichokifanya Mangungo kuwaona wazungu kama wawekezaji ndio hiki tunakiona leo na sisi kuwa wazungu wanauwezo wa kuwekeza katika nchi zetu za kiafrika na uchumi ukakua.
JE MANGUNGO ALIAHIDIWA NINI KWA WAZUNGU?
Binafsi naamini tofauti na mkataba wa kuichukua ardhi na kiutawala tunaoambiwa kuwa ndio huo MANGUNGO alisaini lakini inaonesha wazi kwamba Mangungo alielezwa kuwa kama wazungu watalichukua eneo basi watakuja na mamba yafuatayo ;
mashine ( matreka) za kilimo kama treka nk
Ujenzi wa hospital za kisasa kwa (kipindi hicho)
Ujenzi wa shule
Ujenzi wa maghala ya kuhifadhia chakula
Ujenzi wa barabara
Ujenzi wa mabwawa ya kuzalisha umeme
Ujenzi wa reli ya kisasa kwa wakati huo
Ujenzi wa madaraja katika maeneo yasiyopitika kipindi cha masika
Upatikanaji wa huduma za maji safi .
Je upi unaweza kuwa uthibitisho wa hizo ahadi hadi kupelekea MANGUNGO kukubali?
Ukilitazama vizuri hilo eneo la Msovero ambalo ndio inaelezwa kuchukua eneo kubwa la KILOSA ya leo utagundua yafuatayo.
Maeneo mengi ya wilaya hiyo yana mashamba makubwa ya mkonge yaliyolimwa na mwekezaji wa Mangungo. Kuanzia Msowero ya leo , Gairo, Kimamba, Ludewa, Kilosa mjini ya leo, Chanzuru, Kivungu, Zombo , Mikumi, Kilangali , Malangali ,Ngaite, Melela Mvomero inayopakana na kilosa , ILONGA had maeneo ya dumila nk
Hayo ni maeneo machache sana yanayoonesha mwekezaji alitekeleza kweli ahadi yake ya kuinua kilimo.
Maeneo ya Kilosa mengi yalijegwa hospital. Mfano hospital ya Kilosa , Kimamba , vituo vya afya kama maeneo ya Ludewa , Mkata , na vingine ambavyo vilijegwa na wajerumani . Hivyo vitu havikuwepo kabla ya mkataba wa MANGUNGO.
Uwepo wa barabara kama ya kutoka Kilosa hadi Mikumi kupitia Zombo, barabara ya kutoka Kilosa hadi Morogoro mjini kupitia Mkata na ile kupitia Ludewa ni ushahidi tosha kuwa mwekezaji alifanya yale aliyoahidi mbele ya chifu Mangungo.
Uwepo wa njia ya reli inayopita tokea Morogoro mjini pale kichangani na kupita maeneo kama Mkata, Kimamba, Kilosa mjini ya sasa, Mkadage huko hadi Pwaga na kuingia Mpwapwa hii inaonedha jinsi gani mkataba wa chifu Mangungo na machifu wa kiluguru na wa kizingua ulizaa matunda kwa maeneo yao kiuwekezaji.
Uwepo wa shule ya KIZUNGUZI (kizu boys)
Ajira kwa vijana Uwepo wa huduma za malazi kwa wafanyakazi. Ajira ilipatikana kwa manamba japo mshahara haukuwa mkubwa lakini ukibadili thamani ya mshahara wa kipindi hicho unafanana na baadhi ya mishahara ya baadhi ya watu wanaolipwa hivi leo. Si kwamba hata hivi leo watu hawalalamiki udogo wa mishahara.
Nyumba za watumishi zilijegwa kila kwenye stesheni , kwenye kila kituo chao cha kukusanyia mikonge mfano Kimamba, ludewa , Chanzuru Msiwero , Kivungu nk. Hapa inaonesha ni jinsi gani mkataba aliosaini abwana mangungo haukuwa mbaya kama tunavyoaminishana leo hii.
Bado kama hayo hayatoshi ukipita maeneo ya Ilonga utaona jinsi wajerumani walivyopaendeleza katika kilimo na vituo vya utafiti wa kilimo walijenga ( hapa mtanikosoa kama walijenga wajerumani au waingereza).
Kwa wale watu walio bahatika kuishi Sagara ya zamani au Kilosa ya leo wanaweza kuwa mashahidi . Mji wa kilosa wa leo unaoneka ni mji uliokuwa wa kifahari enzi ya wawekezaji wa Mangungo ( ambao waliitwa wakoloni hapo awali) kabla ya kubadilishwa jina tena na kuitwa wawekezaji kama alivyowaita Mangungo na kizazi cha sasa . Kilosa ulikuwa mji kimbilio la wageni toka mikoa mbali mbali Tanzania. Usifikiri katika "engo" ya manamba kupata mchanganyiko wa kabila katika eneo la kilosa bali hata huduma ziliwavuta vijana wa zamani kwenda kuishi Kilosa.
Je kunyonywa kiuchumi ndio kunatufanya tumuone Mangungo alikuwa mjinga?
Binafsi namuona Bwana Mangungo kama kiongozi aliyeuona uwekezaji tangu mapema. Kwani kama kuhusu kunyonywa bado hadi leo kama taifa bado tuna mikataba mingi ya kinyonyaji isiyoacha alama kwa taifa kuliko ile ya msovero iliyoacha hata reli ,magofu ya nyumba na hospital.
Wapo watakaosema ujinga wa Mangungo ni kuiachia ardhi kwa wazungu kulima pamba na mikonge huku wenyeji kuishi kwa njaa. Binafsi naamini kwa nyakati hizo kulikuwa na watu wachache sana wenye uwezo wa kulima mamia ya ekari kama wawekezaji. Wengi walilima kujikimu kwani ni miaka zaidi ya 70s sasa tangu Mzungu atuachie ardhi yetu lakini kuna maeneo tangu kuumbwa kwa dunia hayajawahi kulimwa na wazawa. Vijana wanashinda kwenye vituo vya kubeti huku redio zikihamasisha nguvu ya buku katika kushinda kamali. Kwa mawazo kama hayo hatuoni kama bwana Mangungo aluoba mbali kuingia mikataba na wawekezaji?
Wapo watakaosema ujinga ni kuwa alisaini bila kuelewa chochote . Binafsi naona si kweli, kwani kama ni kweli Mangungo alisaini kitu asichoelewa historia ingeonesha kutokea mgogoro baina ya mwekezaji na Mangungo. Katika hali ya kawaida mtu akwambie muingie makubaliano ya kulichukua eneo lako lote la ardi na kiutawala na ukakubali bila kumuuliza shughuri atakazofanyia eneo lako. Pili, mkata ulisainiwa kisha Karl na wenzake wakaondoka kurudi Ujerumani . Kama wangekuwa ni walaghai basi pale waliporudi kutekeleza uwekezaji wao lazima pangetokea ugomvi na kutoelewana. Maana katika hali ya kawaida ukimpa mtu eneo alime au akae alafu ghafla unamwona anakuja na fundi wake wanajenga nyumba , hospitali, reli bila kwenda kuwahoji.
MANGUNGO ALIKUWA KIONGOZI MWANADIPLOMASIA
Kwajinsi sasa jamii ya Kiafrika inavyomsifu kiongozi mwenye mahusiano mazuri na wazungu kama kiongozi bora na mwanadiplomasia basi ni wazi Mangungo alikuwa nguli zaidi kama mwanadiplomasia wa mwanzoni kabisa.
NINI WITO WANGU KWA JAMII
Niwakati sasa wa jamii yetu kubadili mtazamo juu ya chifu Mangungo kwa kumchukulia kama kiongozi mjinga na kumwona kama kiongozi wa mwanzoni kuhamasisha uwekezaji nchini. Kumwona Mangungo kama kiongozi mjinga kumeifanya hata familia yake isijulikane leo hii ksma zinavyojulikana familia za ma chifu wengine. Kwakuwa sasa viongozi wetu wamerudi kule kule kuwapokea wazungu na kufanya nao shughuri za maendeleo kama ujenzi wa miundombinu ya maji , barabara, reli, hospitali, na shule jambo ambalo hata Mangungo ndilo alilifanya kwa ustadi basi hatuna budi kumuenzi Mangungo kama mwasisi wa uwekezaji nchini.
Natamani sasa hata familia yake iliyobaki tuiombe msamaha kama taifa kwakuwa tulilewa mvinyo wa uhuru kiasi ya kuwaona waliopinga kushirikiana na wazungu kuwa ndio MASHUJAA.
Nawasaliim
Kwa miaka mingi sana chifu mangungo ameendelea kuonekana kama mfano wa kiongozi mjinga hasa pale linapotokea swala la mikataba. Lakini je Mangungo alikuwa mjinga kweli?
Chifu mangungo ni nani?
Naomba ninukuu kidogo kipande cha historia fupi kuhusu chifu Mangungo kutoka katika uzi wa ndugu humu Jf KILABA
"Mangungo simultaneously for all his people and Dr. Peters for alt his present and future associates hereby concluded a treaty of Eternal Friendship.
Mangungo offers all his territory with all its civil appurtenances to Dr. Karl Peters, as the representative of the Society for German Colonization, for the exclusive and universal utilization for German colonization.
Dr. Karl Peters, in the name of the Society for German Colonization declares his willingness to take over the territory of the Sultan Mangungo with all rights for German Colonization subject to any existing suzerainty of Mwenyi Sagara.
In pursuance thereof, Sultan Mangungo hereby cedes all the territory of Msovero, belonging to him by inheritance or otherwise for all time, to Dr. Karl Peters, making over to him at the same time all his rights.
Dr. Karl Peters in the name of the Society for German Colonization undertakes to give special...attention to Msovero when colonizing Usagara.
This treaty has been communicated to the Sultan Mangungo by the interpreter Ramzan in a clear manner and has been signed by both sides, with the observation of the formalities valid in Usagara the Sultan on direct enquiry having declared that he was not in anyway dependent upon the Sultan of Zanzibar, and that he did not even know the existence of the latter.
Sgd. Dr. KARL PETERS
Sgd. MANGUNGO
This contract has been executed legally and made valid for all time before a great number of witnesses, we testify herewith:
Kwagakinga (mark);
Sultan Mangungo’s son of Golola (mark);
Sultan Mangungo’s second son of Draman (mark);
Graf Pfeil August Otto;
Mark of the intepreter Ramazan etc.
Dr. Karl Juhlke.
Msovero Usagara November 29, 1884.
Kwa tafsiri isiyo rasmi, kwa Kiswahili unasomeka hivi:
Mangungo, Sultan wa Msovero katika Mwenyisagara, na Dk. Karl Peters. Mangungo sambamba na watu wake wote na Dk. Peters kwa niaba yake na washirika wake wengine wajao kwa pamoja wanaweka mkataba wa Urafiki wa Kudumu.
Mangungo amekubali kutoa himaya yake yote pamoja na watu wake na hadhi yake kwa Dk. Karl Peters, kama mwakilishi wa Umoja wa Ukoloni wa Kijerumani (Society for German Colonization), kwa ajili ya matumizi ya moja kwa moja ya koloni la Kijerumani.
Dk. Karl Peters, kwa niaba ya jina la Umoja wa Ukoloni wa Ujermani anatangaza dhamira yake ya kuitwaa himaya yote ya Sultan Mangungo na haki zote kwa ajili ya Koloni la Ujerumani inayohusisha kila kona na amali za Mwenyi Sagara.
Katika kutekeleza hilo, Sultan Mangungo anakabidhi himaya yote ya Msovero, inayomilikiwa na yeye mwenyewe kwa urithi au kwa namna yoyote ile kwa nyakati zote, kwa Dk. Karl Peters, na wakati huo huo kumkabidhi haki zake zote.
Dk. Karl Peters kwa niaba ya Umoja wa Ukoloni wa Kijerumani anakusudia kuweka mkazo maalum kwa eneo la Msovero wakati wa kuitawala Usagara.
Mkataba huu umewasilishwa kwa Sultan Mangungo na mkalimani Ramzan katika dhana ya wazi kabisa na umesainiwa na pande zote, kwa kuzingatia taratibu zilizopo katika Usagara, Sultan baada ya kuhojiwa moja kwa moja alikiri kwamba hakuwa na ushirika ama kutegemea kwa namna yoyote Sultan wa Zanzibar, na kwamba hakuwa hata akimfahamu.
Imesainiwa. Dk. KARL PETERS
Imesainiwa. MANGUNGO
Mkataba huu umefanyika kihalali kabisa na umehuishwa kwa nyakati zote mbele za mashahidi wengi, ambao tunakiri hapa:
Kwagakinga (dole gumba);
Golola mtoto wa Sultan Mangungo (dole gumba);
Draman mtoto wa pili wa Sultan Mangungo (dole gumba);
Graf Pfeil August Otto.
Dole gumba la mkalimani Ramazan etc.
Dk. Karl Juhlke.
Msovero Usagara Novemba 29, 1884.
KWANINI MANGUNGO ALIONEKANA MJINGA?
Historia ilipoandikwa baada ya kupata uhuru , iliwahesabu watu wote waliopambana na wazungu kama mashujaa mfano Mkwawa. Bila kujali utawala wa hao machifu kama ulikuwa wa haki au laa. Historia haikutazama watawala hawa machifu kama watu walio pambania madaraka yao bali inawahesabu kama mashujaa kwa kuwa ilipambana tu mzungu.
Baada ya uhuru watu walisoma hadithi kama "KIBANGA AMPIGA MKOLONI". waliosoma kwa kipindi hicho walimuona Kibanga kama shujaa kwa kumpiga mzungu ( mkoloni). Lakini je Kibanga wa mwaka 1960 bado ni shujaa leo hii au ataonekana anafukuza "WAWEKEZAJI" ?
Kwahiyo kama KIBANGA alionekana shujaa kwa kumpinga mkoloni kipindi cha kutaka kujitawala ni wazi historia yoyote iliyoandikwa kwa kipindi hiko ingemtazama mtu yeyote yule aliyeshirikiana na wakoloni kipindi wanaingia Afrika kama mtu mjinga na msaliti kwa jamii yake.
KWANINI NASEMA MANGUNGO SIO MJINGA?
Kilichotokea kati ya Mangungo na machifu wengine waliopigana na wazungu ni uelewa tu. Mangungo aliona mbali ambapo wengine hawakuona kwa kipindi kile. MANGUNGO aliwaona wazungu kama wawekezaji mapema sana kuliko machifu wenzake. Kile alichokifanya Mangungo kuwaona wazungu kama wawekezaji ndio hiki tunakiona leo na sisi kuwa wazungu wanauwezo wa kuwekeza katika nchi zetu za kiafrika na uchumi ukakua.
JE MANGUNGO ALIAHIDIWA NINI KWA WAZUNGU?
Binafsi naamini tofauti na mkataba wa kuichukua ardhi na kiutawala tunaoambiwa kuwa ndio huo MANGUNGO alisaini lakini inaonesha wazi kwamba Mangungo alielezwa kuwa kama wazungu watalichukua eneo basi watakuja na mamba yafuatayo ;
mashine ( matreka) za kilimo kama treka nk
Ujenzi wa hospital za kisasa kwa (kipindi hicho)
Ujenzi wa shule
Ujenzi wa maghala ya kuhifadhia chakula
Ujenzi wa barabara
Ujenzi wa mabwawa ya kuzalisha umeme
Ujenzi wa reli ya kisasa kwa wakati huo
Ujenzi wa madaraja katika maeneo yasiyopitika kipindi cha masika
Upatikanaji wa huduma za maji safi .
Je upi unaweza kuwa uthibitisho wa hizo ahadi hadi kupelekea MANGUNGO kukubali?
Ukilitazama vizuri hilo eneo la Msovero ambalo ndio inaelezwa kuchukua eneo kubwa la KILOSA ya leo utagundua yafuatayo.
Maeneo mengi ya wilaya hiyo yana mashamba makubwa ya mkonge yaliyolimwa na mwekezaji wa Mangungo. Kuanzia Msowero ya leo , Gairo, Kimamba, Ludewa, Kilosa mjini ya leo, Chanzuru, Kivungu, Zombo , Mikumi, Kilangali , Malangali ,Ngaite, Melela Mvomero inayopakana na kilosa , ILONGA had maeneo ya dumila nk
Hayo ni maeneo machache sana yanayoonesha mwekezaji alitekeleza kweli ahadi yake ya kuinua kilimo.
Maeneo ya Kilosa mengi yalijegwa hospital. Mfano hospital ya Kilosa , Kimamba , vituo vya afya kama maeneo ya Ludewa , Mkata , na vingine ambavyo vilijegwa na wajerumani . Hivyo vitu havikuwepo kabla ya mkataba wa MANGUNGO.
Uwepo wa barabara kama ya kutoka Kilosa hadi Mikumi kupitia Zombo, barabara ya kutoka Kilosa hadi Morogoro mjini kupitia Mkata na ile kupitia Ludewa ni ushahidi tosha kuwa mwekezaji alifanya yale aliyoahidi mbele ya chifu Mangungo.
Uwepo wa njia ya reli inayopita tokea Morogoro mjini pale kichangani na kupita maeneo kama Mkata, Kimamba, Kilosa mjini ya sasa, Mkadage huko hadi Pwaga na kuingia Mpwapwa hii inaonedha jinsi gani mkataba wa chifu Mangungo na machifu wa kiluguru na wa kizingua ulizaa matunda kwa maeneo yao kiuwekezaji.
Uwepo wa shule ya KIZUNGUZI (kizu boys)
Ajira kwa vijana Uwepo wa huduma za malazi kwa wafanyakazi. Ajira ilipatikana kwa manamba japo mshahara haukuwa mkubwa lakini ukibadili thamani ya mshahara wa kipindi hicho unafanana na baadhi ya mishahara ya baadhi ya watu wanaolipwa hivi leo. Si kwamba hata hivi leo watu hawalalamiki udogo wa mishahara.
Nyumba za watumishi zilijegwa kila kwenye stesheni , kwenye kila kituo chao cha kukusanyia mikonge mfano Kimamba, ludewa , Chanzuru Msiwero , Kivungu nk. Hapa inaonesha ni jinsi gani mkataba aliosaini abwana mangungo haukuwa mbaya kama tunavyoaminishana leo hii.
Bado kama hayo hayatoshi ukipita maeneo ya Ilonga utaona jinsi wajerumani walivyopaendeleza katika kilimo na vituo vya utafiti wa kilimo walijenga ( hapa mtanikosoa kama walijenga wajerumani au waingereza).
Kwa wale watu walio bahatika kuishi Sagara ya zamani au Kilosa ya leo wanaweza kuwa mashahidi . Mji wa kilosa wa leo unaoneka ni mji uliokuwa wa kifahari enzi ya wawekezaji wa Mangungo ( ambao waliitwa wakoloni hapo awali) kabla ya kubadilishwa jina tena na kuitwa wawekezaji kama alivyowaita Mangungo na kizazi cha sasa . Kilosa ulikuwa mji kimbilio la wageni toka mikoa mbali mbali Tanzania. Usifikiri katika "engo" ya manamba kupata mchanganyiko wa kabila katika eneo la kilosa bali hata huduma ziliwavuta vijana wa zamani kwenda kuishi Kilosa.
Je kunyonywa kiuchumi ndio kunatufanya tumuone Mangungo alikuwa mjinga?
Binafsi namuona Bwana Mangungo kama kiongozi aliyeuona uwekezaji tangu mapema. Kwani kama kuhusu kunyonywa bado hadi leo kama taifa bado tuna mikataba mingi ya kinyonyaji isiyoacha alama kwa taifa kuliko ile ya msovero iliyoacha hata reli ,magofu ya nyumba na hospital.
Wapo watakaosema ujinga wa Mangungo ni kuiachia ardhi kwa wazungu kulima pamba na mikonge huku wenyeji kuishi kwa njaa. Binafsi naamini kwa nyakati hizo kulikuwa na watu wachache sana wenye uwezo wa kulima mamia ya ekari kama wawekezaji. Wengi walilima kujikimu kwani ni miaka zaidi ya 70s sasa tangu Mzungu atuachie ardhi yetu lakini kuna maeneo tangu kuumbwa kwa dunia hayajawahi kulimwa na wazawa. Vijana wanashinda kwenye vituo vya kubeti huku redio zikihamasisha nguvu ya buku katika kushinda kamali. Kwa mawazo kama hayo hatuoni kama bwana Mangungo aluoba mbali kuingia mikataba na wawekezaji?
Wapo watakaosema ujinga ni kuwa alisaini bila kuelewa chochote . Binafsi naona si kweli, kwani kama ni kweli Mangungo alisaini kitu asichoelewa historia ingeonesha kutokea mgogoro baina ya mwekezaji na Mangungo. Katika hali ya kawaida mtu akwambie muingie makubaliano ya kulichukua eneo lako lote la ardi na kiutawala na ukakubali bila kumuuliza shughuri atakazofanyia eneo lako. Pili, mkata ulisainiwa kisha Karl na wenzake wakaondoka kurudi Ujerumani . Kama wangekuwa ni walaghai basi pale waliporudi kutekeleza uwekezaji wao lazima pangetokea ugomvi na kutoelewana. Maana katika hali ya kawaida ukimpa mtu eneo alime au akae alafu ghafla unamwona anakuja na fundi wake wanajenga nyumba , hospitali, reli bila kwenda kuwahoji.
MANGUNGO ALIKUWA KIONGOZI MWANADIPLOMASIA
Kwajinsi sasa jamii ya Kiafrika inavyomsifu kiongozi mwenye mahusiano mazuri na wazungu kama kiongozi bora na mwanadiplomasia basi ni wazi Mangungo alikuwa nguli zaidi kama mwanadiplomasia wa mwanzoni kabisa.
NINI WITO WANGU KWA JAMII
Niwakati sasa wa jamii yetu kubadili mtazamo juu ya chifu Mangungo kwa kumchukulia kama kiongozi mjinga na kumwona kama kiongozi wa mwanzoni kuhamasisha uwekezaji nchini. Kumwona Mangungo kama kiongozi mjinga kumeifanya hata familia yake isijulikane leo hii ksma zinavyojulikana familia za ma chifu wengine. Kwakuwa sasa viongozi wetu wamerudi kule kule kuwapokea wazungu na kufanya nao shughuri za maendeleo kama ujenzi wa miundombinu ya maji , barabara, reli, hospitali, na shule jambo ambalo hata Mangungo ndilo alilifanya kwa ustadi basi hatuna budi kumuenzi Mangungo kama mwasisi wa uwekezaji nchini.
Natamani sasa hata familia yake iliyobaki tuiombe msamaha kama taifa kwakuwa tulilewa mvinyo wa uhuru kiasi ya kuwaona waliopinga kushirikiana na wazungu kuwa ndio MASHUJAA.
Nawasaliim